• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni awataka wananchi kuwa na utaratibu wa kupima Afya

Posted on: June 7th, 2022

Hayo yamejiri Leo katika viwanja vya Mjimwema katika uzinduzi wa zoezi la upimaji wa afya bure ambapo Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma Almas Nyangasa alikuwa Mgeni Rasmi.


Akiongea katika zoezi hilo litakalochukua siku mbili mfululizo Leo jumanne 7 Juni na jumatano 8 Juni Mhe.Nyangasa amewataka wananchi wa Kigamboni kujenga tabia ya kucheki afya zao mara Kwa mara ili kujitambua mapema iwapo wana maradhi katika miili yao ili kujitibia mapema kabla tatizo halijawa kubwa kwani ,Matatizo ya kiafya ni makubwa na changamoto hii imekua kutokana na kutofatilia afya zetu mara Kwa mara Kwa kuzichunguza ili kutatua tatizo mapema.


Pamoja na hayo Mheshimiwa DC ametoa tahadhari katika kuendelea kujikinga na tatizo la Uvico 19 na kuwasihi kuendelee kuchukua tahadhari ikiwepo kupata chanjo ambayo inapatikana pia katika zoezi hilo, aidha amewataka kuendelea kuwataarifu na wengine kufika kupata huduma.


Aidha amemshukuru mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha kupatikana Kwa huduma hizi kupitia maagizo yake Kwa watendaji wake wa chini na uhusiano mzuri na wadau.


Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amepata nafasi ya kutembelea mabanda yote ya Wadau waliokuwapo hapo( likiwepo Banda la Kigamboni Manispaa ambapo wanatoa elimu ya lishe Kwa ajili ya kulinda afya na kuepukana na magonjwa) wakitoa huduma bure na kupata maelezo ya kina kuhusu huduma zinazotolewa .Amewashukuru wadau wote waliojitokeza kufanikisha zoezi hili na kuwataka kuendelee kuwa na moyo wa kujitolea.


Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Lucas David Ngamtwa,amewashukuru  wadau waliojitokeza kutoa huduma bure,aidha amewasisitizia wananchi waendelee kufika  kwani  zoezi linaendelea ambapo  kutakuwa na madaktari mbalimbali bingwa kutoka muhimbili watakaotoa huduma za uchunguzi wa afya.


Nae Naibu Meya wa Manispaa ya kigamboni Mhe.Stephano  Warioba Kwa niaba ya Mstahiki Meya amewashukuru watoa huduma ya kucheki afya,amewataka wananchi kuzingatia ushauri watakaoupata ili kuepuka kupata matatizo zaidi ,amewataka wananchi kufika kwa wingi kupima afya zao ,na kuwataarifu na  wenzao kuhusu zoezi hili ili waje kwa wingi kuangalia afya zao.


Wadau mbalimbali wameshiriki kutoa huduma ya upimaji afya bure wakiwepo Management for Health Development ( MHD) ambao wametoa sapoti kubwa kuwezesha zoezi hilo lakini pia wametoa huduma ya utoaji chanjo ya  Uvico 19, akiongea Mratibu wa chanjo Kwa wilaya ya Kigamboni ndg.Martha Nkya wao amesema wako bega Kwa bega katika kuunga mkono juhudi za serikali katika masuala ya afya ili kujenga taifa lenye watu wenye afya na kuleta maendeleo.







Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa