• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

WAMILIKI WA HOTELI ZILIZOPO UFUKWENI WAMETAKIWA KUDUMISHA USHIRIKIANO KWA USTAWI WAO KAMA WAWEKEZAJI NA TAIFA KWA UJUMLA

Posted on: March 13th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mh.Hashim Mgandilwa amewataka wamiliki wa hoteli zilizopo pembezoni mwa fukwe mwa bahari kudumisha ushirikiano baina yao ili kuweza kuwaibua wahalifu wanaojificha kwenye maeneo hayo na kuboresha ulinzi na usalama.

Akizungumza kwenye kikao cha wamiliki wa hoteli zalizopo ufukweni mwa bahari leo kwenye ukumbi wa Sunrise Hotel , Mkuu wa Wilaya alisema kuwa ameamua kukutana na wamiliki ili kudumisha ushirikiano pamoja na kujadili masuala ya ulinzi na usalama,uhifadhi mazingira na ulipaji kodi.

Akizungumzia suala la ulinzi na usalama amesema kuwa, kumekuwa na kawaida ya wahamiaji haramu kujificha kwenye maeneo hayo na kufanya vitendo vyakiuhalifu hivyo ni vyema wamiliki kuwatambua watu wao na kuhakikisha wanatoa taarifa pale ambapo wanaona kunamtu hawamuelewi  kwa usalama wao na wananchi kwa ujumla.

Ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya tano inapenda  wawekezaji  na inajitahidi kuboresha miundo mbinu ili kuhakikisha wawekezaji wanakuwa salama hivyo wao pia wanaowajibu kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha mafanikio yaliyokusudiwa yanafikiwa.

Amesema kuwa kila mwekezaji awekeze kihalali na alipe anachostahili kulipa  na kwamba Serikali haitamvuilia mwekezaji ambaye atakwepa kodi kwa makusudi hususani wale wanaofanya biashara kinyemela bila kusajiliwa na kwataka kuhakikisha wanalipa kodi ambazo zipo kisheria ili kuepuka adha zinazoweza kuzilika.

"Tozo zinazofahamika kisheria zilipwe kwa wakati kuepuka adha zinazoweza kuzuilika, na huu muone kama ni uwajibikaji kwenu"alisema Mkuu wa Wilaya.

Aidha katika suala la  mazingira Mkuu wa Wilaya amesema  ni marufuu kuweka uzio kwenye njia zinazoelekea fukweni kwani maeneo yote ya fukwe ni mali ya wananchi hivyo nivyema wakaweka mazingira rafiki yatakayowanufaisha wao kama wawekezaji bila kuwazibia njia wananchi ya kufika maeneo ya fukwe.

Aliwataka pia kuhakikisha tathmini za kimazingira zinafanywa kwenye maeneo yao na kuacha kujenga au kufanya shughuli zozote ndani ya mita 60 kutoka baharini  ikiwa ni pamoja na kuboresha mifumo ya maji taka.

Mh.Mgandilwa ametoa rai kwa wamiliki wa hoteli hizo kudumisha ulinzi na usalama  siku za sikukuu  ambazo wateja  wanakuwa wengi kwenye maeneo yao kwaajili ya mapumziko ili kuweka ulinzi madhubuti kwa kuzingatia ulinzi ni jukumu la kila mwananchi na kwamba  polisi waliopo hawatoshelezi kuwepo kwenye maeneo yote .

Mwisho aliwataka kama wadau wa uwekezaji  kuendelea kutangaza fursa za uwekezaji hususani eneo la ardhi kwani Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni inamaeneo mengi ya ardhi ambayo hayajawekezwa hivyo  watu mbalimbali wanakaribishwa kuja kuwekeza.

Mkutano huo ulihusisha wamili wa hoteli wanaotoka kwenye Kata tano za Manispaa ya Kigamboni ambazo ni  Somangila,Kigamboni,Mji mwema,Pemba mnazi na Kimbiji ambapo Madiwani na wataalamu mbalimbali kutoka TRA,TCCIA, na ofisi ya Mkurugenzi wameshiriki pia.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mh.Hashim Mgandilwa akizungumza na wamiliki wa hoteli zilizopo ufukweni kuhusu masuala ya Ushirikiano, ulinzi na usalama, ushiriki wao kwenye kulipa kodi na  uhifadhi wa mazingira kwenye ukumbi uliopo Sunrise Hotel leo.


Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Bw.David Sukali akiwaeza wawekezaji wa hoteli umuhimu wa kupima ameneo yao ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa kibali cha ujenzi ,kulipa ushuru wa huduma na kupata leseni za biashara.

Mh. Dotto Msawa Diwani wa Kta ya Kigamboni na Mwenyekiti wa Kamati ya uwekezaji Manispaa ya Kigamboni akisisistiza wafanyabiashara kushirikiana na  kuwa wepesi wa kutoa taarifa  hususani za kuhalifu na kuhakikisha wanaleseni halali za kufanyabiashara mahali walipo kuepuka adha mbalimbali.

Bw. Elicontrol Mrema Mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara wenye viwanda na kilimo TCCIA akichangia maada ya ulipaji kodi na umuhimu wa ushirikiano baina ya wafanyabiashara na Serikali.

Meneja wa mamlaka ya mapato Temeke Bw. Gamaliel Mafie akitoa ufafanuzi juu ya elimu huduma zinazotolewa na TRA na kusisitiza umuhimu wa usajili wa hoteli na utoaji kodi pasipo kushurutishwa.

MMoja wa mmiliki wa hoteli akitoa hoja yake kuhusu masuala ya kodi kwenye kikao hicho

Baadhi ya wataalamu na wamiliki wa hoteli za pembezoni mwa fukwe waliofika kwenye kikao wkisikiliza kwa makini.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa