• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mkurugenzi aainisha maeneo ya kupeleka Mifuko ya Plastiki kwa wakazi wa Kigamboni

Posted on: May 30th, 2019

Katika kuelekea kilele cha mwisho Wa matumizi ya mifuko ya plastiki JUNI 1 Mkurugenzi Wa Manispaa ya Kigamboni Leo amepokea makasha(dustbin) mawili kutoka kampuni ya usafi ya green waste ya kuhifadhia mifuko ya plastiki yatayowekwa kwenye Kituo cha daladala Feri.

Akizungumza wakati Wa mapokezi ya makasha hayo Mkurugenzi Wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ng'wilabuzu Ludigija amesema katika kutekeleza agizo la Makamu Wa Rais Green waste imetoa mapipa hayo ambayo yatakuwa msaada mkubwa kwenye eneo la feri ambalo kuna wafanyabiashara wengi na mzunguko mkubwa wa watu.

" ili wote tukae kwenye Mazingira safi lazima kutekeleza kwa pamoja agizo kusitisha matumizi haya ya mifuko " alisema Mkurugenzi

Ameongeza kuwa Kigamboni kama Manispaa ingependa kuendesha zoezi hilo kwa Amani na asingependa kufikia hatua ya kufikishana kwenye faini hali ambayo haitapendeza.

Mkurugenzi amesema amepita kwenye mduka na soko la feri kuwakumbusha wafanyabiashara juu ya kutii agizo bila shuruti na kusema kuwa katika kata zote 9 na mitaa 67 watendaji na wenyeviti watakusanya mifuko itakayohifadhiwa kwenye stoo ya mbwa maji na baadae kupelekwa kwenye maeneo husika ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu kwa wananchi .

Kwa upande wake meneja wa kampuni ya Green waste Bw. Allan Saudi amesema makasha (dustbin) waliyotoa ni mwanzo wa kuweka mazingira safi ya Kigamboni ambapo wameomba yatumike kwenye zoezi la ukusanyaji wa mifuko pekee na baadae wataleta mapipa mengine kwa kuhifadhia taka ngumu .

“Tunamshukuru mkurugenzi na wananchi wa Kigamboni kwa ktupokea vizuri haya makasha tuliyotoa leo nimwanzo tu, tunayo mengi sana tutayaleta hapa Kigamboni tulisha sikia miaka ya nyuma kido alipo kuja aliye kuwa Rais wa Marekani Barack Obama hadi bara bara zilipigwa deki tuanataka sasa hayo yafanyike hapa na kuanzia tarehe saba mtaona haya”Alisema Sud.

Aidha Afisa Mazingira wa Mnispaa ya Kigamboni Juvelus Mauna ,aliesema kupokelewa kwa makasha hayo nimoja ya hatua za kuelekea maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani .

Boda boda wa kituo cha ferry wamesema hawatambeba abiria yeyote atakaye kuwa na mfuko wa Plastick kuanzia juni mosi mwaka huu.

makasha yaliyotolewa na kampuni ya kufanya usafi ya Green waste.

Ziara kueleeka kwenye maduka na soko la feri

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch. Ng'wilabuzu Ludigija akizungumza na baadhi ya wamiliki wa maduka  kuhusu kutii agizo la matumizi ya mifuko mbadala.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Mhandisi. Ng'Wilabuzu Ludigija akimsisitiza jambo mwenyekiti wa soko la feri alipotembelea kukumbusha matumizi ya mifuko ya plastiki.

Mwenyekiti wa Soko la Feri akimtoa hofu mkurugenzi juu ya utekelzaji wa agizo la Serikali

ukaguzi wa mitaro inayohifadhi mifuko ya plastiki inayopepea


Wafanyakazi wa Kampuni ya Usafi ya Green waste wakikokota makasha kwaajili ya kupeleka mahali yatakayokuwa yamewekwa kwa kuwekea mifuko

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa