• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

“Nimeridhishwa na huduma zinazotolewa na vivuko” DC SARA

Posted on: October 9th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri amesema kuwa ameridhika na hali ya uendeshwaji wa kivuko hususani katika eneo la usalama baada ya kutoa maelekezo kwa wasimamizi wa kivuko kuboresha huduma zinazotolewa hapo.

Mhe. Sara amesema hayo leo alipofanya ziara ya ukaguzi wa utekelazaji wa maagizo aliyoyatoa alipotembelea kivuko hicho mwezi uliopita na kusema kuwa kwa kiwango kikubwa maelekezo yamefanyiwa kazi na mabadiliko makubwa yameonekana.

Aliongeza kuwa wametoa namba za simu za dharula kama alivyoelekeza,  namba ya zimamoto na ukoaji, matangazo yanatolewa yanayoeleza  utaratibu mzima wa kupata huduma za vivuko ikiwemo na uwezo wa vivuko ya ubebaji wa watu na magari, wamefunga luninga kwenye vivuko zinazoonesha video fupifupi za elimu ya uokoaji na mawasiliano kwa watumia vivuko.

“ walau sasa kuna elimu kidogo ya uokozi namna ya kutumia life jacket(vazi la uokoaji), maboya, namna ya kuruka kwenye maji, vifaa vimesafishwa na vimewekwa maeneo ya wazi hakuna kufuli kama zamani kwahiyo likitokea jambo lolote inakuwa rahisi kwa abiria kuvipata kwa haraka, kwa kiasi Fulani nimeridhika bado vitu vichache tu” Amesema Mhe. Sara

Aidha ameelekeza kufungwa kwa luninga  kubwa kwenye maeneo ya kusubiria abiria ili elimu inayotolewa iweze kufikiwa na watumiaji wote wa vivuko,kuweka namba ya simu itakayopigwa bure na mwananchi  ikiwa ni pamoja na kufunga kamera itakayosaidia kufuatilia mwenendo mzima wa huduma zinazotolewa na kivuko.

Akizungumzia suala la wavuvi amesema kuwa ni mtambuka kwasababu jinsi soko lilivyojengwa limelenga wafanyabiashara ambao ni wavuvi, mitumbwi iliyopaki pembezoni ambayo inaingilia njia za meli na vivuko lazima wadau wote wahusike kukaa kwa pamoja na kamati ya ulinzi  na usalama kwasababu hawa wadau wanasheria zinazowaongoza kwa hiyo ni vyema utaratibu ukafuatwa katika kutatua changamoto hiyo.

Mkuu wa Wilaya  pia amepiga marufuku mitumbwi kutumika kuvushia abiria kinyume na taratibu na kusema kwamba sheria zifuatwe kwa yeyote atakayebainika anatumia mitumbwi kuvusha abiria.

Kwa upande wake kaimu mtendaji mkuu wa TEMESA Eng.Japhet Masele ameshukuru na kusema kuwa maagizo mengi ambayo yalikuwa yametolewa yalikuwa yameanza kufanyiwa kazi katika kuboresha huduma za vivuko na kusema kuwa wamejipanga kuwa na usismamizi mkali kipindi cha asubuhi na jioni ambapo kunakuwa na abiria wengi na kueleza kuwa wanahakikisha vivuko vyote nchini vinafanya kazi kwa kuzingatia taratibu na kanuni.

Ameongeza kuwa hivi karibuni  wanaweka mfumo wa kuhesabu(electronic counter)  ili kivuko kinavyopakia uongozi uweze kujua kivuko kimeondoka na ujazo sawa kuepuka kuzidisha uwezo wa kivuko husika.

Mkuu wa Wilaya Mhe. Sara Msafiri akieleza namna alivyoridhishwa na maboresho ya huduma zinazotolewa na vivuko.


baadhi ya abiria wakishuka kwenyhe kivuko baada ya kufika ng'ambo

Mtoa elimu ya kujiokoa kwa kutumia vazi la uokoaji(life jacket) akitoa maelezo ya namna ya kulitumia vazi hilo

elimu ya kutumia boya ikitolewa na mkufunzi wa masuala ya ukoaji

Mkuu wa Wilaya akiwa ameambatana na viongozi wengine wakitoka kwenye kivuko cha Mv Magogoni


Kiongozi wa TEMESA aliyenyoosha mkono akieleza changamoto ya mitumbwi ya wavuvi




moja ya luninga iliyofungwa kwenye kivuko cha Mv Magogoni ikionesha video fupifupi za jinsi ya kujiokoa.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa