• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

VIKUNDI 24 KUNUFAIKA MKOPO 10% YA MIL.438,111,518.54

Posted on: December 8th, 2022

MANISPAA YA KIGAMBONI KUTOA MIL. 438,111,518.54 KATIKA ROBO YA KWANZA ,VIKUNDI 24 VITAKAVYONUFAIKA VYAPEWA MAFUNZO


Hayo yamebainika leo katika ukumbi wa Manispaa ya Kigamboni ambapo vikundi 7 vya vijana  ,kina vikundi 11vya wanawake  na vikundi 6 vya  walemavu watapatiwa  mkopo wa mil.438,111,518.54 katika Robo ya Kwanza wamepewa mafunzo namna ya matumizi Sahihi ya pesa watakazopewa ili ziweze kuleta tija na faida na kuwawezesha kuzirejesha,lakini pia elimu ya uongozi,fedha,kanuni na sheria mbalimbali za mikopo ya asilimia 10,masuala ya Rushwa, ukaguzi  na namna ya kutumia mfumo wa TPLMIS.(mfumo wa malipo ya mikopo ya asilimia 10)


Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo kaimu mkuu WA Idara ya maendeleo ya jamii ndg.Aliadina Peter amesema Mafunzo hayo Yana lengo la kuwajengea uwezo katika maeneo mbalimbali ili mikopo wanayopokea uweze kuwa na tija kwao na pia kuweza kutimiza masharti ya mkopo ikiwepo kutumia kwa ombi lililokusudiwa.Lakini pia amewaonya katika suala la marejesho kwani imekuwa tatizo kwa baadhi ya vikundi kutorejesha kwa wakati.



Akiongea akitoa mada ya masuala ya biashara Afisa biashara Nyasama Mohamed ameongelea masharti mbalimbali ya uanzishwaji wa biashara ikiwepo ukataji wa leseni ,ulipaji wa shuru mbalimbali,aidha masuala ya masharti ya kiafya iwapo biashara ni ya masuala ya uuzaji wa vyakula,hivyo amewataka kuzingatia taratibu za kibiashara ili kuepuka faini na usumbufu.


Nae  Afisa Ukaguzi wa ndani ndg.Chacha Nyamriba akitoa mada ametoa msisitizo katika suala zima la uwazi katika masuala ya pesa na matumizi sahihi ya matumizi ya pesa kutokana na lengo ikizingatiwa na nyaraja muhimu zinazotakiwa katika masuala yahusuyo fedha ili kuepuka usumbufu wakati wa kukaguliwa.


Kuhusu masuala ya rushwa Afisa wa TAKUKURU Bi. Neema  akiongelea masuala ya rushwa amewaelimisha kuhusu Aina za rushwa na madhara yake katika maeneo mbalimbali ikiwepo kuvunjwa kwa haki, migogoro baina ya wana vikundi na hata maradhi kupitia rushwa ya Ngono.Hivyo amewasisitizia kuwa na hofu ya Mungu ili iwaongoze katika kuepuka kujiingiza katika masuala ya Rushwa.


Akifafanua sheria na kanuni mbalimbali za mikopo  ya asilimia kumi ya Halmashauri Mwanasheria Bi.Rose Mligo amesema mikopo hii ina kanuni  maalum kila kikundi hakina budi kufuata sheria ambapo mikopo yote inasimamiwa na sheria ya mikopo ya asilimia kumi ,aidha mikataba ambayo wanaisaini nayo ina kanuni zake sheria za mikataba,aidha kuna kanuni ya adhabu ambayo hutumika pale ambapo kikundi kimekiuka masharti ya mkopo, Mwanasheria huyo amewasisitizia kuwa wawe makini katika kuhakikisha wanatumia pesa kulingana na maombi na si kugawana pesa kwa wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa juu yao.


Katika suala la uongozi na utawala Bora Afisa utumishi ndg.Cosmas Hinju alitoa elimu kwa wanavikundi hao ambapo moja ya msisitizo aliowapa viongozi wa vikundi nufaika kuwa wao ndio waonyesha njia katika vikundi vyao hivyo inabidi  wajitambue,wawe wawazi katika masuala ya kikundi ikiwepo uwazi wa taarifa za mahesabu aidha kuwa makini wa kufanya utafiti kabla ya kufanyia maamuzi yoyote,pamoja na hayo awe ni mwenye kuzingatia sheria za nchi,kuwa wasiri na kila mwanakikundi ajihisi ni sehemu ya mafanikio ya kikundi.


Katika elimu ya fedha Mhasibu wa Manispaa Bi.Yusra aliwaelekeza namna ya kutunza kumbukumbu za fedha za marejesho wanayofanya aidha wawe wafuatiliaji wa madeni yao katika ofisi ya Manispaa ilikuwa na ulinganisho wa taarifa zao,pia walisisitizwa umuhimu wa kutunza risiti mbalimbali za miamala na kuhakikisha akaunti zao za vikundi za benki zinakuwa hai.


Pamoja na mafunzo hayo wamepata fursa ya kufundishwa kwa vitendo namna ya kutumia mfumo wa TPLMIS katika kujisajili na kujaza taarifa zao mbalimbali na hata kutuma maombi ya mkopo na namna ya kufungua email ya kikundi kupitia mfumo huo,mafunzo yaliyotolewa na Afisa Vijana Veronika Kiluvia.


Imetolewa na kitengo cha Mawasiliano Serikalini KGMC

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa