• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

LEAT kushirikiana na Serikali kutatua changamoto za kimazingiraa kwa ustawi wa afya za wananchi

Posted on: January 20th, 2021

Wataalamu kutoka Taasisi  isiyokuwa ya Kiserili inayofanya shughuli  za ulinzi na uhifadhi mazingira  na rasilimali za maliasili (LEAT) kwa kushirikiana na watalaamu wa Manispaa  Leo wamefika Manispaa ya Kigamboni Kata ya Vijibweni kwa lengo la kubaini changamoto za kimazingira  na kutoa mapendekezo ya  namna ya kutatua changamoto hizo.

 Akizungumza na wataalamu kutoka LEAT Mara baada ya kutembelea  eneo la  wazi lililopo Vijibweni  linalomilikiwa na mtu binafsi na kutumika kama eneo la kutupa taka  Diwani wa Kata ya Vijibweni Mhe. Zakaria Mkundi amesema kuwa uharibifu unaoonekana kwenye eneo lililopo pembezoni mwa Bahari ulikuwa mkubwa lakini  Manispaa imepambana kuhakikisha wananchi wanaacha kutupa taka maeneo ambayo hayajaainishwa kisheria.

Mhe. Mkundi ameongeza kwa kusema kuwa kama Manispaa imeandaa eneo maalumu litakaloruhusu wananchi kukusanya taka na kwenda kutupwa kwenye dampo la lingato lililopo Kisarawe II kwa lengo la kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

Aidha amesema utaratibu wa usafi wa kila jumamosi umesaidia kwa kiwango kikubwa kuhamasisha wananchi kufanya usafi na kufanya mazingira yao nadhifu.

" Natoa wito kwa wananchi wa Vijibweni na wanakigamboni kwa ujumla kutunza mazingira kwa ustawi wa afya zao kwani bila Afya hatuwezi kufanya shughuli zozote za kimaendeleo'' alisema Diwani.

Afisa Mazingira wa Manispaa ya Kigamboni Hussein Mwoma amesema kuwa kama wataalamu wamebaini watu wamekuwa wakivamia maeneo na kuchimba michanga na mashimo yanayobaki kutumika Kama dampo kinyume cha taratibu hivyo kama Manispaa inajipanga kutafuta wamiliki wa maeneo ya wazi ambao hawajayaendeleza  na kuweka ulinzi ili kuzuia matumizi yasiyosahihi yanayoleta athari kwa jamii.

Kwa upande wa mitaro inayoonekana kutuamisha maji, Hussein amesema taarifa itafika kwa TARURA ambao ndio wahusika wa Barbara za mitaa ili kuona namna bora itakayofanyika ili kuruhusu mitaro kuweza kufanya kazi ya kutiririsha maji kama ilivyokusudiwa.

Mtaalamu kutoka LEAT , Baraka Thomas ( wakili) amesema kuwa kama taasisi yenye lengo la kuhimiza usafi wa mazingira na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa wao kuwa sehemu ya usafi,  wapo tayari kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya mazingira ili kulinda afya na mazingira wanayoishi kwa kushirikiana katika kutatua changamoto zinazobainika kwenye maeneo yao.

LEAT imepata ufadhili  kwa Shirika la Legal Service Facility kuendesha  mradi kwa miaka miwili  wenye jina la " kulinda hali za kimazingira kwa wanawake,vijana, wasichana na jamii kwa ujumla kupitia kuwezesha jamii katika masuala ya kisheria jijini Dar es Salaam.

Mradi huu upo katika Manispaa zote 5 za Jiji la Dar es Salaam ambapo kwa Kigamboni awamu ya kwanza utafanyika katika kata za Kigamboni na Vijibweni.


Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa