• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Jafo amewapongeza Vijana Baraka Erasto na Aboubakari Ali Aboubakari wamiliki wa chuo cha afya cha Kigamboni.

Posted on: July 2nd, 2019

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi (MB) Mhe. Selemani Jafo amewapongeza Vijana Baraka Erasto na Aboubakari Ali Aboubakari wamiliki wa chuo cha afya cha Kigamboni Healthy City Colledge kwa uzalenzo , ukomavu na kuwa mfano kwa Vijana wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuamua kutumia elimu waliyoipata kwa kujenga chuo kinachohudumia wanafunzi 1700.

Waziri ameyazungumza hayo leo alipokuwa kwenye uwekeji wa jiwe la msingi wa Kituo cha Afya kinachojengwa na chuo hicho ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo na kusogeza huduma kwa wakazi wa Tarafa ya Somangila.

Mhe. Jafo amesema kuwa amefurahishwa sana na namna vijana hao walivyoamua kujiwekeza na kwamba watakuwa ni Vijana wa kupewa kipaumbele na Serikali  kwa namna ambavyo wameamua kuunga mkono Juhudi za Rais Dk.John Pombe Magufuli  ya kujenga uchumi wa viwanda.

“Hospitali hiii mnayojenga  itawasaidia wananchi wa maeneo haya kupata huduma lakini pia kuongeza maarifa kwa vitendo kwa wanafunzi wanaosoma hapa, upatikanaji wa ajira  hivyo hongereni sana na nasema kutoka moyoni  nimefarijika” Alisema Mhe. Jafo

Aliongeza kuwa ushirikiano ambao wameingia na nchi ya Poland katika kutekeleza  malengo yao  ni mzuri na usiwe kwaajili ya kujenga kiwanda cha madawa pekee bali iwe hata kwa vifaaa vingine vya Kitabibu vinavyohitajika na kuwasisitiza pia kuwa makini namikataba ya kisheria ambayo wanaingia ili wasije wakapoteza umuliki wao wa kihalali.

Waziri Jafo amesema kuwa Ofisi yake itatoa cheti cha heshima kwa kuwatambua Vijana hao kwa kazi kubwa waliyoifanya kwasababu wamekuwa ni sehemu ya kuongeza ufanisi wa kazi za Ofisi ya Rais Tamisemi na kwamba wamefanya jambo kubwa kwenye Taifa la Tanzania.

Aidha waziri amewaagiza Mkurugenzi na Katibu tawala wa Wilaya kuwasaidia vijana hao kwa lolote wanatalolihitaji kwenye utekelezaji wa mipango yao ili kuwaunga mkono hususani kwenye suala la Ardhi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chuo hicho Bw. Amesema kuwa ujenzi wa Hospitali hiyo umeanza aprili 2019 na kutarajiwa kumalizika Desemba 2019 na baada ya ukamilifu itajulikana kama Kigamboni City Colledge teaching Hospital, ambapo utagharimu kiasi cha Bilioni 2.

Hospitali hiyo itakua na majengo 2 ya wodi ya wazazi,vyumba viwili vya upasuaji,chumba 1 cha wagonjwa wa dharula, maabara ya kisasa itakayokuwan na City scan na MRI na chumba cha kuhifadhia maiti.

Aidha Chuo hicho kinampango wa kujenga kiwanda cha madawa  chenye uwezo wa kuzalisha vidonge Bilioni 3, chupa za sirapu Milioni 400,chupa za infusion Milioni 300 kwa mwaka ifikapo Octoba 2022 ili kuendana na kauli ya Rais kwa kuwa na Tanzania yenye Viwanada, kuzalisha wataalamu na ajira ambapo kiwanda hicho kinatarajiwa kugharimu kiasi cha Bilioni 10.

Wakati huohuo Mhe. Selemani Jafo amewapongeza Viongozi wa Wilaya ya Kigamboni kwa kazi nzuri wanazofanya na kwamba Wilaya ya Kigamboni ianenda vizuri  na anafarijika sana na utendaji wa kazi .

Waziri amesema kuwa Kigamboni ni Wilaya Mpya  na katika Wilaya zilizoanzishwa Kigamboni inaenda vizuri na kwamba miradi ya maendeleo inayotekelezwa inatekelezwa vyema na anamini hata miradi inayotarajiwa kutekelezwa itafanyika vyema pia.






Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa