• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Raiss Dk. John Pombe Magufuli azindua rasmi mitambo ya Tifa Gesi

Posted on: June 25th, 2019

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli leo amezindua Ghala la kuhifadhia gesi lenye uwezo wa kuhifadhi tani 7650 za gesi linalomilikiwa na kampuni ya Taifa Gesi ambayo awali ilikuwa ikijulikana kwa jina la Mihan Gas  eneo la Vijibweni Wilayani Kigamboni .

Akizungumza wakati wa uzinduzi Mhe. Rais amesema kuwa Sekta ya Gesi ni sekta nyeti na muhimu kwa maendeleo ya nchi yoyote duniani, ni muhimu katika kuboresha huduma za jamii ikiwemo afya za wananchi , matumizi ya nishati bora ni muhimu katika kutunza mazingira, kwa kutambua hili chama cha mapinduzi kupitia Ilani yake ya 2015  iliahidi kushirikiana na sekta binafsi hivyo anfarijika kuona utekelezaji wa ahadi hiyo unatekelezwa kwa kiwango kikubwa.

Ameongeza kuwa anapongeza wizara ya nishati kwa jitihada kubwa ya kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini, na kwamba hali inaridhisha tatizo  la kukatika katika kwa umeme pamoja na kwamba lipo baadhi ya maeneo kidogo lakini limepungua sana na wananchi wengi wameunganishiwa na umeme ikiwemo vijijini.

“kadri ya miradi hii inavyoendelea miradi ya umeme na gesi nina uhakika bei zitashuka ili wawekezaji wengi waweze kupata faida katika miradi yao watakayowekeza”

Amepongeza sekta binasfi kwa kuitikia wito na kuungana na Serikali katika  kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini, akisema kuwa Mhe waziri wa nishati amesema nchi yetu inakampuni 8 zenye leseni ambazo zinatumika kusambaza gesi majumbani na viwandani hivyo kusaidia  kutunza mazingira yetu kwa kupunguza matumizi ya mkaa.

Aliongeza kuwa Miongoni mwa kampuni inayofanya biashara ya gesi Taifa Gas, imewekeza kiasi cha bilioni 150 ikihusisha  ujenzi wa maghala na mitambo ya kuhifadhi gesi kwenye mikoa 20, mojawapo ya maghala ni hilo ambalo amelizindua leo lenye uwezo wa kuhifadhi gesi tani 7650 ambapo limeifanya Taifa Gesi kuwa  kubwa nchini, Afrika mashariki na kusini mwa janga la sahara .

Aidha amesema kuwa Ghala hilo limeongeza uwezo wa kuhifadhi gesi nchini  kutoka tani 8050 mwaka 2016 hadi kufikia tani 15600 hivi sasa hivyo kuwapongeza, na kwamba amefurahi kuona wamiliki wakampuni hiyo kuwa ni watanzania, ambao  wameonesha kuwa watanzania wanaweza hasa wanapoamua ambapo wameweza kutengeneza ajira na kulipa kodi na tozo mbalimbali.

“Serikali itaendeela kushirikiana nanyi na kamapuni zote zinazojishughulisha na biashara hii ya gesi lengo letu ni kuona wananchi wetu wanapata nishati bora, salama na kwa gharama nafuu” Alisema Mhe. Rais

Aidha ametoa wito kwa wasambazaji wa gesi ya mitungi kuendelea kutanua huduma zao hadi maeneo ya vijijini itawasaidia kupanua soko lakini pia nchi kutunza mazingira sababu asilimia 60 wananchi wanaishi vijijini na wanatumia kuni na mkaa ambayo sio nzuri sana kwa afya.

Pia ameitaka  Wizara ya nishati kuongeza kasi ya kusambaza nishati ya gesi asilia meneo yote ambayo tayari kuna miundombinu na kutoa wito kwa watanzania hususani wanaoishi Dar es salaam kuacha matumizi ya mkaa kuanza kutumia gesi, ambapo mbali na kutunza mazingira na kulinda afya ni nafuu sana ukilinganisha na gharama za mkaa.

Mhe. Rais ametoa wito kwa Wasambazaji wa gesi majumbani kujaribu kupunguza bei ili kuhamasisha wananchi wengi kutumia gesi na kuacha matumizi ya mikaa ambayo ni uharibifu wa mazingira.

Mwisho Mhe Rais amewapongeza viongozi wa Kigamboni kwa namna ambavyo wameendelea kuiboresha kigamboni kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kusema kuwa Kigamboni inakuwa na  itaendelea kuboreshwa kwenye miundo yote ya Barabara, afya,, maji na sekta nyinginezo kwani ni Wilaya pekee yenye mpango bora wa makazi kwa mkoa wa Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taifa Gesi mhandisi Hamisi Ramadhani amesema kuwa  Hadi sasa wamefanikiwa kuwekeza mitambo ya gesi kwenye mikoa 20 na  uwekezaji huo umefanyika ndani ya mwaka 2016 na 2018, ambapo baada ya uwekezaji huo Aprili mwaka 2019 walibadili jina kutoka Mihani Gasi na kuwa Taifa Gesi ili kuipa kampuni yao jina lenye asili ya nchi Yao baada ya kuwa na wamiliki wote watanzania na  Uwekezaji huo unaifanya kampuni kuwa kubwa zaid kwenye uwekezaji kwa idadi ya mitambo ya kisasa ya Gesi   mashariki  na Kusini mwa Afrika ukiwa umegharimu takribani Bilioni 150.








Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa