• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Manispaa Kigamboni yatoa mafunzo kwa viongozi 700 wa VICOBA

Posted on: August 29th, 2023

Manispaa ya Kigamboni kupitia Idara ya maendeleo ya jamii imeaandaa mafunzo maalumu ya vikundi vya huduma ndogo za kifedha ( VICOBA) kwa lengo la kuwajengea uwezo wanavikundi juu ya sheria na kanuni ya huduma ndogo za kifedha na kuwakumbusha umuhimu wa kusajiliwa.


Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika leo Agosti 29, 2023  katika ukumbi wa Kibada Garden uliopo kata ya kibada, mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii Sigilinda Mdemu amesema kama idara waliona kuna haja ya kuandaa mafunzo hayo ili kuwapitisha viongozi na walimu wa VICOBA ili kujua sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa vikundi vya fedha.


"Tunataka wasajiliwe kwa sababu ni takwa la kisheria na ni kwa pande zote, vikundi vinapaswa kusajiliwa na walimu wanapaswa kuwa na leseni tumeona ni vyema viongozi wapate elimu hii ili waweze kuwa msaada kwenye vikundi hivyo," amesema Mdemu.


Amesema jumla ya viongozi 700 wamepatiwa mafunzo na kuelekezwa namna ya kusajili na kukata leseni kwa vikundi vyote ili kuweza kupata msaada wa kisheria pindi wanapopata changamoto.


" kikao hiki kitatoka na uwezeshaji wa umoja wa kifedha na jukwaa hili litapata fursa ya kusimamia mambo yao na kuzungumza kwa pamoja fursa zote za kifedha," ameongeza Mdemu.


Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Taifa Bi. Fatma Kange akitoa Salamu za Serikali amemuomba Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Halima Bulembo kuwapatia eneo la ardhi ili litumike na kina mama kuendesha shughuli za maendeleo ikiwemo uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo huku wakihamasisha wajasiliamali kutengeneza bidhaa zenye ubora na zilizopatiwa usajili BRELA.


Naye Mjumbe wa kamati ya bodi KIWASA (Kigamboni Wanawake SACCOS)  Bi. Meresiana Kimario amempongeza Mkurugenzi wa  Manispaa kwa kusimamia vyema ugawaji wa fedha za asilimia 10 za mapato ya ndani na akasema kuwa zimeongeza chachu katika kuwaletea maendeleo wanawake na kwa ustawi wa familia.


Jumla ya viongozi wa vikundi 243 wamepatiwa mafunzo hayo.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa