• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Jukumu la Ulinzi wa watoto ni letu sote; DC Fatma

Posted on: June 16th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma almasi Nyangassa ameitaka jamii kutambua kuwa jukumu la ulinzi kwa watoto ni letu sote na hivyo ni vyema kuungana pamoja kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika kwenye viwanja vya shule ya msingi ya St.Joseph iliyopo kata ya Kibada Mhe.Fatma amesema kuwa  mtoto anapaswa kulindwa  bila kujali jinsia kwani malezi yameonesha watoto wa kike ndio waliopewa kipaumbele na wakiume kusahaulika .

Aidha amewataka walimu,wazazi na walezi kuhakikisha wanatoa taarifa za kikatili zinazohusu watoto na kuacha tabia za kuwaficha wahalifu kwani kwa kufanya hivyo kunapelekea Serikali kushindwa kuchukua hatua na kumyima mtoto haki yake ya kisheria.

"Mtindo wa maisha umebadilika wazazi wamekuwa watafutaji na walimu wamekua na muda mwingi na watoto, naomba walimu tulindieni watoto hawa, nawewe mzazi hatakama mda mwingi unautumia kwenye kazi haizuii jukumu lako kama mzazi kuwa karibu na mtoto wako, jenga tabia ya kumsikiliza na kumsaidia anapohitaji msaada" Alisema

 Mhe.Fatma.Ameongeza kwa kusema kuwa Serikali inamuangalia mtoto kwa jicho la mbali na ndiomaana kumekuwa na harakati za kumlinda hivyo jamii iungane katika  jitihada hizo ili Taifa litengeneze watoto wanaojielewa na viongozi bora wa hapo baadae.

Mhe Fatma pia amewataka watoto kuhakikisha wanakua wa kwanza kujilinda kwa kutoa taarifa  kwa wazazi, walezi na waalimu pindi wanapoona dalili za kufanyiwa vitendo vya kikatili ikiwa ni pamoja na kuacha tabia ya kupokea vitu/zawadi kwa watu wasiowajua.

Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Bi.Happy Luteganya amesema kuwa kumekuwa na harakati nyingi za kumkomboa mtoto dhidi ya ukatili hivyo ameiomba jamii kuungana na Serikali chini ya Waziri Dorooth Gwajima ili kufikia azma ya kutokomeza kabisa.


Kwaupande wake Diwani wa Kata ya Mjimwema na mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii Mhe. omary Ngurangwa  amesisitiza watoto kujitambua,kujilinda na kutoa taarifa dhidi ya vitendo vya kikatili kwani Taifa hili linawategema sana.

Maadhimisho haya yalijumuisha michezo mbalimbali na maigizo pamoja na utoaji vyeti kwa wadau mbalimbali wa maendeleo.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma Nyangassa akizungumza na wazazi, walezi na watoto kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika kwenye viwanja vya shule ya Msingi St.Joseph.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Fatma Nyangassa akifurahi pamoja na watoto akiwa ameambatana na  viongozi wengine.

Watoto Shule ya Msingi Kibada wakipita kwa maandamano.


Kaimu Mkurugenzi Bi.Happy Luteganya akizungumza  na walezi kuungana mkono jitihada za Serikali kutokomeza ukatili.


Wimbo wa  umuhimu wa kulinda mtoto wa kiume ukifanywa na wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Mizimbini.


Watoto wa shule ya msingi Mizimbini wakicheza mchezo wa kuvuta kamba



Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii na Diwani wa Kata ya Mjimwema Mhe.Omary Ngurangwa  na watoto

Watoto wakitoa ujumbe kwa njia ya bango


Watoto wakiigiza igizo la umuhimu wa Shule 



Mkuu wa Wilaya Mhe.Fatma Nyangassa akipanda mti kama kumbukumbu ya maadhimisho.


Wanafunzi wa Shule ya Msingi St.Joseph wakiwa kwenye onesho la ngoma




Kiongozi wa Shule ya Msingi St.Joseph Sister Teresia  akipanda mti kama kumbukumbu ya maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa