• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Nishati ya umeme wa uhakika Kigamboni kuvuta wawekezaji

Posted on: June 3rd, 2021

“Nawakaribisha wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi kuja kuwekeza Kigamboni kwasababu tunanishati ya umeme wa kutosha  wa kuweza kuhudumia viwanda na matumizi mengine ya kwaida”.

Hiyo ni kauli ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri mara baada ya kutembelea kituo cha kuzalisha umeme cha Dege ambacho kimekamilika kwa kuweza kuzalisha umeme wa Megawatts 48 ambapo hadi sasa jumla ya megawati 24 ndio zinazotumika kwa matumizi ya viwandani na majumbani kwa Wilaya yote ya Kigamboni na kubakiwa na ziada ya Megawats 24.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Sara alisema kuwa Kigamboni ilikuwa na changamoto mbili ya umeme na barabara ambapo changamoto ya umeme imekwisha malizika kabisa kwani Tanesco wameweza kugawa vituo vinne vya kusambazia umeme vya Muongozo 33kv, Kimbiji (Viwanda) 33kv, Kisarawe II (Viwanda) 33kv na Pembamnazi 33kv.

Mhe. Sara aliendelea kwa kusema kuwa kwa sasa eneo pekee Dar es salaam linaloweza kuwekweza viwanda ni Kigamboni kwa sababu kwanza ni eneo la kimakakati ambalo hata master plan yake imeweza kuainisha maeneo ya uwekezaji lakini pia, Serikali ilikwisha tenga fedha ya miundombinu ya barabara ambayo kwa mwaka wa fedha ujao unaonza Julai barabara hizo zitakuwa zinaanza kujengwa kwa kiwanago cha lami ikiwemo ile ya Kibada-Kisarawe II hadi Kimbiji.

“Nawapongeza sana Tanesco kwa kazi kubwa waliyoifanya kwenye Wilaya yetu na Serikali  kwa kutoa fedha nyingi kuhakikisha tunamaliza changamoto ya umeme,mradi umegharimu Bilion.26 huduma ya umeme imeboreshwa, wananchi wa Kigamboni fanyeni shughuli zenu kwa uhuru”DC Sara.

Aliongeza kuwa Tanesco wamesaidia kupata wawekezaji wakubwa kwani idadi ya maombi ya kuunganishiwa umeme imeongezeka kutoka 200 hadi 1000 na kuunganisha wateja wapya 800 kila mwezi  kutoka wateja 500 hapo awali.

Niwatake Tanesco kutokana na mahitaji makubwa na shughuli za kiuchumi kuwa za uhakika, tunaomba mfanye Kigamboni kuwa Mkoa wa Kitanesco ili iweze kujitegemea kibajeti na kutengeneza mfumo wa kiutawala wa kuweza kuwahudumia wananchi kwa uhakika.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Bara za la wafanyabiashara Elicontro Mrema alisema kuwa anaishukuru Serikali kwa jitihada kubwa ya kuimarisha nishati ya umeme Kigamboni kwa kuondoa ule upungufu uliokuwa unatatiza wawekezaji kuja kuwekeza.

Mkuu wa Wilaya alifanikiwa kuwatembelea wawekezaji wakubwa wawili mmoja  akijulikana kwa jina la ELSEWEDY  watakaojihusisha na utengenezaji wa kebo na transfoma wanaojenga kiwanda chao eneo la Kisarawe II ambao wanatarajia kuanza uzalishaji mwanzoni mwa mwezi wa nane na kutarajia kuajiri watumishi 400-500 wa kitanzania’

Kiwanda cha pili ni AFRICAB-CURE AFYA PHARMACETICAL kinachojengwa Kimbiji watakaojihusiah na uzalishaji wa aina mbalimbali za  dawa wanaotarajiwa kumaliza ujenzi wa kiwanda Desemba mwaka huu na kuanza uzalishaji  Januari 2022 wakilenga kuajiri watumishi 200-400 wa kitanzania.

Kituo cha kuzalishia umeme cha Dege kikiwa kimekamilika na kuanza matumizi tangu 30/04/2021

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Sara msafiri akielekezwa na Meneja wa Tanesco  namna mifumo inavyofanya kazi.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akimutoa rai ya kuifanya Kigamboni kuwa ya Kimkoa Kitanesco ili iweze kujisimamia yenyewe kwa kuwa na rasilimali watu wa kutosha na vifaa vya kutosha.


Muwekezaji wa Kiwanda cha ELSEWEDY akimueleza Mkuu wa Wilaya namna kiwanda chake kilivyolenga kuwaaajiri na kuwafundisha watanzania hususani wale wanafunzi waliotoka kuhitimu masomo yao ili waweze kuwa waalimu kwa wenzao.

Muwekezaji wa Kiwanda cha ELSEWEDY akimuonesha  Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni uwekezaji wanaoufanya na namna walivyojipanga kumaliza kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akiwa amemambatana na wataalamu kutoka AFRICAB na Wenyeviti wa Baraza la Biashara Kigamboni wakizunguka kuangalia uwekezaji wa kiwanda hicho cha kutengeneza dawa.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akizungumza na Meneja Masoko wa AFRICAB juu ya uwekezaji na kiwango cha watumishi atakaowaajiri.

Kiwanda cha ELSEWEDY kinachotarajiwa kuzalisha kebo , transfoma na magenereta na kulenga kuhudumia wateja wa Africa Mashariki na nje .


Kiwanda cha Africab cure pharmaceutical kinachotarajiwa kuzalisha dawa mbailmbali za binadamu na kuhudumia wateja wa Africa mashariki, Afrika ya Kati na Kusini.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa