• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Wanawake vijana jiungeni kwenye vikundi mnufaike na mikopo ya Serikali

Posted on: September 29th, 2018

Katika kutekeleza wa maagizo ya Serikali Manispaa ya Kigamboni leo imefungua jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi ambalo lilianzishwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu ambapo mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bi.Rahel Muhando alishiriki kuzindua jukwaa hilo Ngazi ya Kata na kuwasisitiza wanawake kujiunga kwenye vikundi ili waweze kunufaika na mikopo inayotolea na Manispaa.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa jukwaa Kata ya Kibada Bi. Rahel Mhando (Katibu Tawala Wilaya) alisema kuwa  huo ni mwendelezo na ni utekelezaji wa agizo la Serikali kwamba ngazi ya Wilaya, Kata na Mitaa kote kuwe na majukwaa ya uwezeshaji wanawake ambapo lengo kuu likiwa ni kuwawezesha Wanawake kujikwamua kiuchumi, kupitia asilimia 10 za mapato ya ndani  zinazotolewa na Manispaa inayohusisha pia Vijana na walemavu katika kuwawezesha kujikwamua na umasikini.

Aliongeza kuwa katika ziara aliyoifanya takribani maeneo yote ya Kigamboni amegundua kuwa wakinamama wengi wameitikia wito wa kujiunga katika vikundi ambapo sasa ni jukumu la Serikali kuhakikisha fedha zinazotengwa zinawafikia walengwa kwa wakati.

“Nawasisitiza wanawake muendelee kujiunga kwenye vikundi ili muweze kufikiwa kwa urahisi kwenye mikopo hata na tasisi ambazo zimejitoa kusaidia kuwainua kiuchumi, vijana pia mjiunge kwenye vikundi Serikali ipo kuwahudumia na sisi Kigamboni tumejipanga kutekeleza agizo la Serikali” alisema Bi.Rahel

Kwa upande wake mlezi wa jukwaa la wanawake Kata ya Kibada ambaye pia ni Diwani wa Kata hiyo Mhe. Amin Mzuri Sambo alisema kuwa ni jambo la faraja kuona wakinama wanajikwamua kiuchumi na kuwataka kutumia vyema  fursa ambayo Serikali imeitoa kwao  kwasababu wao kama viongozi wapo kuhakikisha  fedha tengwa zinawafikia walengwa wote wakiwemo vijana na walemavu.

Uzinduzi wa jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi Kata ya Kibada lenye kauli mbiu ya “Wanawake tumieni fursa ya jukwaa kushiriki uchumi wa viwanda” ni muendelezo ambapo mpaka sasa Kata 6 kati ya 9 zimekwishazindua  majukwaa.

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ilitenga kiasi cha milioni 311 kwaajili ya mikopo ya vijana na wanawake na kwa mwaka wa fedha  2018/2019 Manispaa imetenga Milioni 537 kwaajili ya mikopo ya wanawake na vijana na milioni 132 kwaajili ya waalemavu.

Katibu Tawala Wilaya Bi.Rahel Mhando akiwa ameambatana na wanawake akikakua bidhaa mbalimbali

Wanawake wajasiliamali wakimshangilia mgeni rasmi ambaye ni Katibu Tawala Wilaya.

Mlezi na diwani wa kata ya Kibada Mhe. Mzuri Sambo akizungumza na wanawake kwenye uzinduzi wa jukwaa

Viongozi wakiwa wamesisima kutazama  vikundi vyakinamama vikipita kutoka mitaa mbalimbali ya kata ya kibada.

Wanawake wakiwa kwenye shamrashamra

moja ya mtaa wa Kibada ukipita na bango lake mbele ya viongozi ili wapate kusoma ujumbe.

Vijana wa hamasa wakisherehesha

Katibu Tawala Wilaya Bi.Rahel Mhando akikagua bidhaa za batiki kutoka moja ya kikundi cha kinamama

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa