• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

DC Kigamboni atoa siku 30 wawekezaji kuendeleza maeneo yao

Posted on: April 9th, 2018

Mkuu wa Wila ya Kigamboni Mh. Hashimu Mgandilwa ametoa siku 30 kwa wawekezaji ambao  maeneo yao hayajaendelezwa  muda mrefu kuyaendeleza kwani kinyume cha hapo sheria itachukua mkondo wake, huku akiwatoa shaka wawekezaji waliokuwa wamesitisha kuendeleza maeneo yao kwa kuhofia KDA(Kigamboni Development Agency) , na kuwaomba  kuendeleza uwekezaji wao kwani KDA imefutwa.

Akizungumza  ofisini kwake leo  na waaandishi wa habari , Mkuu wa Wilaya amesema kuwa KDA imefutwa na shughuli zote kukasimiwa Manispaa  hivyo kuwatangazia  wale wote waliokuwa wanasuasua kuendeleza maeneo yao  kuwa wanaruhusiwa kuendeleza  kwa kufata utaratibu wa kuwa na vibali na ramani za mipango miji.

" Mnaruhusiwa kuendeleza maeneo yenu  kwa kufuata utaratibu lakini pia wawekezaji waliohodhi maeneo bila kuyaendeleza nimetoa siku 30 kuendeleza maeneo yao kinyume na hapo kwa mamlaka tuliyopewa  tutapendekeza wanyang'anywe na kupewa watu wenye uwezo wa kuyaendeleza"alisema Mkuu wa Wilaya

Akizungumzia ujenzi wa vibali Mkuu wa Wilaya amesema  kuwa kujenga bila vibali ni kinyume cha taratibu  ndio maana ameelekeza  Manispaa kuhakikisha vibali vinapatikana ndani ya siku 5 tangu kuombwa ili kurahisisha upatikanaji wake na kuondoa malalamiko ya wananchi kuhusu kucheleweshewa vibali.

 Kwaupande wa viwanja vilivyopo fukweni (beach plot) Amesema  kuwa ni maeneo ya uwekezaji na sio maeneo ya kujenga makazi kama ambavyo wengine wamefanya na kuwataka waliojenga makazi kuona namna gani wataweza kurejesha maeneo hayo kuwa ya uwekezaji kama yalivyokusudiwa awali.

 Akiongelea ujenzi wa ndani ya mita 60 Mkuu wa Wilaya amaesema kuwa ujenzi wa mita 60 huaruhusiwa sababu ni eneo la wazi hivyo kama mtu atahitaji kujenga anapaswa kufuata taratibu kwa kupata vibali maalumu na ambavyo vitamtaka kujenga majengo ambayo si ya kudumu.

Wakati huohuo Mh.Mgandilwa amewakaribisha wawekezaji kuwekeza kigamboni kwani kuna ardhi ya kutosha na asilimia 60hadi 70 imekwisha pimwa  hivyo wawekezaji wa sekta zote wanakaribishwa kwani miundombinu ya umeme, barabara na maji inaimarishwa katika kuweka mazingira rafiki ya kuwekeza.

Mwisho aliwaasa wananchi kuacha kuwakaribisha wahamiaji haramu na kusema kuwa Tanzania ni sehemu salama wasiingizwe wahamiaji haramu ambao kesho na keshokutwa watakuja kuharibu taswira ya nchi.

 "wahamiaji haramu sio rafiki  kwa maendeleoya nchi, tuendele kuwakataa" alisema Mkuu wa Wilaya

 kwa upande wake Diwani na Mwenyekiti wa Kamati ya uwekezaji Manispaa ya kigamboni Mh. Dotto Msawa  amewahakikishia wawekezaji usalama na kusema kuwa ardhi ya kutosha ipo kwaajili ya uwekezaji hivyo wawe huru kuwekeza katika sekta zote.

 Naye kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni Bi. Nice Mwakalinga amesema kuwa, Manispaa imejipanga kuhudumia wananchi na ipo tayari kutoa vibali ndani ya siku 5 badala ya wiki 2 zilizokuwa zinatumika hapo awali na kuwasisitiza wananchi kufuata taratibu katika kuhakikisha wanapata vibali kwa wakati.

 Amesema kuwa katika kuhakikisha utekelezaji wa mipango miji Halmashauri  kwa bajeti yake ya ndani  imetenga bajeti kwaajili ya kutengeneza mpango mdogo utakao jumuishwa kwenye Master plan ya Mkoa wa Dar es Salaam   ambao unalenga kuendeleza na kupanga mji mdogo wa Kigamboni ambapo kwa sasa upo hatua ya utekelezaji.

Mkuu wa Wilaya amezungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua  maeneo ya uwekezaji yaliyopo pembezoni mwa bahari wiki iliyopita ,yenye lengo la kuimarisha ulinzi na usalama, kuwatambua wamiliki wa viwanja vilivyopo fukweni(beach plots) na kuangalia miundombinu hususani ujenzi wa mita 60 kutoka usawa wa bahari.

.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mh. Hashim Mgandilwa akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake leo

Kaimu Mkurugenzi Bi. Nice Mwakalinga akifafanua juu ya utaratibu wa  utoaji wa vibali vya ujenzi alipokuwa akizungumza na waandshi wa Habari ofisini kwa Mkuu wa Wilaya.


Diwani wa Kata ya Kigamboni na Mwenyekiti wa Kamati ya uwekezaji Manispaa ya Kigamboni Mh.Dotto Msawa akikaribisha wawekezaji kuja kuwekeza Kigamboni kutokana na uwepo wa ardhi ya kutosha.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa