• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Naibu Waziri wa Afya Mh.Ndugulile akabidhi vitanda na magodoro 14 Vijibweni Hospitali

Posted on: May 16th, 2018

Naibu waziri wa Afya,Wazee jinsia na watoto na Mbunge wa Manispaa ya Kigamboni Mhe.Faustine Ndugulile amekabidhi vitanda na magodoro 14 vinavyotarajiwa kuhudumia wagonjwa wa dharula kwenye  Hospitali  ya Vijibweni na kuwataka wataalamu kuvitumia vitanda hivyo kwa lengo lililokusudiwa.

Mhe.Ndugulile ameyasema hayo leo alipokuwa akikabidhi vitanda alivyopokea kutoka kwa jamii ya Australia (Australia Tanzania society) na kampuni ya JACANA ikiwa ni  matokeo ya mkakati ambayo Serikali inashirikisha sekta binafsi katika hali ya utoaji wa huduma za Afya.

Amemtaka  Mkurugenzi wa Manispa ya Kigamboni na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni  kusimamia mapato na kuhakikisha mifumo ya kudhibiti mapato  inafungwa kwenye vituo vyotevya afya  ili fedha zitakazopatikana zitumike kuboresha huduma nyingine  za afya.

Aidha Mhe.Ndugulile amesisitiza ofisi ya Mkurugenzi kuweka mfumo mzuri wa malalamiko ili kuwarahisishia wananchi wanaokuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma kujua waende kwa nani kuweza kuhudumiwa na kusikilizwa malalamiko yao.

“ Mkurugenzi Mtendaji,Mganga Mkuu wa Wilaya na Mganga Mfawidhi wekeni tangazo la namba za simu kwenye bango i ili mwananchi akiwa na malalamiko ajue anampigia simu nani, tunataka uwazi na uwajibkaji kwenye serikali ya awamu ya tano”. Amesema Mhe.Ndugulile

Pia Naibu Waziri  amesema ni vizuri  Wilaya na  hospitali  kujipanga na kuhakikisha dawa zote za msingi zinakuwepo kwa mujibu wa muongozo, Serikali imeongeza bajeti ya dawa kutoka  Biloni 30 hadi Bilioni 66, bajeti ya dawa imeongezeka mara hivyo inahitaji dawa hizo ziwanufaishe wananchi , sambamba na hilo ameagiza duka la dawa lifunguliwe na kutoa  miezi sita kukamilisha zoezi hilo.

Naibu Waziri pia amewapongeza watumishi wa Hospitali ya Vijibweni na kuwataka kufanya kazi kwa kujitoa na kuwahudumia wananchi kwa lugha nzuri mbali na uchache wa watumishi walionao,huku akihitaji idadi ya watumishi wanaohitajika.

“Rushwa , matusi nisingependa kusikia na sitakubali kutolea tarifa za ubora wa huduma sehemu nyingine lakini kwangu hakupo vizuri, Mkurugenzi na Mganga Mkuu simamia hilo, mtu yeyote atakayebainika hatutashindwa kumshughulikia”Amesema Mh.Ngugulile

Afisa uhusiano wa JACANA Bw.Ahmed Merere amesema sera zao ni kujali jamii kila mahali wanapofanya kazi ,wanataka kuona jamii zinakuwa bora na mikakati yao ni kuchangia katika masuala ya afya, elimu , maendeleo ya jamii hususani miradi ya kinamama na Vijana, hivyo ni faraja kwao kukabidhi vitanda hivyo.

Hospitali ya Vijibweni imeanzishwa mwaka 20016 na inahudumia wagonjwa 430 kwa siku sawa na wagonjwa 154,800 kwa mwaka.

kutoka kushoto ni Naibu waziri wa Afya na Mbunge wa Kigamboni Mh.Faustine Ndugulile ,Bw.James Chialo Mkurugenzi wa Australia Tanzania Society,  Afisa Uhusiano wa JACANA Bw.Ahmed Merere,  Meya wa Manispaa Mh.Hoja Maabad wakipokea vitanda

Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa Kigamboni Mh.Faustine Ndugulile wa kwanza kushoto akipeana mkono wa shukurani na Afisa Uhusiano wa JACANA wakati wa Makabidhiano ya vitanda.

Naibu Waziri wa Afya akiwasisitiza watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia maadili.

Naibu Waziri wa Afya akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi na Mganga Mkuu wa  Wilaya ya Kigamboni.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh. Hoja Maabad akiwashukuru wafadhili kwa msaada wa vitanda

Afisa uhusiano  Bw.Ahmed Merere kutoka JACANA akizungumzia lengo la kusaidia Hospitali ya Vijibweni .

Baadhi ya Vitanda vya kuhudumia wagonjwa wa dharula vilivyokabidhiwa Hospitali ya Vijibweni leo na Naibu Waziri wa Afya.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa