• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

MAABARA ,WODI YA KISASA KUJENGWA KIMBIJI

Posted on: January 16th, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni inatarajia kujenga Maabara,wodi ya mama na mtoto pamoja chumba cha upasuaji(Theater) katika kituo cha Afya cha Kimbiji kilichopo mtaa wa Kizito Huonjwa kata ya Kimbiji.

Ujenzi huo unatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi milioni 400 zilizotolewa na Ofisi ya Rais TAMISEMI katika mpango wa uboreshaji wa huduma za Afya nchini.

Timu ya ukaguzi toka ofisi ya Rais-TAMISEMI ikiongozwa na ndg Mwita Weibe ilifika kituoni hapo kuona hatua iliyofikiwa ambapo mpaka sasa eneo la ujenzi limeshasafishwa tayari kwa kuanza ujenzi. Ndg Mwita  alisisitiza kuwa Ofisi yake inatarajia kuona ujenzi huo unakamilika ndani ya miezi miwili kuanzia sasa ili kituo hicho kiweze kutoa huduma iliyokusudiwa.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ndg Renatus Mchau aliwahakikishia wajumbe hao toka Tamisemi kuwa mpaka kufikia mwezi Aprili 2018 ujenzi huo utakuwa umekamilika na kuanza kutumika. Ujenzi huo unatajiwa kusimamiwa na wataalam wa ujenzi wa manispaa kwa kuwatumia mafundi wa kawaida na pia kwa kuwashirikisha wananchi katika hatua zote za ujenzi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kimbiji Mh.Sanya Bunaya  amesema wao kama kata wamejipanga katika mitaa yote kushirikiana na mafundi katika shughuli ndogo ndogo kama kuchota maji, mchanga na kusomba matofali ili kupungiuza gharama za ujenzi na pia kwa kushirikiana na kamati ya uongozi wa kituo hicho kinachoongozwa na Mzee Ally Msumi ambao wote kwa pamoja wamekubaliana kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

Timu hiyo ya ukaguzi pia ilitembelea hospitali ya Vijibweni ambapo baada ya kuongea na watumishi wa hospitali hiyo ilikagua pia ujenzi wa chumba cha X-ray na Utra sound kinachojengwa hospitalini hapo. Mganga mkuu wa Manispaa ya Kigamboni Dr.Charles Mkombachepa alisema ujenzi huo unatajajiwa kukamilika ndani ya miezi miwili na kuanza kutumika ili kuwapunguzia wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kwenda kutafuta huduma hiyo nje ya Manispaa ya Kigamboni.



Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa