• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo dhamana ya mkopo benki kwa wanavikundi Kigamboni.

Posted on: May 31st, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri leo amekutana na kuzungumza na vikundi vya kinamama na vijana kwa lengo la kuwapa elimu na kuwatarifu namna ambavyo vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo vinaweza kuwa dhamana kwenye ukopaji wa mikopo Benki ya CRDB .

 Akizungumza kwenye viwanja vya ofisi Mjimwema Mkuu wa Wilaya amesema kuwa baada ya kuona  taasisi za fedha zinatoa mikopo yenye masharti magumu , uongozi wa Wilaya na Banki ya CRDB walifanya mazungumzo na kuandaa utaratibu ambao utawezesha wafanyabiashara wadogo wenye vitambulisho vya biashara kupata mikopo itakayokuza mitaji yao.

Mkuu wa Wilaya ameongeza kuwa baada ya kukamilisha zoezi la kugawa vitambulisho vya wafanyabiashara wenye mitaji midogo  wameamua kukipa thamani kitambulisho kwani kitawawezesha  kuwaondolea bugudha wafanyabiashara wadogo, kupata taarifa zao na kujiunganisha na benki  kwa namana bora ya kupata mikopo.

Aidha amesema ili uweze kuwa na sifa ya kukopesheka ndani ya kikundi kama mtu mmoja mmoja ni lazima uwe na kitambulisho cha mfanayabiashara na kuongeza kuwa mikopo itakayotolewa itaanzia laki 1 hadi laki 5 ambapo kwa mkopo wa laki 1 riba itakuwa ni 1500 kwa mwezi .

“Mfumo huu ni sisi nchi nzima ndio tumeuanzisha kwa kutumia dhamana ya kitambulisho kuhakikisha mnakuza  mitaji yenu kwa mikopo ya riba nafuu, Nimewaita wanavikundi sababu unamkopesha unayemjua, mikopo inayotolewa na manispaa ile ya asilimia 10 haijitoshelezi ndio maana tumekuja na  njia hii mbadala kwa sababu kila mtu atapata pesa yake mwenyewe”

Meneja wa Benki ya CRDB Bw. Samson Keenja amesema kuwa Benki imetenga Bilioni 10 kwaajili ya kuwakopesha wanavikundi wenye vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo ambapo wameweka masharti mepesi yatakayomuwezesha kila mwakakikundi kukopa.

Ameongeza kuwa kwasababu ndio kwanza wanaanza Kigamboni , angependa ingekua ya mfano ili waweze kusambaa  na maeneno mengine nchini, ambapo pia Elimu ya kutunza fedha, utunzaji wa kumbukumbu na namna ya kupata mikopo itatolewa kwa wote.

“Uamuzi wa kufanikiwa au kutokufanikiwa ni sisi wenyewe, tumieni fursa hii ili kuinua uchumi wenu kama ambavyo uongozi wa Wilaya unavyowapigania” Alisema Meneja

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akizungumza na wanavikundi wakinamama na Vijana

Baadhi ya wakinamam na Vijana wakishangilia vitambulisho kuwa dhamana ya Mikopo kwao


Baadhi ya wananwake na Vijana walioshiriki hafla hiyo

Baadhi ya wanavikundi wakinamama walioshiriki hafla hiyo


Meneja wa CRDB Samson Keeenja akizungumza na wamama na vijana taratibu za kutumia kitambulisho kupata mikopo.


Meneja akizungumza na wakinamama na Vijana walioshiriki kwenye hafla hiyo

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa