• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Waziri Jaffo awataka TBA kukamilisha jengo la utawala na kuanza kutumika Jan 2019

Posted on: September 12th, 2018

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo amewataka wakala wa ujenzi nchini ( TBA)  kuongeza kasi ya ujenzi wa jengo la utawala  la Manispaa ya Kigamboni kwani muda wa awali waliokubaliana katika mkataba unakaribia kwisha huku wakiwa bado wako katika kiwango cha chini ya asilimia hamsini.

Agizo hilo amelitoa alipotembelea ujenzi wa ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigambano linalojengwa na wakala wa Majengo nchini (TBA) katika eneo la Geza ulole kata ya Somangila, ambapo Mhe.Jaffo amemwagiza mkurugenzi  kuhakikisha anahamia katika ofisi hiyo  ifikapo Januari 2019.

Wakati huohuo Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo amepongeza upanuzi wa kituo cha Afya cha Kimbiji kinachojengwa kutokana na fedha zilizotolewa na ofisi yake katika mpango wa uboreshaji wa huduma za afya nchini.

Mhe. Jaffo amepongeza hatua iliyofikiwa huku akisisitiza ujenzi huo kukamilika ili wananchi waweze kupata huduma iliyotarajiwa na kusema kuwa kwa sasa ofisi yake ipo  katika hatua ya kusambaza vifaa katika vituo hivyo ambapo kwa Kimbiji baadhi ya vifaa vimeshapokelewa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe. Paul Makonda amempongeza Mh. Jaffo kwa jitihada zinazofanywa na ofisi yake katika kuboresha sekta ya Afya nchini kwani katika mkoa wa Dar es Salaam zaidi ya vituo kumi vipo katika mpango huo katika awamu ya kwanza na ya pili.

''Mhe.Waziri, kazi inayofanywa na ofisi yako ni kubwa sana na baada ya muda mfupi wananchi wangu wataanza kunufaika na maboresho haya na kuona matunda ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe.Dr.John Pombe Magufuli" alisema Mhe. amakonda.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ndg Ng'wilabuzu Ndatwa Ludigija amesema ofisi yake itaendelea kusimamia maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri ikiwa ni pamoja na kuanza upanuzi wa kituo cha Afya cha Kigamboni ambacho mpaka sasa ofisi yake imeshapokea shilingi milioni mia nne kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI.

Katika kituo cha Afya Kimbiji upanuzi umefanyika katika ujenzi wa chumba cha upasuaji, wodi ya akina mama , maabara pamoja na chumba cha kuhifadhia maiti ambavyo vyote kwa pamoja vitagarimu jumla ya shilingi milioni

Wazir wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Jaffo amefanya ziara ya kutembelea  miradi ya maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya Kimbiji na ujenzi wa jengo la utawala akiwa ameambatana na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na uongozi wa Kigamboni kuanzia ngazi ya Wilaya.

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Suleiman Jaffo akizungumza na uongozi wa manispaa ya Kigamboni

Viongozi wakitembelea jengo la utawala

Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Sulleiman Jaffo kushoto na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Paul Makonda wakikagua jengo la utawala linalojengwa na TBA


Waziri Jaffo na viongozi wengine wakisikiliza maelekezo ya msisamizi wa ujenzi wa jengo la utawala kutoka TBA(aliyeshika kofia)

Viongozi wakitembelea kuangalia ujenzi wa kituo cha afya Kimbiji

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Suleiman Jaffo akipongeza uongozi kwa ujenzi wa kituo hicho.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa