• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

"Nimefarijika na utekelezaji wa miradi ya soko na kituo cha afya Kigamboni” Mhe. Kandege

Posted on: June 25th, 2020

Naibu waziri wa TAMISEMI Mhe. Josephat kandege amesema kama Serikali amefarijika na utekelezaji wa mradi wa soko Kibada na kituo cha afya Kigamboni na kuzishauri Halmashauri zingine kuhakikisha zinasimamia vyema miradi ya maendeleo kwa kuzingatia muda na viwango vya miradi kuendana na thamani ya fedha tumika.

Mhe. Kandege amezungumza hayo leo alipotembelea  mradi wa ujenzi wa soko la kisasa linalojengwa Kibada na Uboreshwaji wa kituo cha afya Kigamboni ambapo amesema amefarijika kuona huduma za afya zimeboreshwa  kwa kiwangio kikubwa na maelekezo ya marekebisho aliyoyatoa kipindi cha ujenzi wa majengo mapya ya mama na mtoto yametekelezwa.

Kwa upande wa soko la kibada amesema kukamilika kwa soko hilo kwanza kutasaidia kuondoa adha ya wananchi kutembea umbali mrefu kuvuka upande wa pili kwenda kufata huduma  na pia Halmashauri  itakua na kitega uchumi ambacho kitaweza  kuongeza mapato.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri amemshukuru Naibu waziri kwa kutembelea  miradi na kusema usahuri alioutoa kwenye kituo cha afya Kigamboni  kumewezesha kurahisisha utoaji huduma na kwamba anamshukuru Mhe. Rais kwa kutoa fedha za uboreshwaji wa huduma za afya ambazo zimewanufaisha wananchi wa Kigamboni.

Mbunge wa Kigamboni Mhe. Faustine Ndungulile ameshukuru Serikali ya Awamu ya tano kwa kuwekeza Kigamboni na kuwapongeza watendaji kwa usimamizi mzuri wa miradi na  kutoa rai kuhakikisha wanaendelea kusimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maendeleo na fedha zinazotolewa na Serikali.

Mkurugenzi wa Kigamboni Arch.Ng’wilabuzu Ludigija amesema Kigamboni imefarijika sana kwa kupata miradi hususani ya afya kwani  tangu ukamilikaji wa majengo na utoaji wa huduma za mama na mtoto Kituo cha Afya Kigamboni tayari kimeweza kufanya upasuaji kwa wamama 218.

Kwa upande wa soko la kibada Mklurugenzi amesema  hadi ujenzi kukamika kiasi cha Bilioni 6.6 kitatumika  na kwamba Manispaa imejipanga kusimamia mradi ili uweze kukamilka kwa wakati kwa lengo la kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi nakuongeza pato kwa Manispaa.



Mkurugenzi wa Kigamboni Arch.Ng'wilabuzu Ludigija  kulia akitoa maelezo mafupi juu ya ujenzi wa soko hilo la Kisasa

Mhe. Josephat Kandege akipongeza jitihada za ujenzi wa Soko la Kibada.

Ziara ikiendelea kwenye Soko la Kibada

Muonekano wa ndani ya soko

Viongozi wakitoka kukagua mradi wa Soko, kutoka kushoto ni Mkurugenzi Manispaa ya Kigamboni Arch. Ng'wilabuzu Ludigija , Naibu waziri TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege na Mbunge wa Kigamboni Mhe. Faustine ndungulile.

ujenzi ukiendelea

Naibu waziri TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege akizungumza kwa uchache juu ya ubooreshwaji wa kituo cha Afya Kigamboni

Viongozi wakitoka kukagua jengo la upasuaji.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa