• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Changamoto za fidia wananchi Somangila na vyoo Shule za Kisota na Tungi zatolewa ufafanuzi

Posted on: August 22nd, 2019

Katika kukamilisha ufungaji wa mwaka wa fedha 2018/2019 ulioisha june, leo Baraza la Madiwani limeanza kwenye ukumbi wa Kisota Sekonadri kwa kujadili taarifa za maendeleo ya Kata kwa kila kata inayounda Halmashauri ya Manispaa ya kigamboni ambapo hoja za changamoto ya matundu ya vyoo shule ya Kisota Sekondari na Tungi  na ulipwaji wa fidia ya viwanja vya somangila kwa wananchi umetolewa ufafanuzi.

Akizungumza kwa niaba ya Madiwani Mstahiki Meya wa Manipaa ya Kigamboni Mhe.Maabad hoja Amesema kuwa mbali na uchanga wa Manispaa lakini miradi ya maendeleo inaenda vizuri isipokuwa kwa deni la wananchi wa Somangila ambalo limerithiwa kutoka temeke linaendelea kulipwa kwa awamu kadri ya mapato yanavyopatikana.

Kaimu Mkurugenzi  Bw.Charles Lawiso amesema kuwa, wananchi wote watalipwa stahiki zao na kwamba malipo yao yaliandaliwa katika mpango wa bajeti changamoto iliyosababisha wasilipwe kwa wakati ni matatizo ya kufungwa kwa mfumo wa fedha ambayo yalijitokeza kwenye ufungaji wa mwaka wa fedha 2018/2019.

Akizungumia changamoto ya vyoo  kwa niaba ya Mkurugenzi  Kaimu Muhandisi kutoka Manispaa ya Kigamboni Bi. Paskazia Tibalinda amesema kuwa  Kisota mkandarasi anamalizia marekebisho ambayo anafanya lakini wakati huohuo vyoo vilivyokamilika Mwalimu mkuu ameandikiwa barua kuanza kutumia vyoo hivyo  ili kupunguza changamoto wakati wanasubiri ukamilishwaji wa vyoo vingine.

Aidha ameongeza kuwa  wakandarasi wote wa Kisota na Tungi wameandikiwa barua ya kuhakikisha wanakamilisha kazi wanazopaswa kufanya kwa wakati  kinyume na hapo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao ikiwemo kukatwa fedha zao za muda wa uangalizi wa mradi (retention).

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya Bw. Abasi Seleman amelipongeza Barazala Madiwani  na wataalamu  kwa namna ambavyo wamekuwa wakisimamia miradi ya maendeleo , na kushauri kuhakikisha changamoto za vyoo zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati na wananchi  wanatatuliwa changamoto zao.

Baraza la Madiwani limeanza leo kwenye ukumbi wa Kisota Sekondari ambapo kesho kutakuwa na uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji  kutoka kwa Mkurugenzi , taarifa ya Mwaka na uchaguzi wa Naibu Meya na wenyeviti wa Kamati za kudumu.


Kaimu Mkurugenzi Bw. Charles Lawisso akifafanua ulipaji wa fidia kwa wananchi wa Somangila


Wajumbe na wageni waalikwa wakifuatilia Taarifa za Kata zinazowasilishwa na Madiwani.

DIwani wa Kata ya Mjimwema  Mhe. Selestine Maufi akitoa hoja ya changamoto ya vyoo Kisota Sekondari leo kwenye baraza.

Baadhi ya Watumishi wakifatilia baraza

Waheshimiwa Madiwani wakifatilia Taarifa za Maendeleo ya Kata ya Somangila

Diwani wa Kata ya Somangila Fransis Masanja akiomba ufafanuzi wa malipo ya wananchi wanaodai fidia ya Viwanja Somangila.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya  Bw. Abasi Seleman akipongeza Baraza na watendaji kwa kazi wanazofanya.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa