• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mkurugenzi Kigamboni aonya watumishi wasio waadilifu

Posted on: July 2nd, 2019

Mkurugenzi wa Mnaispaa ya Kigamboni Arch.Ng’wilabuzu Ludigija amewataka watumishi wa Hospitali ya Vijibweni na watumishi wote kwa ujumla kuepuka vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa bidii wakizingatia sheria taratibu na kanuni pamoja na  ubunifu kazini.

Ameyazungumza hayo leo alipokuwa kwenye kikao cha watumishi wa h

Hospitali ya Vijibweni leo kkilichofanyika kwenye ukumbi wa Hospitali , Mkurugenzi amesema anataka kuona huduma za afya zinabadilika kwa kutolewa kwa upendo na ikiwezekana kuondoa ile dhana iliyopo kwa baadhi ya wananchi wanaoamini  huduma bora za afya hazipatikani kwenye hospitali za Serikali.

Mkurugenzi amesema kuwa anajua watumishi wanaohudumu ni wachache lakini kwa uchache huohuo anawataka kufanya kazi kwa weredi kwa  kuzingatia kanuni za utendaji kazi huku akisisitiza kuwa utumishi wa umma ni Utii kwa viongozi wanaowaongoza mbali na mapungufu ambayo wanaweza kuwanayo hao wanaowaongoza.

Aidha Mkurugenzi amewataka watumishi ambao wanafanya kazi kwa weredi kuwaripoti watumishi wanaowashawisishi kutokufanya kazi kwasababu ya masalahi ya posho na kwamba wakimbaini mtumishi wa namna hiyo wawe huru kumripoti kwa Mkurugenzi ili aweze kumchukulia hatua stahiki kwa kuleta ushawishi mbaya kwa watumishi.

Mkurugenzi amesema anatamani kuona Kigamboni inakuwa ya Mfano kwa utoaji mzuri wa huduma za afya kuanzia mapokezi mpaka mwisho wa huduma ili watu watoke maeneo mbalimbali kuja kujifunza namna kazi zinatekelezwa na sio uwepo wa majungu unaosababisha kushuka kwa ufanisi wa baadhi ya watendaji wazuri wa kazi unaosababishwa na watendaji wachache ambao hawajui thamani yao ya nafasi walizopatiwa.

“Natamani mama mjamzito anayekuja kuhudumiwa leba aone kama ni sehemu salama na nzuri kwake, vifo vitakavyojitokeza viwe kwa bahati mbaya lakini sio vya kusababishwa na mtumishi kwa utoaji mbaya wa huduma”Alisema Mkurugenzi.

Aidha Mkurugenzi amesisitiza kuwa upandishwaji wa vyeo kwa watumishi kwa sasa utazingatia utendaji kazi wa mtumishi ikiwa ni pamoja na uwajibikaji wake uliopo kwenye mpango kazi na kwamba ili akupandishe cheo ni lazima vyombo vya usalama vihusike ili kujiridhisha na mwenendo wako wa kikazi.

“kupanda vyeo sio kama zamani kwamba ukifika muda Fulani ni lazima upande, sasahivi ni lazima upimwe,na mimi napenda watumishi wawajibikaji na wanaojituma , mtumishi anayetekeleza wajibu wake kwa ukamilifu nipo tayari kumpigania kwa namna yoyote ile” alisema Mkurugenzi.

Wakati huohuo Mkurugenzi amemtaka Mganga Mkuu wa Wilaya kuwa ndio mtoaji wa ED (EXCEMPTION FROM DUTY) kutokana na uhuru mbaya wanaotumia watumishi kwa kutumia kigezo hicho na kwenda kufanya kazi kwenye hospitali binafsi hali na kusema kuwa huo ni uvivu na utumizi mbaya wa  mishahara inayotolewa na Serikali bila kuifanyia kazi.

Mkurugenzi amewataka wajumbe wa menejimenti ya Hospitali (CHMT) kuwa washauri kwa Mkurugenzi na warekebishaji  na sio kuondoa thamani ya utendaji kazi wa vituo na kuwataka watumishi wote,Makatibu wa Afya  kufanya majukumu yao kwa weredi.

watumishi wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi

watumishi wa afya wakimsikiliza Mkurugenzi kwa umakini

Baadhi ya watumishi

Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt CHarles Mkombachepa  akipokea maagizo kutoka kwa Mkurugenzi na kuahidi kuyatendea kazi.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa