• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Wakazi wa Kijaka kunufaika na Zahanati ya Kisasa

Posted on: July 3rd, 2019

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ngwilabuzu Ludigija leo amekabidhiwa rasmi zahanati ya Mtaa wa Kijaka iliyopo kwenye Kata ya Kimbiji ambayo imejengwa kwa ushirika wa Shirika lisilo la Serikali Caritas Jimbo kuu Katoliki  la Dar es Salaam ambao wamekamilisha ujenzi wa jengo hilo kwa gaharama za Milioni 69.46 huku nguvu za wananchi ikiwa ni milioni 7.6 na Mfuko wa jimbo Milioni2.

Akipokea makabidhiano hayo kwenye Zahanati hiyo kutoka kwa Mkurugenzi wa Caritas Jimbo la Dar es Salaam, Mkurugenzi amesema kwamba anashukuru sana kwa msaada amabao Caritas wameutoa kwa wananchi wa Kijaka ambao utarahisisha upatikanaji wa huduma kwao ambapo utapunguza vifo vya mama na mtoto.

Mkurugenzi amesema kuwa Kigamboni ni Manispaa changa na inaupungufu mkubwa wa miundombinu kwenye sekta za elimu, zahanati kila mitaa, ofisi za watendaji wa Kata na Mitaa hivyo kama Serikali wanalazimika kushirikiana na wadau wa maendeleo kama  caritus kutatua baadhi ya changamoto hivyo anawaomba caritus kuendelea kuisapoti Manispaa.

Aidha amewataka wananchi waliokabidhiwa Zahanati hiyo kuhakikisha wanaitunza  kwa kupanda miti na maua ambayo yatafanyika kama kivuli na mapumziko kwa  wagonjwa watakaofika kuhudumiwa hapo, na kuwaomba kutoa ushirikiano kwa wahudumu walioletwa kwenye Zahanati hiyo.

Mkurugenzi amewapongeza  wananchi wa Kijaka kwa Umoja na nguvu kazi walizojitolea kufikisha jengo hilo kwenye hatua ya lenta na kuwaomba viongozi wa Kimbiji kuhamasisha wananchi kujitolea nguvu kazi ili wafadhili na Serikali wanapoombwa kuwasaidia iwe rahisi tofauti na  kama wananchi wanapoomba msaada wakiwa hawajaaanza kufanya kitu chochote.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya kigamboni Dkt.Charles Mkombachepa  ameshukuru uongozi wa Caritus  kwa kuwasogezea wananchi wa Kijaka huduma Karibu na kusema kuwa zahanati hiyo  inafanya jumla ya zahanati 20 zinazomilikiwa na Serikali na inatarajiwa kuhudumia wananchi zaidi ya 500 ambapo tangu mei ilipoanza kufanya kazi imehudumia wagonjwa 176.

Mganga Mkuu  amesema kuwa Caritus wanaisaidia Kigamboni kuendana na kasi ya Rais na utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya kusogeza na kuimarisha huduma za afya kwa wananchi hususani wale waliopo pembezoni mwa mji ambao wanapata changamoto kuzifata huduma maeneo ya mbali .

Mkurugenzi wa Caritus Jimbo kuu la Dar es salaam Christian  amesema kuwa fedha zilizotolewa zimesaidia kurekebisha kuta za jengo  na kuweka madirisha ya vioo,kuweka dari(gypsum), kupiga plasta na rangi,kupiga bati la paa rangi, kuchimba kisima,tanki la maji, umeme wa jua(solar),ufungaji wa solar kwaajili ya kupampu maji pamoja na mtandao wa taa kwenye maeneo yanayozunguka Zahanati.

Ameongeza kuwa fedha pia zimetumika kujenga vyoo,ujenzi wa sehemu maalumu ya kuchomea taka,feni zinazotumia solar na televisheni itakayowawezesha wagonjwa kupata elimu ya afya na namna bora ya kujikinga na maradhi mbalimbali.

Aidha ameshukuru uongozi wa kijaka kwa kujali afya ya jamii na kuanzisha mradi huo na kusema kuwa  hiyo ndiyo tafsiri mojawapo sahihi ya maendeleo ya  jamii inayosisitizwa na Serikali  hivyo wataendelea kuunga mkono juhudi za Serikali.

Diwani wa Kata ya Kimbiji Mhe. Sanya Bunaya ameshukuru Caritus na Mkurugenzi kwa namna ya Kipekee walivyowasaidia wakazi wa Kijaka kupata huduma za afya na kwamba yeye kama kiongozi atahakikisha kuwa kipaumbele katika kuwahamasisha wananchi kujenga mazoea ya kujitolea nguvu kazi zao ili kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Zahanati ya Kijaka ilianza ujenzi rasmi mwaka 2008 kupitia nguvu za wananchi baada ya kuona uhitaji mkubwa wa huduma za afya ambapo baada ya Caritus kupokea maombi ya ukamilishwaji wa jengo hilo Januari 2019, Aprili 2019 waliwezesha kumalisha jengo hilo na huduma kuanza kutolewa rasmi mei 2019.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ng'wilabuzu Ludigija akipokea feni kutoka kwa Mkurugenzi wa Caritus Jimbo kuu la Dar es Saam kwaajili ya watumishi wa Zahanati hiyo

Baadhi ya wananchi wa Kijaka waliofika kushuhudia makabidhiano hayo

Mkurugenzi wa Caritus akionesha cheti cha shukurani alichopokea kutoka kwa Mkurugenzi wa  Manispaa ya Kigamboni

Stoo ya dawa

Chumba cha Kujifungulia/uzazi

Jengo la Maliwato

Wananchi wa Kijaka wakiimba ngonjera ya shukurani kwa kupatiwa Zahanati hiyo.

Muonekano wa jengo la Zahanati kwa mbele

Mganga mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Dkt.Charles Mkombachepa akizungumza na wananchi na kutoa shukurani

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa