• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mmefanya vizuri kwa awamu zilizopita, naomba mmalizie sehemu iliyobaki vizuri zaidi.Waziri Nape.

Posted on: May 18th, 2022

Hongereni Wilaya ya Kigambon kwa kutekeleza vizuri zoezi la Anuani za makazi kwa awamu ya kwanza na ya pili, sehemu iliyobaki naomba mtekeleze vizuri zaidi’

Ni kauli ya waziri wa habari na mawasiliano Mhe.Nape Nnauye wakati alipokua akitoa maelekezo matatu ya kufanyiwa kazi baada ya kupokea utekelezaji wa zoezi la anuani la makazi wilaya ya kigamboni  kwenye ukumbi wa mkuu wa wilaya ya kigamboni wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa zoezi.

Waziri Nape amesema kuwa Kigamboni imetekeleza vizuri sana katika zoezi hili na kuwaomba kuendelea kufanya vizuri zaidi katika zoezi lililobaki la kuweka vibao vya namba kwenye kila nyumba na nguzo za barabara .

Wazri Nape ameongeza kwa kusema kuwa baadhI ya maeneo ambayo yanamigogoro ya umiliki  kama maeneo ya jeshi, uwekezaji, hospitAli na mengineyo ,anauni za makazi hazitawekwa hadi migogoro hiyo itakapopatiwa ufumbuzi kwani kwa kuweka anuani wakati kunamigogoro ni kuhalalisha umiliki kinyume cha taratibu.

Aidha amesema kuwa viongozi wahakikishe majina ya mitaa yanaamuliwa na wananchi  sambamba na kuhakikisha majina yanayotumika yaweze kutunza historia ya eneo husika na viongozi kutakiwa kuhakikisha wanashawishi wananchi kuridhia majina yanayoonekana kutunza historia ya maeneo yao.

Waziri amewataka viongozi kuanzia ngazi ya Wilaya hadi wajumbe wa nyumba kumi kuhakikisha wanahamasisha wananchi kushirki kwenye zoezi hili la anuan za makakazi kwani kuna nyakati zitafika mwananchi hataweza kupata huduma mbalimbali kama asipokuwa na anuani inayomtambulisha.

Naye Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. David Silinde ametumia fursa hiyo kuzitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinakamilisha zoezi la anunani za makazi kabla ya  kufikia mei 30 kwani hakuna sababu itakayopelekea Halmashauri yoyote kushindwa kufikia malengo kwaua miongozo ya utekelezaji yote imekwishatolewa ikiwemo ya kutumia fedha za mapato ya ndani.

‘Niweke wazi Halmashauri itakayoshindwa kufikia malengo hatutasita kuichukulia hatua za kinidhamu”Alisema Naibu Waziri.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amosi Makalla meshukru ujio wa Waziri na Naibu Waziri na kusema kuwa kwa ngazi ya Mkoa zoezi limetekeleza kwa namna yake na wapo tayari kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangassa ameshukuru kwa ziara ya kikazi ya viongozi iliyolenga kukagua utekelezaji wa zoezi na kuahidi kuyafanyia kazi malelekezo yote yaliyotolewa ili kufikia lengo la Serikali lililowekwa.

Ikumbukwe Kigamboni ilikadiria kuzifikia anuani za nyumba 49,353 anunani zilizoingizwa kwenye mfumo ni 58,508 sawa na 118.5%, Makadirio ya barabara yalikuwa 1,864 na zilizoingizwa kwenye mfumo 3,617, idadi ya barabara zilizowekwa nguzo ni 85 ambapo 26 zimewekwa katika zoezi hili na 59 ziliwekwa na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) mwaka 2018. Jumla ya namba za majengo ya makazi na Ofisi za Serikali 47 zimewekwa.Aidha Wilaya ya Kigamboni ilishika nafasi ya kwanza katika zoezi la Ukusanyaji wa taarifa za Anuani na Makazi.


Waziri wa Habari Mhe. Nape NNauye akikagua uwekwaji wavibao vya namba na anuani kwenye ofisi za Serikali ya Mtaa wa Feri .


Viongozi akiwa kwenye Mtaa wa Feri kukagua utekelezaji wa zoezi la uwekaji vibao vya barabara.

Waziri wa Habari na Mawasiliano Mhe. Nape NNauye akiipongeza Kigamboni na kutoa rai ya kumaliza vizuri utekelezaji wa sehemu iliyobaki.


Baadhi ya Viongozi na watumishi waliofika ofisi za Mkuu wa Wilaya Kigamboni kumpokea na kumsikiliza Waziri wa Habari na Mawasiliano Mhe.Nape Nnauye.


Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe.David Silinde akitoa maelekezo ya utekelezaji wa zoezi la anuani za makazi nchi nzima.


Diwani wa Kata ya Kigamboni Mhe. Dotto Msawa akiwaelezea viongozi namna anavyotekeleza zoezi la anuani za makazi kwenye Kata yake.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akizungumzia mkoa namna ulivyofanikisha zoezi na Kuipongeza Kigamboni kwa kuongoza kimkoa kwenye utekelezaji wa Anuani za Makazi.


Mkuu wa Wialaya ya Kigamboni akikaribisha viongozi na kupoea malekezo ya uboreshaji wa utekelezaji wa Anuani za makazi kwa sehemu iliyobakia.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa