• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Ubalozi wa Kuwait wakabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya milioni 12 Hospitali ya Vijibweni.

Posted on: June 11th, 2018

Ubalozi wa Kuwait umekabidhi zawadi ya vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni ya Vijibweni vyenye thamani ya shilingi milioni 12 za kitanzania ikiwa ni utekelezaji wa  mwanzo wa ushirikiano mzuri baina ya Kigamboni na Taifa la Kuwait.

Akizungumza jana kwenye mapokezi ya vifaa tiba hivyo Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Mgandilwa ameshukuru kwa zawadi hizo alizozitoa  Balozi wa kuwait ikiwa ni ahadi aliyoitoa alipotembelea Hospitalini hapo wiki mbili zilizopita.

Mhe. Mgandilwa alisema kuwa  matembezi ya Balozi wa Kuwait katika Hospitali ya vijibweni yalimfanya kubaini changamoto ya baadhi ya vifaa, hivyo kuahidi kurudi kabla ya mwezi wa ramadhani kuisha.

Aliesma kuwa Kuwait na Tanzania ni marafiki  na kuna kila sababu ya kuendelea kusapotiana na kudumisha urafiki uliopo huku akimuomba Balozi wa Kuwait kuendelea kusaidia baadhi ya vifaa ambavyo ameahidi atavileta kama vile vitanda vya kung'olea meno vitakavyosaidia kuboresha huduma za afya kwa ubora zaidi.

"Naomba usiishie hapa kwa chochote utakaachona unaweza kusapoti kwenye sekta hizi tatu usisite kutusaidia na mimi kama Mkuu wa Wilaya naahidi kudumisha urafiki wetu" Alisema Mkuu wa Wilaya.

Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Mhe. Jasem Al-Najem alisema zawadi alizozitoa ni  mwanzo wa ushirikiano mzuri uliotokana na mapokezi mazuri aliyoyapata kipindi chote kutoka kwa Mkuu wa Wialaya ya Kigamboni pindi alipotembelea Wilayani kwake.

Aliongeza kuwa Ubalozi wa Kuwait umetoa Vitanza 3 vya watoto, vitanda3 vya kujifungulia kinamama, mashine za oksijeni, mabeseni 8 ya watoto waliozaliwa , mashine ya kutolea uchafu pindi mtoto anapokunywa maji machafu wakati wa kujifungua na vifaa vingine ili kuboresha huduma za afya zinazotolea na Hopsitali ya Vijibweni.

Balozi Jasem aliongeza kusema kuwa  ataangalia namna atakavyoweza kusaidia kutoa mashine za moyo zilizoombwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni  na kuahidi kuendeleza ushirikano uliopo na Kigamboni na Tanzania kwa ujumla.

Aidha alisema kuwa Kuwait ina mpango unaojulikana kama Kuwait Blood Bank yenye lengo la kutunza damu salama  hivyo atajitahidi kuhakikisha Kigamboni inakua miongoni mwa wanufaika wa mpango huo hususani Hospitali ya Vijibweni ambapo viataletwa vifaa vitakavyotumika kuhifadhia damu salama kwaajili ya kuokoa maisha ya Wananchi wa Tanzania.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mhe.Hoja Maabad alimshukuru Balozi wa Kuwait kwa zawadi alizozitoa na kumuomba kuendeleza urafiki na ushirikiano mzuri ulioanzishwa kwa manufaa ya wote.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Hashim Mgandilwa kushotoakipeana mkono na Balozi wa Kuwait Mhe.Jasem Al-Najem ikiwa ni ishara ya makabidhiano ya moja ya mshine alizozitoa.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni kushoto Mhe.Hashim Mgandilwa akipokea zawadi ya Beseni kutoka kwa Balozi wa Kuwait Mhe.Jasem Al-Najem.

Balozi wa Kuwait Mhe.Jasem Al-Najem akimkabidhi zawadi ya beseni mwanamama Olivia Jelard kutoka Ungindoni, Mkuu wa Wilaya Kushoto na Mstahiki Meya Kulia wakishuhudia.

Baadhi ya mabeseni na vifaa vyake yaliyokabidhiwa kwa wamama waliojifungua watoto Hospitali ya Vijibweni 

Baadhi ya Vifaa Tiba Vilivyokabidhiwa na ubalozi wa Kuwait 

Balozi wa Kuwait Mhe. Jasem Al-Najem akiwa amembeba mmoja wa watoto waliozaliwa siku chache kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni ya Vijibweni, Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni na Mganga Mkuu .

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa