• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Wakulima wawezeshwe badala ya kukatishwa tamaa" Waziri wa Viwanda"

Posted on: August 4th, 2018

Waziri wa Viwanda,Biashara na uwekezaji Mh.Charles Mwijage ameagiza wakuu wa mikoa, wakurugenzi wa majiji na Halmashauri zote nchini kuandaa mpango utakaowawezesha kuwadhamini wakulima na hata watumishi katika mikoa na Halmashauri zao ili waweze kuwakopesha vifaa vya kilimo.

 Waziri Mwijage amesema serikali imeagiza matrekta 250 kwa ajili ya kuwakopesha wakulima kote nchini na kwambani jukumu la Halmashauri kujua ni nani anastahili kukopeshwa na kusimamia urejeshaji wa mikopo hiyo.

Agizo hilo limetolewa alipokuwa akizindumaonesho ya nanenane kanda ya kati leo ambapo pia, Mh.Mwijage ameziomba taasisi za serikali zinazofanya kazi za udhibiti ubora kama TFDA,TBS ziwasaidie wazalishaji wakubwa na wadogo badala ya kuwafungia au kuwanyima vibali kama baadhi ya taasisi zinavyofanya.

 “Nyie ndio jicho la serikali, muwasaidie wakulima na wafugaji kufikia malengo yao badala ya kuwakatisha tamaa” alisema Mh.Mwijage.

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ni mojawapo kati ya halmashauri sita  katika mkoa wa Dar Es salaama ikiwa ni  halmashauri kubwa kijografia ikiwa na ukubwa wa kilometa za mrabaShughuli kuu za kiuchumi za wananchi wa kigamboni ni biashara, uvuvi katika bahari ya Hindi , kilimo pamoja na ufugaji wa mifugo wa aina mbali mbali. Mifugo hii hufugwa katika njia mbali mbali za kisasa na za asili kulingana na eneo husika  kwani mpaka sasa yapo baadhi ya maeneo ya Kigamboni yenye muonekano wa vijiji na hivyo kuruhusu watu kufuga kiasili. Mifugo inayofugwa ni kama vile ng’ombe, kuku, mbuzi, kondoo pamoja na samaki

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni inashiriki maonesho ya wakulima nane nane kwa mara ya pili tangu kuanzishwa kwake waka 2016, ambapo rai kubwa ni kuwahamasisha wananchi na wawekezaji kuja kuwekeza ndani ya ardhi ya Manispaa ya kigamboni kwasababu, kuna  ardhi ya kutosha ya kuwekeza kwa  maeneo ya viwanda,  kilimo Mjini, maegesho ya magari na viwanja vya makazi.

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imeweza kuudhirishia umma kuwa kilimo mjini inawezekana kwani shughuli mbalimbali na mazao yaliooneshwa kustawi ndani ya ardhi ya Kigamboni kwenye maonesho ya wakulima nanenane mwaka 2018  imetoa fursa kwa wananchi kuwekeza ili kuendana na kauli mbiu ya mwaka 2018 ya "Wekeza katika Kilimo,Mifugo na Uvuvi kwa maendeleo ya viwanda".


Waziri wa Viwanda Mhe.Charles Mwaijage akihutubia wananchi kwenye ufunguzi wa maonesho ya wakulima nanenane Mkoani Morogoro.

wanafunzi wa shule ya wakiwa pamoja na mwalimu wao walipotembelea banda la Kigamboni Mc.

Waziri wa Viwanda Mhe.Charles Mwaijage akikagua moja ya banda la wakulima kabla ya kufungua maonesho ya wakulima nanenane Morogoro  mwaka 2018


Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Mhe. Gulam Hussein Shaban Kifu akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Kigamboni kwenye maonesho ya nanenane, pembeni ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni Ndg.Stephen Katemba.

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Mhe. Gulam Hussein Shaban Kifu akinunua bidhaa kutoka kwa wajasiliamali wa Kigamboni , alipotembelea banda la wajasiliamali kuona shughuli zinazofanyika.

wataalamu wa kilimo wakitoa elimu ya kilimo kwa wageni walifika kujionea shughuli za kilimo zinazofanywa na Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni.

Zao la Bilinganya linavyostawi kwenye ardhi ya Kigamboni.

Watoto na wazazi waliofika kwenye banda la Kigamboni Kuona ufugaji wa kisasa wa samaki aina ya Sato

Baadhi ya mazao yanayostawi Manispaa ya Kigamboni.

mwananchi aliyetembelea banda la wajasilimali wa Manispaa ya Kigamboni akioneshwa bidhaa kablaya kuinunua.

Wanafunzi wa kidato cha kwanza kutoka morogoro waliofika kuona na kujifunza shughuli za kijasiliamali zinazofanywa na wananchi wa Kigamboni.

wanafunzi wakipewa elimu ya afya na mtaalam wa afya namna ambavyo mifugo inavyoweza kuepelea kuhatarisha afya zetu


Mtaalamu wa Kilimo akitoa elimu kwa wageni waliotembelea Banda la Kigamboni kwenye maonesho ya nanenane mwaka 2018

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa