• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

KIGAMBONI TAJIRI,KUNUFAIKA NA UWEKEZAJI HAUJAWAHI TOKEA AFRIKA MASHARIKI, VIJANA 50000 KUPATA AJIRA

Posted on: March 9th, 2022

Hayo yamebainishwa   9/3/2022 na Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na  biashara Mhe.Dkt.Ashatu Kijaji katika ukumbi wa Wilaya ya Kigamboni wakati wa tukio la kusaini mkataba wa  mauziano ya eneo la  square mita za mraba mil.2.2  lililopo Kisarawe II Kigamboni Kwa ajili ya uwekezaji mkubwa wa Kongani ya Viwanda ambao haujawahi kutokea Kati ya property international na kampuni ya Elsewedy ya Egypt.


Akizungumza katika hafla hiyo ya utiaji saini mkataba wa mauziano ili utekelezaji wa mradi uanze Mhe.Dkt.Ashatu Kijaji amesema mafanikio hayo ya mchakato wa kuanza kutekelezwa Kwa mradi huo ni matokeo ya jitihada za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ambapo amekuwa akiifungua Tanzania kiuchumi toka aingie madarakani.


Aidha amesema mradi huu unaenda kuifanya kigamboni kuwa tajiri kutokana na mapato yatakayopatikana kutoka katika Viwanda  vitakavyowekezwa katika eneo hilo ikiwepo Viwanda vya nguo,Viwanda vya kuunganisha magari ,kiwanda cha madawa ambapo tayari mwekezaji wa kiwanda cha madawa ameshasaini mkataba na Elsewedy Kwa ajili ya kuja kuwekeza katika eneo hili ,pamoja na hayo  fursa za ajira zitakazopatikana Kwa uwekezaji huu ni ajira 50,000.


Mhe Waziri amewataka watendaji kujiandaa na kazi hiyo njema na wananchi wafanye jitihada kuchukua fursa hii adimu kwani ni fursa ya uhakika Kwa kuwa tayari masoko ya uwekezaji huu yapo nje ya nchi Jambo ambalo litaiingizia nchi yetu fedha za kigeni.


Kwa upande wa miundo mbinu rafiki kuelekea eneo la mradi amesema serikali tayari imetenga fedha Kwa ajili ya kujenga barabara ya lami ya kilometa 11 kutoka Kibada mpaka eneo la mradi Kisarawe II na utekelezaji utaanza mara moja ili Kurahisisha utekelezaji wa mradi.


Nae katibu Mkuu wa Uwekezaji, Viwanda na biashara Prof.Godius Kahyarara katika hafla hiyo amewashukuru timu nzima iliyohusika katika kufanikisha mchakato huu hadi kufanikiwa wakiwepo wanasheria wa pande zote  mbili na Property International.


Aidha ameahidi kutoa Afisa katika ofisi yake atakaekuwa akifuatilia utekelezaji wa mradi huu kila siku mpaka kukamilika kwake ambapo amesema mradi utakamilika ndani ya miaka 2 .


Licha ya kuzungumzia manufaa mengi ya mradi huu Mhe.Fatma Almas Nyangasa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Rais Samia Suluhu Hassan Kwa maono yake ya kuifanya Tanzania yenye maendeleo kiuchumi na jitihada zake za  kuifungua nchi kiuchumi na kuwaletea maendeleo watanzania na tupo tayari kumuunga mkono Rais katika jitihada za kuiletea nchi maendeleo,akizungumzia kunufaika Kwa wanakigamboni na wananchi Kwa ujumla amesema wingi wa ajira Kwa vijana ,kuongezeka kwa mapato kutokana na Kodi amegusia pia faida itakayopatikana Kwa wanakigamboni kutoka Kwa wawekezaji kusaidia jamii(CSR)Kwa kurudisha faida Kwa jamii.Pia amewashukuru wote waliohusika na kushirikiana nao tangu kuanza Kwa mchakato huu , shukrani Kwa Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na biashara Mhe.Ashatu K.Kijaji, Katibu Mkuu wa Uwekezaji,Viwanda na biashara Prof.Godius Kahyarara na Property international.


Akifunga hafla hiyo Kwa kutoa shukrani Mhe.Ernest Mafimbo Meya wa Manispaa ya Kigamboni amemshukuru Mhe.Rais na serikali yake Kwa jitihada za dhati za kuiletea maendeleo Tanzania kiuchumi, akirejea katika tukio la uwekaji jiwe la msingi 6/12/2021 katika kiwanda cha vifaa vya umeme cha Elsewedy cha Kisarawe II ambapo Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan aliweka jiwe la msingi na kuwaambia wanakigamboni kuwa kuna kitu kinaendelea kinachohusu uwekezaji Kwa hapa kigamboni hivyo wananchi watarajie uwekezaji  mkubwa na kweli Leo hii tunashuhudia utiaji saini ili uwekezaji mkubwa wa aina yake kuanza ni furaha ilioje Kwa wanakigamboni ,yeye na Baraza la Madiwani wanaunga mkono juhudi zake .


Uwekezaji huu hadi kumalizika utagharimu Dola Bilioni 3,na Kwa awamu ya kwanza itatumika Dola milioni 400.Kwa awamu ya kwanza kutajengwa Viwanda 50 Hadi kukamilika vitakuwa Viwanda 100.Eneo ni la  square mita za mraba mil.2.2 litakuwa na huduma za jamii ndani,Viwanda vya nguo,madawa na vya kuunganisha magari,barabara na taa zake,mtandao wa mawasiliano,matanki makubwa ya maji n.k.


Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa