• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Naibu Waziri TAMISEMI asisitiza kuzingatia muongozo ujenzi wa vituo vya Afya.

Posted on: October 2nd, 2018

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI  Mhe. Josephat Kandege ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Kigamboni kujenga  majengo ya Kituo cha Afya Kigamboni kwa kufuata ramani ya sasa inayotumika kwenye vituo vyote Tanzania nzima.

Maelekezo hayo ameyatoa leo alipotembelea kituo hicho cha afya na kubaini kuwa jengo la upasuaji halijaungana na jengo la mama na mtoto na kumtaka Mkuu wa Wilaya kusimamia ujenzi wa majengo hayo kwa kuhakikisha yanaungana kama muongozo unavyoelekeza.

“  Ramani inayotumika ilikuwa bado haijafanyiwa maboresho nimeelekeza majengo yajengwe  kwa kuzingatia ramani ya sasa yaani jengo moja linakuwa na chumba cha  upasuaji na jengo la mama na mtoto,ni matarajio yetu kwamba mama anapojifungua iwe  kwa njia ya  kawaida au kwa upasuaji tukikutana naye tukute ana mtoto ili kupunguza adha kwa mama hususani katika kipindi hiki ambacho huduma za mama na mtoto zinasogezwa karibu” Alisema Naibu Waziri.

Akizungumzia eneo la soko katika kata ya Kibada, Naibu Waziri amesema kuwa eneo lipo vizuri na ukubwa unatosheleza, zaidi ni kuhakikisha wanafatilia maandiko  ili ujenzi wa soko uanze mara moja, kwasababu linatarajia kuwa chanzo cha uhakika cha mapato kwa Halmashuari na kuondoa adha kwa wananchi kwa kwenda umbali mrefu kufata huduma na wafanyabiashara kupeleka bidhaa zao .

Aliongeza kuwa eneo la stendi  liongezwe kama wataalamu walivyoeleza kwa kufikia  mita  za mrada 16000 ambalo litakidhi haja na kuwa stendi ya uhakika  lakini pia  chanzo cha mapato cha uhakika kwa Halmasuri husika.

Kwa upande wa  ujenzi wa jengo la Halmashauri amesema kuwa   ujenzi unaendelea vizuri lakini hajapata taarifa nzuri ya  kasi ya ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwasababu ya kuchelewa kupata  majibu ya sampuli ya kupima udongo lakini wamekubaliana kuwa kasi ya kuchimba msingi itaongezeka.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri amesema kuwa  maelekzo yote yaliyotolewa na Naibu waziri atakaa na wasaidizi wake  kwa kushirikiana na Mkurugenzi na kwamba marekebisho ya haraka yatafanyika kwenye kituo cha Afya ili kukidhi vigezo vya ramani iliyotolewa  kwasababu ujenzi bado upo kwenye hatua za awali.

Naibu Waziri amefanya ziara ya kutembelea miradi inayotekelezwa na Wilaya  ya Kigamboni ambayo italeta tija kwaajili ya kusaidia  wananchi, ambapo alitembelea eneo linalotarajiwa kujengwa soko na stendi lililopo Kata ya  Kibada, ujenzi wa jengo la Utawala linalojengwa Somangila na upanuzi wa kituo cha afya cha Kigamboni.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni (kulia) Arch.Ngw'ilabuzu Ludigija  akimpokea Naibu Waziri TAMISEMI Mhe.Josephat Kandege alipowasili kwenye ofisi za Wilaya ya Kigamboni.

Naibu waziri Tamisemi Mhe. Josephat Kandege akizungumza na viongozi na baadhi ya watumishi mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za Wilaya ya Kigamboni.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akitoa  utangulizi  kwa Naibu Waziri TAMISEMI alipofika kwenye ofisi yake Kabla ya kuanza ziara yake .

Mchumi Ruperto M. Mboya  (Mratibu wa uwekezaji) akielezea mpango wa ujenzi wa soko na stendi ya mabasi itakayojengwa Kata ya Kibada.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ngw'ilabuzu Ludigija  akitoa maelezo ya ujenzi wa soko la kisasa Kata ya Kibada.

Naibu Waziri TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege na Mkurugenzi wa Manispaa Arch.Ngw'ilabuzu Ludigija wakitazama ramani ya ujenzi wa soko la kisasa litakalojengwa Kata Kibada.

Mhandisi wa Manispaa Bw.Pius Mtechura akitoa maelekezo ya mpangilio wa majengo katika ramani kwa Naibu Waziri TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege.

Ukaguzi wa ujenzi jengo la utala ukiendelea

Naibu Waziri TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege mwenye suti ya kijivu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa jengo la utawala.

Naibu waziri TAMISEMI akiwa ameambata na viongozi mbalimbali wakitoka kuangalia maendeleo ya ujenzi wa jengo la utawala Somangila.

Naibu waziri TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege wa kwanza kushoto akitazama eneo la ujenzi wa jengo la mama na mtoto

Eneo linalojengwa jengo la  mama na mtoto na mafundi wakiendeleana kazi.

ukaguzi wa eneo la ujenzi wa jengo la upasuaji .

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa