• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

DC Sara apongeza kamati na uongozi uboreshwaji wa huduma za afya Kigamboni

Posted on: February 12th, 2019

Mkuu wa wilaya ya kigamboni amepongeza ujenzi wa kituo cha afya kimbiji na kutesema kuwa muundo wa majengo kwa kuongeza vyumba sita haufanani  na kituo chochote nchi nzima hivyo kitakuwa ni kituo cha mfano huku akipongeza pia  hatua za ujenzi wa hospitali ya Wilaya iliyoanza kujengwa.

Akizungumza leo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa kituo cha afya kimbiji na hospitali ya wilaya inayojengwa somangila, Mhe.Sara amesema anaishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kuwaboreshea wananchi huduma za Afya hususani kwa  Wilaya hii mpya ya Kigamboni ambayo bado ndio inakua. 

" Nawapongeza kamati na uongozi mzima kwa kufanikisha ujenzi wa kituo hiki ambacho hapo awali kilitaka kuonesha kwamba kigamboni hakuna usimamizi mzuri, majengo yanapendeza huduma zinaboreshwa, tuwahamasishe wananchi kuja kutibiwa hapa lakini pia watumishi wawajibike katika kutunza mazingira haya kwa kupanda miti ambayo mimi nitashiriki kuileta" alisema Mhe.Sara

Aidha akizungumzia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Mhe.Sara amesema  kuwa Kigamboni ni miongoni mwa Halmashauri ambayo imepewa fedha  kiasi cha bilioni 1.5 na kwamba ipo kwenye orodha ya Halmashauri 15 ambazo zimethubutu kuanza ujenzi  kwa haraka na zinafanya kazi vizuri, tofauti na Halmashauri nyingine ambazo bado wanasafisha maeneo na wengine wakihangaika  kutafuta maeneo.

 Hadi kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha afya kimbiji kiasi cha milioni 455 zimetumika ambapo milioni 400 kutoka Serikali kuu na Milioni 55 kutoka Manispaa kwasasa  huduma za uzazi na maabara tayari zimeanza kutolewa.

     Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya unatarajiwa kukamilika june 2019 na majengo yaliyopangwa kujengwa ni utawala, wazazi, OPD,mionzi,maabara, stoo ya dawa na chumba cha kufulia nguo.

                                       

Msafara wa Mkuu wa Wilaya Mhe. Sara Msafiri kushoto ukiongozwa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Dk.Charles Mkombachepa wakitoka kuangalia jengo la m,ama na mtoto kituo cha afya Kimbiji.

Mkuu wa Wilaya kushoto kiongozwa na Mganga Mkuu wakifurahia huduma ya vitanda kwenye jengo la mama na mtoto.


muonekano wa ndani jengo la mama na mtoto

Mganga Mkuu Dk. Charles Mkombachepa kulia akitoa maelezo ya baadhi ya vifaa ambavyo tayari vimeletwa na MSD kwaajili ya kutolea huduma.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sara Msafiri (katikati) akitoa maelekezo ya uboreshwaji wa mazingira ya kituo cha afya kwa kupanda miti na maua.

wataalamu mbalimbali wakiwa wameambatna na Mkuu wa Wilaya wakikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya inayojengwa Kata ya Somangila

mafundi wakiendelea na ujenzi wa msingi jengo la utawala la Hospitali ya Wilaya.

Mkuu wa Wilaya akisoma ramani ya Majengo ya Hospitali ya Wilaya inayojengwa.


Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa