• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

MAANDALIZI TAMASHA LA HAMASA YA SENSA YAWIVA

Posted on: August 11th, 2022

MAANDALIZI TAMASHA LA HAMASA KWA WANANCHI KUSHIRIKI SENSA YAWIVA,MKUU WA WILAYA YA KIGAMBONI APANGA MIKAKATI KWA KUSHIRIKISHA NGAZI ZOTE ZA WILAYA


Mkakati wa  Tamasha la kuhamasisha wananchi wa Wilaya ya Kigamboni kushiriki katika Sensa ya watu na  makazi unaendelea vizuri ambapo leo hii 10/8/2022 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni amekaa kikao na Viongozi mbalimbali wakiwepo na Wadau mbalimbali kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa Tamasha hilo.


Akiongea Mh.Fatma Almas Nyangasa  wakati  akifungua kikao hicho amesema kuwa zoezi la Sensa ni zoezi kubwa la kitaifa  ambapo serikali imefanya maandalizi makubwa kwa ajili ya kufanikisha zoezi hili ambapo kwa sasa maandalizi yapo kwenye hatua ya mwisho ya kutoa mafunzo kwa watakaoshiriki kupita nyumba kwa nyumba kuhesabu watu."Ni wajibu wetu sasa kuhamasisha wananchi wetu kushiriki kikamilifu katika zoezi hili ili liwe na ufanisi."alisema Nyangasa


Aidha ameongeza kuwa baadhi ya wananchi hawana uelewa kwa undani umuhimu wa zoezi hili hivyo kuna haja ya kuwahamasisha na kuwaelimisha kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwemo hii ambayo leo imetukusanya hapa ili kujadiliana kwa pamoja namna tutakavyotekeleza Tamasha hili lenye lengo la kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika kuhesabiwa.


Aidha aliwapa fursa kamati ndogo kutoa mapendekezo yao ili washiriki wa kikao waweze kutoa maoni yao na kuongezea mawazo yao katika kufanikisha utekelezaji.


Tamasha hili linatarajiwa kufanyika tarehe 20 ambapo siku sita kabla ya tamasha kutakuwa na utekelezaji wa shughuli mbalimbali kwenye kata za Kigamboni zenye lengo la kuhamasisha  wananchi kuelekea kilele siku ya tamasha.


Shughuli hizo zitahusisha jogging asubuhi kutoka ferry hadi Mji mwema kwa siku ya Kwanza 13/8/2022 ,tarehe 16/8/2022 uhamasishaji utafanyika Kisarawe II na Tundwi Songani,18/8/2022 uhamasishaji utafanyika Kimbiji na Dege,18/8/2022 kutakuwa na bonanza la mpira litakalofanyika viwanja vya Mji mwema,18/82022  Mkuu wa Wilaya ya kigamboni atakutana na makundi maalum ya watu wenye ulemavu katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya kigamboni,19/8/2022 Mkuu wa Wilaya atakutana na wavuvi saa 4:00 asubuhi na tarehe 20/8/2022 ndio itakuwa kilele na tamasha litafanyika katika viwanja vya mjimwema ambapo litaanza saa 5:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni.



Katika Tamasha hilo kutakuwa na upimaji wa afya ikiwepo upimaji na chanjo ya COVID na utoaji elimu ya lishe ,vilevile kutakuwa na michezo mbalimbali,wasanii watatumbuiza ,viongozi watatoa salam,fursa za wilaya ya kigamboni zitaongelewa.


Hivyo mwananchi wa kigamboni anza kujipanga kuhudhuria Tamasha hili litakalokuwa na mambo mengi yenye manufaa.


Kikao kimehudhuriwa na Mbunge wa Kigamboni Mh.Faustine Ndugulile,Katibu Tawala wa Wilaya ndg.James Mkumbo,Viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa,Kamati ya Ulinzi na usalama,viongozi wa dini,Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh.Ernest Mafimbo,na Madiwani,Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni ndg. Erasto Kiwale na menejimenti yake,watendaji wa Kata,Watendaji wa Mitaa,Viongozi wa kikundi cha wasanii,Mwenyekiti wa bodaboda,Mwenyekiti wa wenye malori,Mwenyekiti wa wafanyabiashara,Mwenyekiti wa wasanii. Kigamboni


Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano serikalini

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa