• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mambo5 msisitizo wa DC Fatma kwa Watendaji wa Manispaa ya kigamboni

Posted on: June 29th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangasa leo amefanya kikao kazi na wakuu wa Idara na vitengo, Watendaji wa Kata na Mitaa kwa lengo la kufahamiana lakini pia kuwekeana mikakati mizuri katika kuhakikisha lengo la Serikali linafikiwa.

Akizungumza na wataalamu hao kwenye ukumbi wa Manispaa Mhe. Fatma amesema kuwa kwanza angependa kuona ushirikianao unapewa kipaumbele katika kutekeleza majukumu ikiwemo kuona maeneo ya Mapato, Kero za wananchi, ulinzi na usalama, usafi pamoja na usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo (MKUUU) yanapewa kipaumbele.

Akizungumzia suala la ukusanyaji mapato Mhe. Fatma amesema kuwa ni vyema kuhakikisha vyanzo vyote vya mapato vilivyoainishwa vinakusanywa vizuri,kuongeza bidii ya kubuni vyanzo vipya vya mapato ambavyo vinaweza kuiongezea Manispaa Mapato,kuhakikisha mianya ya upotevu wa mapato yote inadhibitiwa kwa ukamilifu,pamoja na kudhibiti fedha za umma kwa kufanyi matumizi kwa kuzingatia taratibu na kanuni.

Kwa upande wa kushughulikia kero amewaasa Watendaji wa Kata na Mitaa kuepuka kuwa sehemu za migogoro na badala yake kuwa sehemu ya utatuzi kwa kusimamia haki,kuzingatia kufanya mikutano ya kisheria kwa ngazi za chini (Kata na Mitaa) na kutolea taarifa sahihi kwa wananchi.

Aidha amewataka Watendaji wa Kata na Mitaa kuhakikisha wanaainisha migogoro ya ardhi iliyopo kwenye maeneo yao kwa kuonesha chanzo na namna ambavyo wanapendekeza itatuliwe,  kuandalia taarifa na kuipeleka ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Ameongeza kwa kuwataka maafisa utumishi kutatua kero za watumishi kwa kuwafata mahali walipo na kwakuanzia amewataka maafisa hao kushughulikia kero zinazowakabili waalimu.

Eneo la ulinzi na usalama Mkuu wa Wilaya amesema Watendaji wa Kata na Mitaa ndio watu muhimu katika kuhakikisha ulinzi na usalama upo katika maeneo yao hivyo ni vyema wakaimarisha vikundi vya ulinzi na usalama vilivyopo kwenye maeneo yao, nakuhakikisha wanasimamia na kudhibiti upitishwaji wa bidhaa za magendo kwenye maeneo yao na uhamiaji haramu.

Katika suala la usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo amesema ni muhimu kuhakikisha wananchi wanashirikishwa katika utekelezaji wa miradi kwa kuwapa uelewa wa kutosha na kuwafanya waone wao kuwa ni sehemu ya miradi iliyopo kwenye maeneo yao.

Watendaji wa Kata na Mitaa kuhamasisha wananchi wa Kigamboni kuhusiana na kujilinda kwa kuchukua tahadhari dhidi ya wimbi la tatu la ugonjwa wa korona.

Kwaupande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Ndg. Erasto Kiwale amesema kuwa ,anaahidi kuhakikisha maelekezo yote yaliyotolewa kufanyiwa kazi kwa weredi na kwamba amefurahishwa na  neno la mkuu wa wilaya kutaka kuwa sehemu ya maendeleo ya Kigamboni na kuhimiza ushirikiano jambo ambalo ni jema katika ufanisi wa kazi .

Baadhi ya watendaji wakifatilia maelekezo ya Mkuu wa Wilaya kwa makini.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Erasto Kiwale akipokea maelekezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya na kumhakikishia utekekezaji kwa weredi.


Wataalamu wa Manispaa wakiendelea kuchukua maelekezo ya Mkuu wa Wilaya kwaajili ya utekelezaji.


Wataalamu wa Manispaa wakiendelea kufuatilia maelekezo ya  Mkuu wa Wilaya.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa