• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

DC Bulembo apiga marufuku ukataji miti na uchomaji wa mikaa.

Posted on: June 9th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Halima Bulembo ameendelea na ziara yake ya kutembelea mitaa kwa mitaa ambapo leo amefika katika mtaa wa Mahenge, Kibungo, Puna na Kwa Moris katika Kata ya Pembamnazi.

DC Bulembo amepiga marufuku ukataji wa miti hovyo na kwenda kuchoma mikaa kwani ni kosa kisheria na ni uharibifu wa Mazingira ambapo amesema iwapo atabainika mtu yeyote kufanya hivyo basi hatua kali kisheria zitachukuliwa juu yake.

Ni marufuku kukata miti, tunatakiwa kutunza mazingira yetu, miti yetu ya asili mnakata na kuchoma mikaa tukikukamata tutakuchukulia hatua kali za kisheria_ "

Pia DC Bulembo ametoa msisitizo kwa Afisa Biashara kuhakikisha wawekezaji wanapokuja kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali ni lazima watoe nafasi za ajira hata za muda kwa wananchi wanaoishi maeneo husika walipowekeza ili pia na wao wanufaike, Aidha amesema Mradi wowote wa Serikali unapofanyika ni lazima Vijana wa eneo hilo wapewe kipaumbele kwenye ajira za muda katika ujenzi wa mradi husika.

Kwa upande mwengine, DC Bulembo amewataka Vijana kuwa waaminifu pindi wanapopata ajira hizo za muda kutoka kwa wawekezaji mbalimbali wanaokuja kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao kwani changamoto kubwa imekuwa ni wizi wa vitendea kazi kama misumari, mbao na mifuko ya cement.

Aidha Meneja DAWASA amesema katika Bajeti inayokuja zimetengwa Km 50 za usambazaji wa mabomba ya maji na katika hizo kwa mtaa wa Kibungo zitafika Km 20 na kazi inaanza rasmi Mwezi Julai mwaka huu, Pia Meneja TANESCO amesema awamu ya pili ya mradi wa Umeme utaanza kutekelezwa Mwezi Julai kwa kufikia mitaa yote ya Pembamnazi ambayo bado haijafikiwa.

Akizungumza kuhusu migogoro ya Ardhi, Afisa Ardhi amesema Manispaa imeanza kutekeleza kwa kuchukua maeneo yote ambayo hayajaendelezwa hivyo kuyapima na kuyatoa kwa Wananchi, Aidha Halmashauri kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi itaanza mchakato wa kupima ardhi na kumilikisha Hati kwa wahusika ili kuondokana na Migogoro ya Ardhi.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa