• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mkurugenzi Manispaa ya Kigamboni apokea msaada wa Milion 20 kutoka NMB

Posted on: July 17th, 2019

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ng’wilabuzu Ludigija leo amepokea msaada wa madawati  150 na bando 14 za mabati zenye thamani ya Milioni 20 kutoka Benki ya NMB  ikiwa ni  sehemu ya benki ya kurejesha faida kwa jamii.


Akipokea msaada huo kwenye shule ya Msingi Mjimwema Mkurugenzi amesema kuwa ,Wilaya ya Kigamboni  ni mpya bado ina mahitaji ya miundo mbinu ikiwa ni pamoja na madawati sababu kumekua na idadi kubwa ya wanafunzi wanaojiunga darasa la kwanza na kidato cha kwanza,hivyo ni imani yake kunapokua na  wadau kama NMB wanaounga mkono  Serikali inafarijika kwani hawataki kuona mtoto anakaa chini sababu  ufundishaji unakua mgumu.


Mkurugenzi amesema kuwa NMB wamekua na ushirikiano mzuri na wamekuwa wakisaidia Manispaa katika  huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na  vitanda vya kujifungulia na oparasheni  walivyotoa hivi karibuni kwenye  kituo cha Afya Kigamboni .


 “NMB wamekua karibu kila mwaka wanatusaidia na sio mara moja hivyo tunashukuru pia kwa msaada huu wa madawati, Nashukuru na naahidi nitaendelea kushirikiana nanyi katika kuhakikisha kigamboni inakua na maendeleo”Amesema Mkurugenzi


Ameongeza kuwa  Kutokana na mchango mkubwa  unaoupata  Manispaa kutoka NMB, Manispaa   inataka washirikiane nao kwa kiasi kikubwa ndio maana kutokana na changamoto mbalimbali inayokabiliana nazo imeamua  kufungua akaunti ambayo itawezesha kukusanyia mapato ya ndani lakini pia asilimia 10 inayoenda kuwezesha makundi maalumu ya vijana wanawake na walemvu itakua ikipitia NMB na mikopo itakapokuwa inatolewa itatokea huko.


Mkurugenzi amewashukuru pia walimu kwa jitihada wanazofanya za kutoa elimu kwa wanafunzi mbali na changamoto wanazokabiliana nazo na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa weredi kwani anatambua na kuthamini mchango wao katika ukuaji wa Elimu.


Mkuu wa Mahusiano Serikalini (NMB) Bi. Vicky Bishobu amesema  anashukuru  na kupongeza jitihada ambazo zinafanywa  katika kukuza elimu,pia kuona NMB ni mahali ambapo  Manispaa imeweza kwenda kuomba  ushirikiano ili waweze kuwa  sehemu ya jitihada nzuri  katika kukuza sekta ya elimu”


Bi.Vicky Bishobu amesema kuwa  Benki inakabidhi madawati 150 yenye thamani ya milioni 15  kwenye Shule za Msingi za Ufukoni ,Kibugumo na Amani gomvi  na mabati bando  14 yenye thamani ya  Milioni 5 na kusema kuwa wanaamini kuwa dawati 1 wanaka wanafunzi 5  haitakua imemaliza tatizo  lakini imepunguza kwa kiasi  jitihada za kuhakikisha wanafunzi wanakua na mazingira mazuri ya kusoma .

Aidha amesema kuwa kwa niaba ya Benki anamshukuru Mkurugenzi  kwamba tangia amekuja amewaunga mkono na amekuwa mwepesi  katika kujibu maombi yao ya kutaka kushirikiana zaidi na serikali hasa kusaidia katika jitihada za kukusanya mapato  kwenye Halmashauri na Vituo vya Afya ambapo  hatua iliyofikiwa ni nzuri na wameridhika nayo.


“ ni kitu ambacho hatukua nacho, kwa niaba ya Benki naomba uendelee kutuamini  na utupe nafasi  ili tuweze kushirikiana na kuhakikisha kwamba mianya yote  ya kupotea kwa mapato  inazibwa na sisi tunakua sehemu ya jitihada nzuri ya kuboresha mapato ili kuhakikisha huduma za kijamii zinakua nzuri”. Amesema Vicky


Tunashukuru pia kwa kuitikia wito wa kuchangamkia fursa katika benki tunaendelea kuhakikisha huduma zetu zinabioreshwa zaidi ili kuona ni sehemu ya kupata huduma  nzuri, msisite kutushirikisha maeneo mengine ambayo Benki inaweza ikafanyia kazi.


Akisoma taarifa ya miundombinu ya Shule za Msingi na Sekondari kwa niaba ya Afisa elimu Wilaya Frank Makingi (Afisa elimu Vifaa na takwimu) Amesema kuwa Hali ya miundombinu katika shule bado haikidhi mahitaji kulingana na idadi ya wanafunzi waliopo shuleni  hivyo wadau mablimbali wa ndani na nje ya Halmashauri wanaendelea kualikwa kuunga mkono katika kuboresha miumbombinu ya madawati, vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo ili  mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji  shuleni yawe bora.







Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa