• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

UJENZI KITUO CHA AFYA KIMBIJI KUWAKOMBOA WANANCHI NA ADHA YA UMBALI MREFU.

Posted on: March 20th, 2018

wananchi wa Kata ya Kimbiji na maeneo jirani Manispaa ya Kigamboni wataondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kufata huduma za afya bada ya ujenzi wa kituo  cha afya kinachojengwa kwa sasa kukamilika.

Ujenzi wa kituo cha afya umekuja baada ya kupandishwa hadhi mwaka 2015 kufuatia mapendekezo yaliyotolewa na vikao vya ndani ya Halmashauri , Madiwani kupendekeza Zahanati ya Kimbiji kupandishwa hadhi kuwa kituo cha Afya ikiwa ni utekekelezaji wa sera ya  Wizara ya Afya,ustawi wa jamii, jinsia wazee na watoto ya kuwa na kituo cha afya katika kila kata.

Akizungumza juzi kwenye ziara na Umoja wa Vijana CCM mkoa ya ukaguzi wa miradi ya maenedeleo inayotekelezwa na Manispaa, Kaimu  Mkurugenzi Bw. David Sukali alisema kuwa ,kuna zahanati  14 lakini vituo vya afya vya Vijibweni na Kigamboni ndivyo vinavyotegemewa hali inayopelekea wananachi wa Kimbiji kutembea umbali wa kilomita 40 - 45 kufata huduma za afya kwenye vituo hivyo.

Aliongeza kuwa Serikali katika mpango wake wa adhima ya kupunguza vifo vya Mama wajawazito na kuboresha huduma za afya, iliandaa mpango maalumu ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni iliingia katika awamu ya pili ya mpango huo, Mnamo mwezi Disemba 2017 Halmashauri ilipokea jumla ya fedha shilingi milioni mia nne (400,000,000) kutoka Serikalini kwaajili ya utekelezaji.

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ilianza kwa ujenzi wa jengo la upasuaji,wodi ya kina mama,maabara na chumba cha kuhifadhia maiti ikiwa ni vipaumbele.

Aliongeza kuwa ujenzi umetumia Mafundi wenyeji “local Fundi” kufanikisha ujenzi huu wa mradi ambapo baada ya taratibu kufanywa walipatikana mafundi 4 na kila fundi jengo 1.

wananchi wameshiriki kikamilifu wakiongozwa na Diwani wa Kata ya Kimbiji Mh. Muhidini Bunaya aliyewahamasisha wananchi kushiriki nguvu kazi ya kusafisha eneo na kuokota mawe kwaajili ya ujenzi ambapo Diwani alishiriki kwa kutoa roli nne za mchanga.

Aidha wafanyabiashara  watatu wa usafirishaji walijitolea mchanga roli moja kwa kila mfanyabiashara na Kiwanda cha Lake Cement kilichopo kimbiji kujitolea bulldoza kwaajili ya kusafisha eneo la ujenzi na kupunguza bei ya mfuko wa saruji kutoka shilingi 11,500 hadi 8,000.

Wakazi wa Kimbiji kwa sasa wameweza kuimarika kiuchumi kwani  mafundi na vibarua hawa wanahitaji huduma za malazi, chakula na usafiri hivyo kuwa fursa kwa wakazi wa Kimbiji wanaojishughulisha na biashara za chakula,maradhi na usafiri.

Katika kutekeleza Mradi huu vifaa vyote vya ujenzi vinavyopatikana katika maeneo ya kata ya Kimbiji vilinunuliwa,hivyo kusaidia ukuaji wa biashara katika kata Kimbiji kwa kuongeza mzunguko wa fedha ambapo baadhi ya vifaa Vilivyonunuliwa ndani ya Kata ni  Mchanga,kokoto,matofali,vifusi na mawe.

Jengo la Maabara,Upasuaji na la kuhifadhia maiti yamefikia katika hatua ya kupaua na Jengo la kina Mama wajawazito, hatua ya kujenga msingi imekamilika., ambapo hadi kufikia tarehe 30/5/2018 majengo yote yanatarajiwa kukamilika.


Msafara kuelekekea kwenye ujenzi wa majengo ya kituo cha afya kimbiji yanapojengwa.

Kaimu Mkurugenzi akitoa baadhi ya maelezo kwenye jengo la kinamama wajawazito.

Mafundi wakiendelea na kazi ya ujenzi.


Kaimu Mkurugenzi Bw.David Sukali wa mwenye suti ya bluu akionesha baaadhi ya vyumba na matumizi yake  kwenye jengo la wakinamama wajawazito.

jengo la maabara na upasuaji likiwa kwenye hatua ya upauaji kama inavyoonekana kwenye picha.

Mafundi wakienedelea na ujenzi wa msingi kwenye jengo la wakinamama wajawazito.

ukaguzi jengo la kuhifadhia maiti.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa