• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Watoa huduma wa afya ngazi ya jamii wajengewa uwezo mafunzo ya ulishaji kwa watoto kwa lengo la kupunguza Utapiamlo.

Posted on: October 24th, 2022


Watoa huduma wa Afya ngazi ya jamii  67 wajengewa uwezo wa mafunzo ya ulishaji wa watoto wadogo kuanzia mama anapokuwa mjamzito ,mtoto anapofikisha umri wa miezi 6 -24 ili kuwasaidia kutoa elimu  inayohitajika kwa jamii kwa lengo la kupunguza hali ya utapiamlo.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo kwenye ukumbi wa Manispaa Afisa lishe wa Wilaya Bi.Henerietha Henry amesema kua, lishe bora inaanzia kipindi mama anapokua mjamzito kwasababu mtoto anaanza kupata chakula kupitia milo anayokula mama yake hivyo ni vyema kuzingata ulaji sahihi ili kumjenga mtoto tangu akiwa tumboni.

Akiongelea kuhusu elimu ya lishe na upungufu wa damu kwa waamama wajawazito Afisa lishe amesema kuwa vyakula vyenye asili ya mimea na wanyama ni muhimu kuvizingatia ikiwemo na matumizi sahihi ya dawa za kuongeza damu wanazopewa kliniki ili kumuwezesha kujifungua mtoto mwenye afya bora.

Akizungumzia suala la unyonyeshaji wa watoto mara baada ya mama kujifungua kwa kipindi cha miezi sita afisa lishe amewasisitiza watoa huduma za afya kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa maziwa ya mama pekee kwa kipindi hicho kwani yanajitosheleza na yanavirutubisho vyote  anavyopaswa kuvipata mtoto.

Aidha amewaeleza watoa huduma kuelimisha jamii kuwa maziwa ya mama asilimia70 ni majimaji hivyo ile dhana ya maziwa mepesi na kuona watoto hawashibi waiondoe kwani kumuanzishia chakula mbadala katika kipindi cha miezi 6 kunaathari kubwa.

Akizungumzia faida ya kumnyonyesha mtoto miezi 6 bila kumpatia chakula mbadala  Afisa lishe amesema kuwa, maziwa ya mama ni Kinga tiba, sio gharama na yanajitosheleza . chakula mbadala kwa mtoto chini ya miezi 6 kunaweza kupelekea  kupata magonjwa sugu kama kisukari na presha , uwezekano wa kupata aleji, athari katika mfumo wa mmeng’enyo wa chakula sababu haujakomaa na maradhi mengineo.

Kwa upande wa elimu ya  ulishaji wa watoto kuanzia umri wa miezi sita hadi miezi ishirini na nne Afisa Lishe Fauzia Msuya amesema kuwa ni muhimu kwa wazazi au walezi kuzingitia  kumpatia mtoto  nishati inayohitajika kulingana na umri wake kwa kuzingatia makundi maalumu yoe ya chakula.

Mafunzo hayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Manispaa na kuhudhuriwa na watoa huduma wote kutoka mitaa 67 ya Manispaa ya Kigamboni.



Afisa lishe wa Wilaya Bi.Henerietha Henry akitoa mafunzo ya ulishaji kwa watoto kuanzia wakiwa tumboni mwa mama zao kwa watoa huduma ngazi ya jamii kwenye ukumbi wa manispaa


watoa huduma ngazi ya jamii wakisikiliza kwa umakini mafunzo yanayotolewa na Afisa lishe.


Mmoja wa watoa huduma ya Afya ngazi ya Jamii akichangia mada ya athari za kumuanzishia mtoto chakula mbadala kwa kipinddi cha miezi sita ya mwanzo baada ya kuzaliwa.


Watoa huduma ya afya ngazi ya jamii wakifuatilia mafunzi ya lishe bora kwa mama mjamzito ili kuimarisha ulishaji wa mtoto akiwa tumboni.


Watoa huduma ya Afya ngazi ya jamii wakifuatilia kwa umakini mafunzo ya ulishaji kwa watoto.


Mmoja wa watoa huduma ya Afya ngazi yajamii akichangia faida za unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa watoto kipindi cha miezi 6.


Watoa huduma ya Afya ngazi ya jamii wakifuatilia mafunzo.



Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa