• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Kigamboni yasaini Mkataba na CRDB Benki wa kuwezesha wajasiliamali wadogo .

Posted on: September 17th, 2019


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri ameshukuru uongozi wa CRDB Benki kwa kukubali ombi la kuwawezesha wajasiliamali walio na vitambulisho vya ujasiliamali kwa kusaini mkataba utaowawezesha kutumia vitambulisho vyao kuwa dhamana ya kupata mikopo ili kuinua uchumi wao.

Akizungumza leo kwenye ukumbi wa mkutano ofisini kwake Gezaulole, Mhe Sara amesema kuwa anayofuraha  kuwa Kigamboni iliweza kutoa vitambulisho kwa wajasiliamali 22elfu na kwamba mfumo wa kitakwimu wa kuwatambua wafanyabiashara wote, mahali walipo na shughuli wanazofanya umefanyika  ambapo kwa kuanza wajasiliamali 3042 wataanza kupata mikopo kwenye uzinduzi wa awamu ya kwanza na kiasi cha Bilioni 10 zimetengwa kwaajili yao.

Mkuu wa Wilaya amesema kuwa Rais alilenga kutoa vitambulisho hivyo ili kuwajengea uwezo wafanyabiashara wadogo kuweza kutoa huduma kwenye miradi mikubwa ya kimkakati ambapo Kigamboni imeamua kutumia fursa hiyo ya kukipa thamani kitambulisho kwa kutumika kama dhamana ya kukopa ili kufikia lengo la Rais la kuwakwamua kiuchumi wananchi na wafanyabishara wadogowadogo  ambao walikuwa hawawezi kukopesheka bila kuwa na  dhamana za uhakika.

“Tunaishukuru CRDB kwa kukubali ombi letu na kuamua kuanza na Kigamboni , niwahakikishie hii mbegu mnayoipanda haitafutika na wajasiliamali wetu hawatawaangusha” Alisema Mkuu wa Wilaya

Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Kigamboni Ng’wilabuzu Ludigija amesema kuwa Ubunifu wa Vitambulisho hivi vya Rais leo unaleta matokeo chanya kwakua lengo kuu lilikua ni kuwawezesha wafanyabiashara  ambapo Kigamboni imeweza kuvipa thamani kuwa dhamana ya kupata mikopo na kwamba CRDB itawezesha kuwakopesha wajasiliamali kwa kima cha chini kuanzia 10,000 hadi 500,000.

Ameongeza kuwa huu ni ukombozi mkubwa kwa wajasiliamali na katika  safari ya kuelekea uchumi wa kati hawataki kumuacha mtu hata mmoja ndiomaana kitambulisho hicho kitawawezesha kupata huduma za kifedha na kwamba anaipongeza CRDB Benki kwa ubunifu wa kutumia fursa hiyo ambayo itakua ni mfano kwa benki nyingine .

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Benki Abdul Majid Nsekela amesema kuwa anampongeza Mkuu wa Wilaya na watendaji wake kwa ubunifu wa kuona namna bora yakukipa thamani  kitambulisho cha mfanyabiashara ili  kumkuza mjasiliamali mdogo katika kufikia uchumi wa kati.

Ameongeza kuwa CRDB ni Benki ya wote na kupitia Kigamboni huduma hii itasambaa nchi nzima hivyo CRDB ipo tayari kuwahudumia wafanyabiashara wadogo ambao kwa kundi kubwa ni wamachinga na kwamba kwa kushirikiana na watendaji wa Manispaa hadi sasa wameweza kusajili wajasiliamali 3000 kutoka makundi balimbali.

“Safari ya kuboresha maendeleo ya wajasiliamali inaanzia Kigamboni ,tunatarajia Benki yetu itawafikia na kuwawezesha wafanyabiashara kwa mitaji, elimu na uwekezaji kwa vikundi na mtu mmoja mmoja kwa kupata huduma bora  kwa urahisi na wakati wote na sasa tupo kwenye utoaji wa elimu ili kuwawezesha biashara zao kukua” Alisema Mkurugenzi wa CRDB Benki.

Mkurugenzi amesema kuwa wameamua kutumia mfumo wa kidigitali ili kuweza kuwafikia wajasiliamali wengi kwa kutumia mfumo wa simu akaunti ambao ni rahisi na hauna gharama katika utumiaji wake na kwamba CRDB imejipanga kuwahudumia ili kuwatoa kwenye hatua moja kwenda nyingine.


Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Benki Ndg.Abdul Majid Nsekela kushoto na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch. Ngw'ilabuzu Ludigija wakisaini mkataba wa kuwawezesha wajasiliamali wa Kigamboni leo kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya Gezaulole.

Mkurugenzi wa CRDB Benki kushoto Abdul Majid Nsekela akipeana mkono na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni kuashiria ushirikiano wao mara baada ya kuweka saini mkataba wa kuwezesha wajasiliamali wadogo





Mkurugenzi wa CRDB Benki Abdul Majid Nsekela akizungumza namna CRDB ilivyojipanga kuhakikisha huduma bora zinatolewa leo kwenye utiaji wa saini ya mkataba wa kuwezesha wajasiliamali






Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri akizungumza kabla ya utiaji wa saini mkataba wa kuwezesha wajasilimali wadogo wa Kigamboni



Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Arch.Ng'wilabuzu Ludigija akizungumza namna ambavyo vitambulisho vya wajasilimali vinakua mkombozi katika kuelekea uchumi wa kati

Picha ya pamoja na viongozi kutoka CRDB Benki na Wilaya ya Kigamboni mara baada ya kusaini mkataba

Baadhi ya watendaji wa CDRB na Manispaa ya Kigamboni

Baadhi ya watendaji wa Manispaa

baadhi ya watendaji wa Wilaya


Picha ya pamoja na wawakilishi wa wajasilimali na viongozi mara baada ya kusaini mkataba





Picha ya pamoja na kamati ya ulinzi na usalama

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa