• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Wananchi jitokezeni kupata matibabu ya kibingwa -Mkurugenzi Kigamboni

Posted on: June 17th, 2019

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch. Ng’wilabuzu Ludigija ametoa rai kwa  wananchi wa kigamboni kujitokeza kwa wingi kupata huduma ya matibabu kutoka kwa madaktari bingwa waliopo kwenye kituo cha Afya Kigamboni  yatakayoendeshwa  kwa muda wa siku nne kuanzia leo Jumatatu hadi alhamisi.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa matibabu kutoka kwa madaktari hao bingwa wa wanawake,watoto,upasuaji,mifupa, meno na Koo uliofanyika kwenye kituo cha Afya Kigamboni, Mkurugenzi amesema kuwa uchache wa watumishi wa afya hausababishi wananchi kushindwa kufikiwa kwa kupata huduma za kibingwa kama hizo ndio maana wameamua kuandaa kambi hiyo ambayo itawasaidia wananchi wengi kupunguza gharama , muda  na usumbufu wa kufata huduma hizo maeneo ya mbali.


“Niwahakikishie Madaktari hawa ukiondoa utaalamu wao ni wakarimu na wanamapokezi mazuri  hivyo ni sahihi kabisa, kwasababu mbali na matibabu tunaamini pia katika mapokezi kama tiba,  muamini kuwa matatizo mtakayowapelekea yatapatiwa ufumbuzi”Alisema Mkurugenzi.


Ameongeza kuwa Mhe. Rais amewekeza nguvu kubwa kwenye huduma za afya kwa kuamini kuwa ili Taifa liweze kujenga uchumi bora na imara  lazima liwe na wananchi wenye afya nzuri na salama , na Kigamboni kwasababu  Serikali imewekeza majengo bora ya afya haina budi kuhakikisha majengo hayo yanatumiwa ipasavyo na kutendewa haki.


Aidha Mkurugenzi amesema kuwa huduma hii ni endelevu ambapo baadaya siku hizo nne kuisha kila wiki kutakuwepo na kliniki ya Madaktari Bingwa na kwamba ushiriki wa wananchi kwenye zoezi hili la siku nne litafungua njia ya kufanya zoezi hilo kuwa endelevu zaidi kutokana na wingi wa wananchi watakaojitokeza.


Mkurugenzi pia ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanajiunga na Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii CHF ambayo itawawezesha kupata huduma hizo za matibabu kwa urahisi kwa kuzingatia ugonjwa haupigi hodi na wakati mwingine hujitokeza kipindi ambacho mwananchi anakua hana fedha za kujitibia.


Mganga mfawidhi wa Kituoa cha Afya Kigamboni DK.Julius  Nyakazilibe amesema kuwa katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi wameona vyema kuhakikisha wananchi wanapata huduma za matibabu ya kibingwa kwenye maeneo yao ambapo wapo wagonjwa  watakaotibiwa kwa msamaha, kwa bima za afya CHF na NHIF, na watakaochangia gharama kidogo kuwezesha kupata matibabu hayo.
Mratibu wa Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Rufaa ya Temeke Dk.Hussein Msuma amesema kuwa wameamua kuunga mkono juhudi za Serikali kwa vitendo kwa kuhakikisha  wanasogeza huduma za Kibingwa karibu na wananchi na kuwataka watumie vyema fursa hiyo ambayo wangeweza kuipata mpaka kwa rufaa.


Huduma hii ya matibabu ya madaktari Bingwa Itasogezwa pia kwenye Hospitali ya Vijibweni.

Mkurugenzi akisalimiana na wagonjwa waliofika kupata huduma ya matibabu ya kibingwa.

Mkurugenzi wa Manispaa Arch.Ng'wilabuzu Ludigija kulia akisalimiana na mratibu wa madaktari bingwa Dkt. Hussein Msuma

Mgonjwa akijaza taarifa zake ili akatibiwe

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Kigamboni Dkt. Julius Nyakazilibe akizungumza na wananchi waliofika kupata matibabu 

baadhi ya wananchi waliofika kupata matibabu

jengo la maabara

Mkurugenzi na viongozi wengine wakikagua maabara iliyosheheni vifaa vya kisasa

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa