• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Milioni 400 ilivyoboresha upatikanaji wa huduma za Afya kwa Wananchi kituo cha Afya Kigamboni

Posted on: October 5th, 2020


Ikiwa ni mwendelezo wa Serikali wa kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa kwa wananchi wote, Halmshauri ya Manispaa Kigamboni Julai 2018 ilipokea tena  kiasi cha shilingi Milioni 400 kutoka Serikali kuu ili kuboresha kituo cha afya Kigamboni ambacho kabla ya upanuzi kilikua na changamoto ya kuzidiwa na wagonjwa hali iliyopelekea  kudhoofu kwa  utolewaji wa huduma.

Upanuzi wa kituo cha afya kigamboni umefanikisha kuongeza majengo ya mama na mtoto, jengo la kuhifadhia maiti ambalo halikuwepo hapo awali, jengo la upasuaji na maabara ya kisasa yenye vifaa vyote ambapo hadi sasa ujenzi umekamilika na huduma zote zimeanza kutolewa.

Mganga Mfawidhi wa kituo hiki cha Afya Kigamboni Dkt. Sophinias Ngonyani alisema kuwa, uboreshwaji wa kituo hicho kwanza kumewezesha kuboresha mazingira ya kazi, lakini pia kusogeza huduma kwa wananchi hususani huduma hii ya mama na mtoto.

Maganga aliongeza kusema kuwa awali kabla ya majengo hayo kujengwa walikuwa na chumba kimoja cha kuzalishia ambapo kwa wastani walikuwa wakizalisha wazazi 40-50 kwa mwezi lakini baada ya uboreshwaji wameweza kuzalisha wazazi 200 – 250 na jengo hilo linyeuwezo wa kuchua wazazi 8 ambao wanaweza kujifungua kwa wakati mmoja.

Huduma za upasuaji ambazo zilikuwa hazipatikani hapo awali zimeanza kutolewa tangu 1/12/2019 ambapo hadi kufikia june 2020 jumla ya wagonjwa 280 wameweza kufanyiwa upasuaji wa wazazi na magonjwa ya kinamama ambao kabla ya huduma hiyo iliwalazimu kupewa rufaa kwenda Temeke au Muhimbili.

Mganga mfawidhi ameshukuru Serikali kwa kuboresha huduma za Afya na kusema kuwa maabara ya kisasa yenye vifaa vyote imewezesha kutoa huduma nzuri na kwa wakati, na jengo la kuhifadhia maiti ambalo halikuwepo awali limewezesha wananchi kuhifadhi miili ya ndugu zao na kupata muda wa kujipanga namna bora ya kuweza kuendesha misiba pindi inapotokea.

 Uboreshaji wa kituo hiki umewezesha wananchi kupata huduma zote bora na kwa wakati hususani kupunguza vifo vya mama na mtoto pamoja na kupunguza  kuzidiwa kwa wagonjwa kulikokuwa kunasababishwa na ufinyu wa majengo ya kutolea huduma.


muonekano wa Maabara kwa ndani.

Maabara

Maabara

Vifaa vya Maabara

Vifaa vya maabara

Jengo la upasuaji

wodi ya wazazi

Chumba cha kuhifadhia maiti

Gari la wagonjwa la kituo cha Afya Kigamboni

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa