• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Mama lishe na Baba lishe wamshukuru Mhe. DC kwa kutatua na kusikiliza kero zao

Posted on: September 25th, 2023

Wafanya biashara wa Chakula (Mama na Baba Lishe) kata ya Pemba mnazi Leo Septemba 25,2023 wamemshukuru na kumpongeza  Mkuu wa wilaya ya  Kigamboni Mhe. Halima Bulembo kwa kutenga mda na kufanya ziara ya kuwatembelea kwenye maeneo yao ya biashara huku akipokea changamoto zinazowakabili na kuzitatua.


Akiwasilisha shukrani hizo kwa niaba ya baba na mama lishe Shabani Mwinyimkuu amesema amefurahishwa na namna ambavyo mkuu wa wilaya anafanya kazi zake huku akilenga kukutana na makundi ya watu wa chini ambayo ndiyo yenye changamoto nyingi huku akimtaka asiache kushuka kusikiliza kero za makundi mengine mara baada ya kumaliza hili kundi la Mama na Baba lishe.


Sambamba na hilo Mwinyimkuu ambaye ni Baba lishe wa mtaa wa Buyuni amemuomba Mkuu wa Wilaya hiyo kuwaunganisha wafanyabiashara wa kata ya Pemba Mnazi na kuwaweka sehemu moja huku akipendekeza eneo la sokoni kujengwa vibanda watakavyotumia wafanya biashara wote huku akisisitiza kuwa kwa kufanya hivyo kutaongeza tija kwenye biashara yao ya chakula huku wafanya biashara wa mboga na matunda wakinufaika kutokana na Muingiliano utakaokuwepo.


"Ili Serikali iweze kutuhudumia sisi Baba lishe na Mama lishe ni vyema mkatukusanya na kutuweka pamoja na kama itakupendeza utujengee vibanda kwenye eneo la soko ambapo kutakua na uwezekano wa wafanya biashara wote kukaa sehemu moja na hivyo kusababiisha mzunguko wa fedha kuwa mkubwa" Alisema Shabani Mwinyimkuu.


Sambamba na hilo bi. Asha Lyimo aliwasilisha ombi la kusaidiwa upatikanaji wa mikopo ili waweze kukuza mitaji yao na kuifanya biashara ya chakula kwa weledi na ufanisi wenye matokeo chanya kwa jamii na Serikali kwa  kuwawezesha kukusanya kodi husika kwa urahisi.


"Tunakuomba Mkuu wetu utusaidie kupata mikopo kwani mitaji yetu ni dhaifu na haikidhi kufanya biashara hii kwa viwango stahiki," Alisema.


Mkuu wa Wilaya hiyo Bi. Bulembo, alitumia  fursa hiyo kumuagiza Mkurugenzi wa Manispaa Erasto kiwale aliyewakilishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Sigilinda Mdemu kufanya marekebisho ya miundo mbinu ya soko la Tundwi Center ili kuzuia maji ya mvua kujaa ndani ya soko na kusababisha uharibifu wa bidhaa za wafanya biashara katika soko hilo.


"Mkurugenzi, nikuombe utafute namna ya kuwaondolea adha wafanya biashara hawa kwa sababu mvua zipo karibu kuanza ili tusiendelee kuwapa hasara zinazosababishwa na maji ya Mvua kuvujia kwenye bidhaa zao," Alisema DC Bulembo.


Samba na hilo, Mhe. Bulembo alimtaka Afisa Maendeleo kata kuwapitia watoa huduma za chakula na kuwapa elimu ya namna bora ya kupata mikopo ya serikali ili mara baada ya mchakato wa maboresho ya mikopo itakapokamilika  basi kundi hilo kwa kata ya pembamnazi liwe sehemu ya wanufaika huku akimsisitiza afisa biashara kuchukua maoni ya kutaka kuwekwa pamoja na kuyafanyia kazi.


Naye Afisa Afya  Manispaa ya  kigamboni Maua hayeshi alitoa elimu ya umuhimu wa kupima afya kwani sheria inawataka wafanya biashara wa chakula  kupima afya na kuzingatia usafi wa mazingira katika maeneo yao ya kazi huku akiwasisitiza umuhimu wa  kuvaa mavazi rasmi (sare) wakati wanapotekeleza majukumu yao.


Aidha Afisa Lishe (w) Bi. Henerietha  Kyomushula amewataka kuzingatia uaandaaji wa mapishi ulio sahihi ikiwemo kutoivisha mboga za majani kupita kiasi, huku akiwataka kuzingatia matumizi  madogo ya mafuta, sukari na chumvi ili kujiepusha na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo shinikizo la Damu.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa