• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

WATUMISHI MANISPAA YA KIGAMBONI WATAKIWA KUFUATA SHERIA NA KANUNI KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO

Posted on: June 22nd, 2022

WATUMISHI MANISPAA YA KIGAMBONI WATAKIWA KUFUATA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEJELEZAJI WA MAJUKUMU YAO


Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Ndg.Erasto Kiwale amewataka watumishi wa Manispaa hiyo kufuata Sheria na Kanuni katika kutekeleza wajibu wao.Akiongea katika Mkutano uliofanyika Leo wa uongozi wa Manispaa hiyo na watumishi wote uliokuwa na lengo la kusikiliza changamoto mbalimbali za watumishi ili ziweze kutatuliwa.


 Ndg.Kiwale amesema kuna kanuni na Sheria ambazo kwa vyovyote vile mtumishi anatakiwa na anawajibika kuzifuata kwani ndio muongozo wa utekelezaji wa majukumu katika eneo la kazi akitolea mfano kanuni ya Kuwahi kufika kazini kwa wakati ni kanuni ambayo kila mtumishi anatakiwa atekeleze na kufika kufanya majukumu yake ili kuepuka kuvunja kanuni hiyo.Akiongelea suala la kufika kazini kwa wakati amesema kila mtumishi ana wajibu wa Kuwahi kufika kazini kwa wakati ,muda wa kufika kazini umeweka kisheria,hivyo mtumishi hatakiwi kufika muda anaoutaka yeye.


Pia amesisitiza mfumo rafiki kati ya wakuu wa idara wakati  ambapo mtumishi anaomba ufafanuzi kuhusu Jambo au anapompelekea shida inayohitaji utatuzi ili kufanya eneo la kazi kuwa sehemu salama na penye Amani, pia amesisitiza  suala la watumishi kuwahudumia wananchi wanaokuja kufata huduma kwa weledi bila kuwanyanyasa au kutumia lugha mbaya.


"Katika utekelezaji wa majukumu yenu kuna kanuni zinazowaongoza ambazo mnawajibika kuzifuata na si kuzikwepa ili kuwe na ufanisi,usalama na Amani katika eneo la kazi hivyo hamna budi kuzifuata."alisema ndg.Erasto Kiwale.


Nae Afisa Utumishi Mkuu Bi.Florah Malima  akiongelea suala la kufata utaratibu na kanuni katika utekelezaji wa majukumu katika mengi aliyoongelea amegusia pia suala la utaratibu wa kuombabkibali cha malipo ya masaa ya ziada ambapo amesema Mkuu wa Idara ana wajibu wa kuomba kibali pale ambapo anajua kutakuwa na kazi itakayowataka watumishi katika idara yake kufanya kazi katika muda wa ziada ili kuweza kufuata utaratibu wa kuwaimbea stahiki zao wale watakaofanya kazi hizo nje ya muda wa kazi na si kuamua tu bila kufuata utaratibu ulioelekezwa.


Akiongea Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Mkoa Bi.Shamila Hassan wa TALGU ambao walialikwa kwenye Mkutano huo wamempongeza Mkurugenzi kwa utaratibu huu aliojiwekea wa kukutana na watumishi wa Manispaa yake kwa ajili ya kusikiliza changamoto walizo nazo ili kuzitaftia ufumbuzi .


Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni ameweka utaratibu wa kukutana na Watumishi wake mara moja katika kila robo ya mwaka ili kusikiliza changamoto walizo nazo ili zifanyiwe kazi na pia kutoa msisitizo katika suala la kuwajibika bila shuruti.


IMETILEWA NA KITENGI CHA HABARI NA MAWASILIANO MANISPAA YA KIGAMBONI

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa