• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Kila mwananchi Kigamboni anawajibika kwenye USAFI. DC Fatma

Posted on: November 26th, 2022

Kila mwananchi wa Kigamboni afahamu kuwa suala la usafi ni wajibu wa kila mtu, Tujitokeze kufanya usafi wa jumla kwani maeneo yote tunayofanya usafi tunayatumia.DC FATMA.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangassa ambaye ameongoza zoezi la usafi leo amesema, zoezi la usafi ni endelevu kuhakikisha Dar es Salaam inapendeza kama kauli mbiu yake inavyosema PENDEZESHA DAR ES SALAAM na Kigamboni inaendelea kuwa safi kwa kauli mbiu ya KIGAMBONI SAFI WAJIBU WANGU hivyo, kila mtu kwa nafasi yake iwe eneo la makazi, biashara au umma  wote tunawajibika kuhakikisha ni masafi.

Mkuu wa Wilaya amesema kila mtu aone anawajibika kushiriki kwenye usafi wa jumla na lakini kuhakikisha eneo lake  linakuwa safi kwani tukienda na mwenendo huu itarahisisha mwisho wa siku kutotumia muda mwingi kwenye usafi wa jumla bali kujiridhisha tu, kwani usafi unakuwa umekwisha fanyika.

Ameongeza kuwa iwe kwa  mfanyabiashara au sio, hakikisha eneo unalotumia ni safi na taka unazozalisha zinahifadhiwa na kuteketezwa vizuri kwenye eneo husika, hivyo amewaagiza  Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa kusimamia ili kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa na iwapo kunaikuikwaji wowote kuchukua hatua kwa kutumia sheria ndogondogo zinazoiongoza Manispaa.

“Tupo tayari kuchukua hatua stahiki kwa yeyote atakayekaidi, kwa sasa tunazungumza kirafiki kwasababu wewe ni mwananchi wetu ,hivyo timiza wajibu wako kuhakikisha mazingira yanakuwa safi” Alisema Mhe.Fatma.

Akiongelea kuhusu usafi wa Fukwe Mhe. Fatma amesema Fukwe ni fedha na ni uchumi hivyo amewaomba wananchi wanaofanya shughui zao kwenye maeneo hayo na wanaojipumzisha kuhakikisha wanaweka  mazingira safi mbali na mkakati uliopo ambao kama Serikali wamejipanga kuhakikisha fukwe zote zinakua safi.

Aidha amewataka wafanyabiashara wote wanaofanya biashara maeneo yasiyo rasmi kurejea kwenye maeneo yao waliyopangiwa na iwapo kunachangamoto zinazowakwamisha wawe tayari kuzifikisha ofisini ili zifanyiwe kazi kuliko kurejea kwenye maeneo ambayo tayari yamekatazwa kufanya biashara.

“Nirudie tena ni Marufuku kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi na yanafahamika”. Mhe. Fatma alisema

Madereva wa dalala dala pia wametakiwa kudhibiti utupaji taka hovyo hasa maeneo ya Barabarani kwa kuweka vitenga vya kuwekea taka ndani ya magari yao kuwezesha abiria kuzihifadhi humo.

Usafi wa Jumla wa mwisho wa mwezi huu wa kuminamoja umefanyika kwenye maeneo yote ya Barabara kuu za Kigamboni na maeneo yote ya Kata na Mitaa.

#KIGAMBONI SAFI, WAJIBU WANGU


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangassa  kulia na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni  Ndg.Erasto Kiwale wakishirikiana kukusanya taka ili kuzihifadhi kwenye kifaa maalumu baada ya kuzikusanya.


Mkuu wa Wilaya Mhe. Fatma Almasi Nyangassa akishirikiana na baadhi ya wananchi kwenye zoezi la ukusanyaji taka na kuzihifadhi kwenye chombo maalumu.


Baadhi ya wananchi waliojitokeza kufanya usafi wakisafisha mitaro ya barabara eneo la feri Kigamboni.

Zoezi la usafi likiendelea huku viongozi mbalimbali wakishiriki kwa kuongozwa na Mkuu wa Wilaya Mhe. Fatma Almasi Nyangassa.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kufanya usafi wakikusanya taka hizo na kuzihifadhi kwenye kifaa maalumu cha kukusanyia taka.


Mkuu wa Wilaya Mhe. Fatma Almasi Nyangassa akiwa ameambatana na mdau wa mazingira wakihifadhi taka kwenye chombo maalumu kilichowekwa mara baada ya kuzikusanya.


Mwananchi akikusanya taka kwaajili ya kuzipeleka sehemu maalumu ya kuhifadhia baada ya kufanya usafi.



Mandhari za barabara mara baada ya kufanyiwa usafi.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa