• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mbunge na Naibu waziri wa Afya Dkt.Faustine akabidhi gari ya kubebea wagonjwa Hospitali ya Vijibweni

Posted on: July 11th, 2019

Mbunge wa Kigamboni na Naibu waziri wa Afya Wazee Jinsia na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile jana amekabidhi ambulance (gari ya kubebea wagonjwa) kwenye hospitali ya Vijibweni kwa kushirikiana na Ubalozi wa Australia nchini Tanzania (Autsralia Tanzania society)  kwa lengo la kutoa huduma nzuri kwa wananchi wa Kigamboni .

Wakikabidhi gari hilo Dkt.Faustine alisema kuwa anaomba gari hilo  litumike  kwa malengo yaliyokusudiwa kwani hatarajii  kukuta au kuelezwa  kuwa linafanya kazi kinyume na taratibu kwasababu  lengo lake ni kuhakikisha sekta ya afya  inasimamiwa imara  na ikiwezekana Kigamboni iwe ya Mfano

“Kigamboni ni Wilaya Mpya ila inapiga hatua kwa haraka sana,Napenda mtu akija kigamboni kwenye suala la afya aone kweli huu ni mfano ambao unaweza kuigwa sehemu nyingine yoyote , tusijekukuta gari hizi zinabeba mikaa huko” alisema Dkt.Faustine

Aidha Mbunge alitoa rai kwa watumishi wa afya wa Manispaa ya Kigamboni  kuendelea kutoa huduma kwa upendo , kuhakikisha dawa zinakuwepo na kutumia lugha nzuri kwa wagonjwa wanaokuja kupata huduma kwenye vituo vyao vya kutolea huduma.

Aliongeza kuwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya unaendelea , Serikali ilitoa Bilion 1.5 na Bajeti ya juzi wameongeza milioni 500, vilevile kwa kipindi cha awamu hii ya nne ya uongozi Zahanati nne za Kijaka,Kigogo, Pembamnazi na Buyuni zimafanikiwa kuzinduliwa na kuanza kufanya kazi.

Mbunge aliongeza kuwa ili Kigamboni izidi kukua inahitaji wawekezaji na tayari watu wa Autralia wamegundua uwepo wa madini eneo la KisaraweII na kwamba kwa kulitambua hilo Serikali imetoa Milioni 90 kwaajili ya kuboresha miundombinu ya barabara itakayorahisisha usafirishaji.

Kwaupande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri aliwashukuru watu wa Australia kwa kuikumbuka Kigamboni na kusema kuwa  bado uhitaji wa magari ya wagonjwa upo , kwanye matarajio yao ya kuleta gari zingine 10 basi waikumbuke tena kigamboni hata kwa magari mawili.

Aidha kwa kipekee alimpongeza Mbunge Dkt.Faustine Ndungulile kwa kuipambania Kigamboni  kwenye suala la afya ambapo hadi sasa ina jumla ya magari 5 ya kubebea wagonjwa , pia ametekeleza ahadi nyingi kwa wapiga kura na kwakupitia jitihada hizo wananchi wananufaika sana na Wilaya ya Kigamboni.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni  Arch.Ng’wilabuzu Ludigija amemshukuru Naibu waziri wa Afya na watu wa Australia kwa msaada walioutoa na kusema kwamba uhitaji bado ni mkubwa , kupatikana kwa gari hilo kutasaidia kuokoa maisha ya wananchi wa Kigamboni.

“Naibu waziri huyu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kigamboni  tunamshukuru na anastahili kupongezwa anafanya kazi bila kuchoka na amekua msaada mkubwa kwetu, kwa niaba ya wananchi wa Kigamboni  tunakushukuru kwa namna unavyoendelea kutupambania” Alisema Mkurugenzi

Australia Tanzania Society wanashirikiana na Wizara ya afya wazee jinsia na watoto kuboresha huduma za afya na hivi karibuni wanatarajia kuleta magari mengine 10 ya kubebea wagonjwa yatakayopelekwa maeneo mengine yenye uhitaji.

Mbunge wa Jimbo la Kigamboni na Naibu waziri wa Afya Dkt.Faustine Ndungulile akizungumza na watumishi na uongozi wa Kigam,boni kabla ya kukabidhi gari la wagonjwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akishukuru Mbunge na Australia kwa msaada wa gari hilo na kuomba msaada wa kuongezewa gari 2 nyingine pale itakapowezekana.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ng'wilabuzu ludigija akishukuru ubalozi wa Australia kwa msaada walioutoa kwenye hospitali ya Vijibweni

Viongozi wakishuhudia gari kwa muonekano wa ndani

Mwenyekiti wa Australia Tanzania society Bw. Didier Murcia akionesha muonekano wa gari hilo kwa ndani.

Muonekano wa gari kwa ndani

muonekano wa gari kwa nje

mwenyekiti wa Australia Tanzania society Bw. Didier Murcia akitoa maelekezo matumizi ya eneo la kuhifadhia oxygen

Naibu waziri wa Afya na Mbunge wa Kigamboni Dkt. Faustine Ndugulile akimshukuru mwenyekiti wa Australia Tanzania society Bw. Didier Murcia  kwa msaada walioutoa Kigmaboni

Picha ya pamoja  baada ya makabidhiano

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa