• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mkuu wa Wilaya Kigamboni awatoa hofu wananchi wanaochoma chanjo ya uviko19 .

Posted on: August 5th, 2021

“Niwatoe hofu chanjo ni salama, hapa nilipo ninawiki mbili tangu nichanjwe naendelea na shughuli zangu nawashauri kutumia nafasi hii kupata chanjo hususani makundi ainishwa”

Ni kauli ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Nyangassa  leo alipokuwa akizindua zoezi la utoaji chanjo lililofanyika kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni iliyopo Gezaulole na kusema kuwa chanjo ni hiari lakini ni jambo la muhimu hasa kwa kuangalia nchi zilizotutangulia kupata chanjo namna ambavyo wameweza kupata matokea chanya ya kupunguza vifo.

Mkuu wa Wilaya amesema Kuwa chanjo iliyoletwa ni 1500 lakini  mpaka sasa siku ya tatu chanjo tayari ni pungufu ya 1000 hivyo, ni lazima wananchi kuelewa kuwa hili ni jambo muhimu hasa kwa makundi ambayo yamepewa kipaumbele.

“Jukumu la afya ni la mtu binafsi, sisi kama Binadamu tunafanya kadri Mungu anavyotujalia ili kulinda afya zetu, ni lazima tuelewa madhira mengine ya chanjo ni matokeo ambayo yanaweza kutokea hata kwa chanjo nyingine kwasababu binadamu tumetofautiana” alisema Fatma

Aidha Mkuu wa Wilaya amatoa rai kwa  wataalamu wa Afya  na waliokwisha pata chanjo kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya uelewa wa umuhimu wa chanjo, faida zake  na mahali zinapopatikana ili kusaidia chanjo kuwafikia wananchi wengi kwani lengo ni kuhakikisha watanzania wanakuwa salama.

Ameongeza kwa kusema kuwa wananchi wote hata ambao wamekwisha kupata chanjo wanatakiwa kuendelea kuchukua tahadhari zinazoelekezwa ili kuendela kujikinga na maabukizi ya UVIKO 19

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kigamboni Henry Chaula amesema kuwa ni vyema wananchi wakafuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu badala ya kusikiliza maneno yamitandaoni na kusema kuwa wao kama viongozi  wanaunga mkono msimamo wa Serikali kuhusu umuhimu wa wananchi kupatiwa chanjo.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Dkt.Ikaji Rashid amesema kuwa Manispaa imepokea Jumla ya dozi 1500 kwa kuanzia ambazo zimepelekwa kwenye maeneo ya kutolea chanjo ya Hospitali ya Wilaya Kigamboni dozi 500, Hospitali ya Vijibweni Dozi 500, Zahanati ya Kibada dozi 300 na kituo cha afya Kimbiji Dozi 200 na dozi nyingine zitaletwa kadri ya mahitaji.

Ameongeza kuwa chanjo inatolewa kwa watumishi wa afya,watu wenye umri zaidi ya 50 na  wenye magonjwa sugu ambapo  tangu chanjo imeanza kutolewa kwa siku mbili  jumla ya wahudumu wa afya na wananchi 509 wamepatiwa chanjo kwa hiari yao .

Uzinduzi ulihudhuriwa na viongozi wa Chama cha mapinduzi ngazi ya Wilaya,  Madiwani, viongozi wa dini, wananchi na wataalamu wa Wilaya ya Kigamboni.


Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Dkt.Ikaji Rashid akimuelezea Mkuu wa Wilaya na viongozi wengine namna utaratibu wa kupata chanjo unavyofanyika tangu mteja anavyopokelewa.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma Almasi Nyangassa akikata utepe sanduku lililohifadhiwa chanjo ishara ya uzinduzi rasmi wa utoaji chanjo.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma Almasi Nyangassa akifungua sanduku lenye chanjo mara baada ya kukata utepe wa ufunguzi ili kujiridhisha na uwepo wa chanjo hizo.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma Almasi Nyangassa akishirikiana na muhudumu wa afya kunyanyua sanduku la chanjo ishara ya kufuhia uzinduzi rasmi wa chanjo ya Uviko 19


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya Bw. Henry Chaula akipokea chanjo mara baada ya uzinduzi


Mwananchi Christoms Malingumu akipokea chanjo mara baada ya ufunguzi


Mkuu wa Idara ya Kilimo na Umwagiliaji Priscilla Mhina akipokea chanjo mara baada ya uzinduzi.


Katibu wa CCM Wilaya Bw. Evarist Mluge akipatiwa chanjo mara baada ya ufunguzi.

Diwani wa Kata ya Mjimwema  Mhe.Omary Ngurangwa akipata chanjo mara baada ya uzinduzi.


Diwani viti maalumu Elizabeth Kimambo akipata chanjo mara baada ya uzinduzi.


Kaimu Mkuu wa Idara ya Mipango miji na Maliasili Said Swalehe akipata chanjo mara baada ya ufunguzi.


Naibu Meya na Diwani wa Kata ya Somangila Mhe. Stephano Waryoba akipata chanjo wakati wa uzinduzi.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa