Kamati ya Mipango Miji na Mazingira:
Majukumu ya jumla
Kamati hii itashughulikia masuala ya uzalishaji mali ikiwemo kilimo, mifugo, viwanda, madini, Biashara n.k. Aidha itashughulikia pia miundombinu na suala zima la mendeleo ya Ardhi na hifadhi ya mazingira.
Majukumu maalum ya Kamati;
(i)Kupendekeza kwa Halmashauri mipango ya kupanua biashara na jinsi ya kukusanya mapato yatokanayo na upanuzi huo.
(ii)Kupendekeza mipango ya matumizi ya ardhi katika eneo la Halmashauri.
(iii)Kusimamia matumizi ya Sheria ya nguvu kazi.
(iv)Kuandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya upanuzi wa kilimo katika Halmashauri
(v)Kusimamia na kuhakiki miradi ya ujenzi wa masoko, minada, majosho na vituo vya mifugo.
(vi)Kushughulikia uanzishaji na uendelezaji wa vyama vya ushirika kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika.
|
|
|
|
Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni
Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam
Simu: +255222928468
Simu ya Mkononi: +255222928468
Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz
Haki MilikiĀ©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa