• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Kigamboni Manispaa yashika nafasi ya kwanza Kimkoa zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anuani za Makazi.

Posted on: April 21st, 2022

Katika kuhakikisha Halmashauri nchini zinafikia azma ya Rais Samia Suluhu Hassani ya kuhakikisha kila mwananchi  anakuwa na  anuani  ya makazi ifikapo mei 2022, Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imefanikiwa  kushika nasafi ya kwanza kimkoa kwa kufikia asilimia 102 za ukusanyaji wa taarifa za anuani za makazi.

Muwakilishi wa Mkurugenzi Charles Lawiso (Mwanasheria wa Manispaa) amebainisha hayo leo wakati alipokua akitoa mrejesho wa kazi nje ya Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mjimwema na kuwapongeza wawezeshaji wa zoezi na vijana kwa ujumla kwa kufanya kazi kwa umoja na ufanisi na kuifanya kigamboni kushika nafasi ya kwanza mbali na changamoto zilizowahi jitokeza.

Mwanasheria amesema kuwa walilenga kuzifikia anuani 49,353 lakini wameweza kuzifikia anuani 50,545 na kuongeza kuwa, kijiografia Kigamboni inaeneo kubwa na mahali kwingine kufikika kwake imekua ni changamoto lakini wawezeshaji na vijana waliofanya kazi ya kukusanya taarifa wamefanikiwa kuyafikia.

"Nawaasa Vijana ikitokea kazi yoyote fanyeni kwa  ufanisi, na sisi Manispaa tupo tayari kuwataumia katika matukio mengine ya kiserikali sababu tumeona ufanisi wenu" Alisema Mwanasheria

Kwa upande wake Muwezeshaji wa Manispaa Bi. Ariadina Peter amewapongeza vijana kwa kazi mbali na ugumu uliokuwepo lakini  waliweza  kuvumiliana na kubebana ili kuhakikisha  lengo la Serikali linafikiwa.

Ameongeza kwa kusema kuwa zoezi hili limewasaidia vijana kujifunza mambo mengi ikiwemo jinsi ya kuongea na jamii lakini pia namna ya kufanya kazi kwa kuisoma jamii na hilo wamelifanya vizuri na ndio maana wamefanikiwa kuvuka asilimia.

Akizungumza kwa niaba ya wakusanya taarifa Selemani Anexwa amesema, wanashukuru kwa nafasi waliyopewa kwani walikua vijana wengi lakini Manispaa ikawaona wanastahili kupata ajira hiyo ya muda mfupi sababu waliwaamini.

"Asanteni kwa kutufikiria kwa mambo mengine kama Sensa na sisi tupo tayari kufanya kwa ufanisi zaidi sio kwasababu ya fedha lakini kwa uzalendo tupo tayari kutekeleza kazi zingine mtakazoona zinafaa na tunaomba radhi kwa mahali popote ambapo tulikiuka maadili" Alisema Selemani.

Selwmani ameongeza kusema kuwa wao kama vijana wamejifunza mambo mengi mbali na kufanyakazi lakini wameweza kufamimiana na kutengeneza (mtandao)connection baina yao.

Halmashuri ya Manispaa ya Kigamboni ina Tarafa 3, Kata 9 na mitaa 67 ambayo kwa kiasi kikubwa yote imefikiwa na taarifa zimekusanywa. Ikimbukwe zoezi la ukusanyi wa Tarifa za anuani za makazi lilianza rasmi tarahe 4/03 mara baada ya uzinduzi wa Kiwilaya.


Msoma ramani Bi. sada akiwafafanulia ramani ya eneo walilopo  wakusanya taarifa za ananuani za makazi ili kuwawezesha vijana hao kutekelza jukumu lao.


Mandhari ya makazi ya Kigamboni.


Moja ya bango  linaloonesha uelekeo wa barabara.


Muwakilishi wa Mkurugenzi Bw. Charles Lawiso (Mwanasheria wa Manispaa) akitoa mrejesho wa kazi leo kwenye eneo la ofisi ya Mtendaji Kata ya Mjimwema na vijana wa ajira  ya muda waliokusanya taarifa za anuani za makazi.

Baadhi ya Vijana wa ajira ya muda waliokusanya taarifa za anuani za makazi wakisikiliza kwa makaini mrejesho wa kazi yao.



Vijana wakiwa kwenye moja ya mtaa kwa lengo la kuanisha nyumba na kukusanya taarifa za anuani za makazi

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa