• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mkurugenzi Kigamboni aungana na wananchi kuhitimisha juma la usafi Feri.

Posted on: June 12th, 2019

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni leo ameungana na wadau wa usafi kampuni ya Green waste na wafanyabiashara wa Kigamboni Feri kuhitimisha juma la Usafi kwa kusafisha mitaro na Barabara.


Akizungumza baada ya kukamilika kwa usafi huo Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ng’wilabuzu Ludigija amesema Halmashauri ya Manispaa imeona vyema kuhitimisha wiki ya mazingira na kuwakumbusha wananchi kufanaya usafi ili kujikinga ma magonjwa ya mlipuko yatokanayo na uchafu.


Ameongeza kuwa kampuni ya usafi ya Green waste ni wadau wa Kigamboni na kwamba viufaa vyao vya kisasa walivyonavyo vitasaidia kwa kiwango kikubwa kuweka Kigamboni safi lakini pia wananchi na wafanyabiashara wanao wajibu kuhakikisha maeneo yao ni masafi na wale wanaoishi kando ya barabara na mitaro hawatupi taka ovyo kwenye maeneo hayo.

“Wiki iliyopita tulifanya usafi kwenye mitaro yote ya Feri na kunyunyizia dawa ili kuua vimelea vya mbu vinavyosababisha ugonjwa wa dengue,Wananchi waone ni wajibu wao kuweka mazingira safi sio kusubiri hadi viongozi waje ndio waanze kuchukua hatua za usafi”Amesema Mkurugenzi


Aidha amesema amewaagiza watendaji wa Kata, Mitaa na Maafisa afya wote kuhakikisha wanasimamia suala la usafi wa mazingira ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu kuhusu usafi wa kila mwisho wa mwezi na kwamba wale watakaoshindwa kutekeleza watalazimishwa.


Diwani wa Kata ya Kigamboni Mhe.Dotto Msawa amesema kuwa baada ya kuingia mkataba na kampuni ya usafi ya Green waste anatarajia kuwa Kigamboni inaenda kuwa ile aliyoitarajia na kuamini sasa itakua ya kwanza kwenye suala zima la usafi sababu kampuni hiyo inavifaa vya kisasa na wafanyakazi wa kutosha na kwamba hata changamoto ya ukusanyaji wa maji taka inaenda kutatuliwa sababu kampuni hiyo itasaidia kuleta magari yatakayokuwa yanavuta taka hizo.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Green Waste Bw. Allan Sudi Amesema Manispaa imetoa mkataba wa kufanya usafi ambapo kwa kuanza wanaanza na Kata ya Kigamboni na baadae kusogea kwenye Kata 5 na kwamba wamejipanga kuhakikisha wanasambaza makasha ya kutosha ya kuhifadhia taka, kutoa eleimu kwa wananchi ya utunzaji mazingira na utupaji taka na kuchakata taka kabla ya kupeleka dampo ambapo eneo hilo la uchakataji wameomba Manispaa iwapatie.


Mkuu wa Idara ya Mazingira Manispaa ya Kigamboni Juvenalis Mauna amesema Manispaa itahakikisha kila mwananchi anafata taratibu za uhifadhi taka, kulipa tozo ikiwa ni pamoja na kutupa taka maeneo elekzi ili kuweka Mazingira safi kwa ustawi wa afya kwa ujumla.

Mkurugenzi wa Manispaa mwenye suti ya kijivu Arch.Ng'wilabuzu Ludigija  akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya usafi ya Green waste wakipanga mikakati ya kuweka Kigamboni safi

Diwani wa Kata ya Kigamboni Mhe. Dotto Msawa mwenye kofia ya kijivuakishirikiana na wananchi wa Feri kufanya usafi

Mkurugenzi wa Manispaa Arch.Ng'wilabuzu Ludigija kushoto akisaidiana na Afisa Mazingira wa Manispaa Juvenalus mauna wakiweka uchafu kwenye gari la kukusanyia taka.

wafanyakazi wa green waste wakikusanya taka na kuziweka kwenye gari la kubebea taka hizo

usafi ukiendelea

wafanyakazi wa Manispaa na kampuni ya Green waste  wakiendelea na usafi

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa