• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

LEAT yaishauri Kigamboni kuweka mikakati imara ya kudhibiti taka

Posted on: March 24th, 2021

Manispaa ya Kigamboni imeshauriwa kuwa na miundombinu wezeshi ili kuwa wadau namba moja wa kudhibiti taka kwa kuelimisha wananchi na kuweka walau vihifadhi taka kwenye Mitaa ili kuwawezesha wananchi kutupa taka kwenye vifaa hivyo maalumu ili kulinda mazingira.

 Hayo ameyazungumza muwezeshaji Baraka Thomas kutoka taasisi isiyokuwa ya kiserikali LEAT alipokuwa akitoa elimu ya mazingira kwa Mama lishe,Watendaji wa Kata na baadhi ya Mitaa na kusema kuwa,  tukiacha mazingira yakaharibika kana kwamba hayatuhusu tutasababisha kizazi kijacho kushindwa kuishi vizuri sababu ya uharibifu wa mazingira unaofanywa leo hivyo ni  vyema tukaonesha njia ili hata watoto wetu wajifunze kutoka kwetu.

 Baraka alisema kuwa uzalishaji taka umegawanyika kwenye makundi  mbalimbali kama Taka ngumu (solid waste), Taka za vimiminika (maji machafu),Taka za mfumo wa gesi, (mfano hewa za ukaa zinazalishwa viwandani),Taka hatarishi maranyingi zinaambatana na sumu mfano madawa vifaa vya mahospitali nk

Ameongeza kwa kusema kuwa Sheria ya mazingira inasema taka lazima zitenganishwe kwasababu makundi hayo yanatofautiana  namna ya kudhibiti, kuzalishwa na kusafirishwa  kwa kiwango kikubwa hivyo, ni vyema kuhakikisha tunadhibiti  taka husasani taka ngumu na vimimika kwenye ngazi ya Kata na Mitaa, kwani zinaathari kubwa zikiachwa kuzagaa zagaa.

Aliendelea kwa kusema Watendaji wa Kata na Mitaa wakumbuke wanawajibu wa kuhakikisha taka zinazozalishwa kwenye maeneo yao zinadhibitiwa lakini pia wananchi kupewa  uelewa wa umuhimu wa kutunza mazingira Ikiwa ni pamoja na kuzingatia kanuni ya tozo kwa kila anayezalisha taka na ndio maana sheria ndogo zimetungwa ili kusimamia usafi wa mazingira.

Aidha alisema, uteketezaji  taka majumbani unafanywa kwa njia ambayo sio sahihi kulingana na magawanyo wa taka uliopo kwani sio kila taka zinatakiwa kuchomwa sababu baadhi moshi wake ni sumu, hivyo ni muhimu kuzingatia uteketezaji wa taka.

“Wananchi waelimishwe kuacha kuzalishaza taka ambazo hazina ulazima na kuchukua tahadhari kabla ya kuzalisha taka ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza jitokeza ”

Aliongeza kusema  kadri watu wanavyoongezeka na uzalishaji wa taka unakua mkubwa hivyo tusipokuwa na mikakati ya kudhibiti taka, mazingira yetu yatakuwa machafu sana, kwani usafi wa mazingira unakupa nafasi ya utulivu, kuimarisha uwezo wa kufikiri hali inayopelekea  kuwa na kizazi chenye nguvu, akili na afya.

Kwa upande wake Diwani wa Vijibweni Mhe. Zacharia Mkundi Alisema anashukuru kwa elimu iliyotolewa, lakini wamegusa sehemu tu ya Manispaa  hivyo anapendekeza mradi huu kama ni wa muda mrefu ushuke ngazi za chini kabisa ili kuwe na uelewa wa pamoja mwisho wa siku  lengo lililokusudiwa liweze kufikiwa..

Mafunzo hayo yalitolewa jana kwenye ukumbi wa G5 na  taasisi isiyokuwa ya Kiserili inayofanya shughuli za ulinzi na uhifadhi mazingira na rasilimali za maliasili (LEAT) yaliyohusisha Kata za Kigamboni, Mjimwema,Tungi, Vijibweni, Kisarawe II na Kimbiji.


wataalamu kutoka Manispaa wakifatilia mafunzo


Diwani wa Kata ya Vijibweni Mhe. Zacharia Mkundi akishukuru LEAT kwa elimu waliyoitoa.


wataalamu ngazi ya Manispaa na wadau wengine wakifatilia mafunzo

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa