• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

"Thamani ya fedha inaonekana kwenye miradi inayotekelezwa na Manispaa kigamboni" Mwenyekiti CCM Mkoa

Posted on: April 12th, 2018

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Kate Kamba ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni kwa utekelezaji wa Ilani wa chama cha Mapinduzi na kusema kuwa ameiona thamani ya fedha katika miradi yote aliyoitembelea hivyo mshikamano uliopo uendelezwe.

Amayezungumza hayo jana mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi aliyoifanya Manispaaa ya Kigamboni yenye lengo la kuona ni namna gani Ilani ya Chama inatekelezwa.

Akizungumza na watumishi na wananchi wanao shiriki kusimamia miradi Bi.Kamba amesema kuwa, Miradi yote inatekelezwa katika ubora na ndani ya wakati na thamani ya fedha ( Value for money) inaonekana.

"Miradi yenu mizuri na inatekelezwa kwa ubora na wakati, mnaspidi nzuri sana hii inaonesha ni naman gani mnaushirikiano, Kigamboni ni Wilaya changa lakini mambo mnayofanya mnawazidi hata Wilaya kongwe, tumependa" Alisema Kamba

Aliongeza kuwa ameona ushirikishwaji katika utekelezaji wa miradi hiyo na kwamba jamii imeshiriki kikamilifu hali inayopelekea kuona wanao wajibu wa kutunza na kusimamia miradi yao ndio maana wameweza hata kufikia makubaliano ya  punguzo la bei ya ununuzi wa  vifaa vinayohitajika kwenye ujenzi miradi.

Aidha Bi. Kamba alisema kuwa sheria ya manunuzi inagharimu sana utekelezaji wa miradi , urasimu mwingi tofauti na utaratibu wa mafundi wenyeji unaosaidia kutumia fedha kidogo na miradi kujengwa kwa wakati huku thamani ya fedha ikionekana.

 Kamba aliwataka watumishi kuona wanao wajibu na sehemu yao  kufanya kazi na kuhudumia wananchi ikiwa ni utekelezaji wa Ilani na kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa kiwango cha juu.

Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mh. Hashim Mgandilwa  alisema kwamba yeye pamoja na Madiwani , Mkurugenzi na watendaji wake wanaimba wimbo mmoja , thamani ya fedha inayoonekana katika kila mradi ni matokeo ya usimamizi uliopo ambao wamepewa na mamalaka kusimamaia.

Ameongeza kuwa kigamboni inaweza kuwa ya kwanza kwa Halmashauri zinazotekeleza ujenzi wa makao makuu tangu kuanzishwa kwani ndani ya kipindi kifupi cha miaka 2 tangu kuanzishwa kwake, watumishi watakuwa tayari kwenye jengo lao la Utawala lenye ghorofa 3, hii  imewezekana kutokana na mfumo mzuri wa matumizi ya fedha.

Aidha  alisema kuwa mfumo unaotumika wa mafundi wenyeji unaokoa kiwango kikubwa cha fedha ambazo zilikuwa zinapotea bila sababu katika mfumo wa manunuzi.

"Nadhani tuendelee kuangali hizi sheria  za manunuzi, zinazumiza sana Serikali na tuanze kufuata taratibu za kawaida, mfano mfuko wa misumari kwa mfumo wa manunuzi unaweza nunua hadi elfu 6000, wakati kawaida unanunua  elfu3000 hadi elfu 3500"Alisema Mkuu wa Wilaya.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Bw. Stephene Katemba alishukuru  kutembelewa na viongozi wa CCM  na kuona namna gani Ilani  ya Chama cha Mapinduzi  inatekelezwa.

Alisema hadi sasa ameshapokea Bilion 2 kwaajili ya ujenzi wa jengo la utawala na taratibu zote zimezingatiwa za kupata mkandarasi , mradi unayobond ya kulinda( secured bond) ikitokea mkandarasi ameshindwa kuendelea na kazi  na performance bond ( fedha zitekelezwe  kwa kadri inavyotakiwa).

Mwisho aliwakaribisha tena viongozi wa Chama na kwamba kwake ni hamasa kubwa hivyo yeye kama kiongozi atajitahidi kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa kadri ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi inavyotaka.

Ziara ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa iliyoambatana na viongozi mbalimbali wa Chama ilipata fursa ya kutembelea mradi wa ukarabati wa Zahanati ya Buyuni, Ujenzi wa kituo cha Afya Kimbiji, Ujenzi wa miundombinu ya Shule kwaajili ya kuanzisha kidato cha tano kwenye Shule ya Sekondari Nguva, ujenzi wa jengo la utawala na ujenzi wa  uanzishwaji Sekondari eneo la Shule ya Msingi Kigamboni.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa Bi. Kate Kamba akizungumza na kutoa pongezi zake kwa Manispaa ya Kigamboni.

Baadhi ya Wakuu wa idara na vitengo wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa CCM Mkoa alipokuwa akizungumza nao.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mh.Hashim Mgandilwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani jana kwenye ukumbi wa Mkikutano uliopo shule ya Msingi Mjimwema


Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kigamboni Dk.Charles Mkombachepa  akitoa maelekezo ndani ya jengo la maabara na upasuaji

Mkurugenzi Mwenye suti nyeusi Bw.Stephen Katemba  akiongoza msafara kwenda kukagua majengo ya kituo cha afya Kimbiji 

Msafara kuelekea jengo la kuhifadhia maiti

jengo la wamama wajawazito likiwa kwenye hatua  ya renta 


Mwenyekiti wa CCM Mkoa Bi. Kate Kamba akiambatana na viongozi wengine walipotoka kukagua jengo la wamama wajawazito.


Jengo la maabara na upasuaji likiwa katika hatua ya upauaji kama inayoonekana katika picha

Mkurugenzi wa Manispaa aliyenyoosha mkono Bw. Stephen Katemba akifafanua kuhusu mandhari ya Hospitali yatakavyokuwa ,mara baada ya kumalizika ujenzi , hapo ni mbele ya jengo la kuhifadhia maiti.

muonekano wa jengo la kuhifadhia maiti


Muonekano wa nje wa moja ya maabara ya Kisayansi iliyopo Shule ya Sekondari Nguva

muonekano wa moja ya maabara ya kisayansi Shule ya Sekondari Nguvu inayotarajiwa kuwa na kidato cha 5


muonekano wa ndani wa bweni la wanafunzi watkaoanza kidato cha 5


Moja ya chumba ndani ya bweni watakacholala wanafunzi wa kidato cha 5


Mkurugenzi mwenye suti nyeusi akionesha ramani ya jengo la utawala kwa Mwenyekiti wa Mkoa CCM alipotembelea kuona hatua ya ujenzi ilipofikia.


Hatua ya ujenzi jengo la Utawala ilipofikia hadi sasa

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi na viongozi wengine walipotembelea kuona mradi wa ujenzi shule ya sekondari itakayokuwa karibu na shule ya Msingi Kigamboni


Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Bw.Stephen Katemba akishukuru uongozi wa CCM kutembelea miradi na kuona utekelezaji wa Ilani.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa