• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

"Asante NMB, tunaomba muendelee kutushika mkono Kigamboni" DC Fatma

Posted on: September 7th, 2021


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangassa amewashukuru NMB kwa msaada wa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya M.25 walivyotoa katika  Hospitali ya Wilaya ( mabenchi 50 ya kupumzikia wagonjwa) , Madawati 50 shule ya msingi Ungindoni , mabati 200 Shule ya Msingi Rahaleo na mabati 180  Sekondari ya Kigamboni ikiwa ni sehemu ya kurejesha faida kwa jamii.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mkuu wa Wilaya amesema vifaa walivyovitoa vitasaidia kuboresha utoaji huduma na kitendo cha NMB kuichagua Kigamboni  kimeonesha ushirikiano mzuri walionao kwani wangeweza kwenda kwingine sababu wahitaji ni wengi.

Ameongeza kwa kusema kuwa changamoto haziishi  lakini tunaowajibu wa kuhakikisha tunatatua moja moja kwa kadri nafasi inapopatikana hivyo, amewaomba NMB kuendelea kuishika mkono Kigamboni katika kusaidia juhudi za Serikali za kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.


Wakati  huohuo amewataka wahudumu wa afya na walimu wa shule waliopokea vifaa kuhakikisha wanavitunza na kutumia kadri ya mahitaji ili kuwapa morali NMB na wadau wengine kuendelea kuiona Kigamboni inastahili kupewa kipaumbele katika kuunga mkono juhudi za maendeleo.


Mstahiki Meya wa Manispaa Mhe. Ernest Mafimbo amewashukuru NMB kwa niaba ya wananchi na kusema kuwa Serikali haina uwezo wa kutatua changamoto zote kulingana na ufinyu wa bajeti hivyo wanapotokea wadau kama NMB inakuwa inaisaidia katika utoaji huduma bora.


Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam  Donatus Richard ameishukuru kigamboni kwa ushirikiano na kuwatambua kama wadau wa maendeleo  na kusema kuwa kila mwaka imekua ikitenga 1% kwaajili ya kurudisha faida kwa jamii na wamelenga maeneo ya afya, elimu na majanga yasiyotegemewa.

Ameongeza kuwa kwa mwaka uliopita walitenga  zaidi ya Bilioni 2 ili itumike katika kurejesha kwa jamii , kigamboni ni jamii yao na wamekuja  kuadhimisha rejesho kwa jamii kwani hawawezi kuendelea kama jamii haipo.


Mkuu wa Wilaya Mhe. Fatma Almasi Nyangassa akiwashukuru NMB kwa kuamua kuifanya Kigamboni kuwa sehemu ya upokeaji wa faida kwa jamii.


Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam Donatus Richard na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangassa wakizungumza wakati wa makabidhiano ya madawati ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Ungindoni.


Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Fatma Almasi Nyangassa akielezea namna mabenchi yaliyotolewa yataziba nafasi zilizokuwa zinawafanya wagonjwa kusimama wakingoja huduma.


Viongozi wakiwa kwenye picha ya pamoja Mara baada ya kukabidhiana mabenchi ya kuketia wagonjwa pindi wanaposubiri huduma



Mstahiki Meya Manispaa ya Kigamboni Mhe.Ernest Mafimbo akishukuru NMB kwa niaba ya wananchi kwa msaada wa vifaa walivyovikabidhi.


Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam Donatus Richard akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa  ikiwa sehemu yao ya kurejesha faida kwa jamii.


Baadhi ya madawati yaliyotolewa.



Mkuu wa Wilaya Mhe.Fatma Almas Nyangassa kulia na Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam Donatus Richard wakikabidhiana mabenchi ya kupumzikia wagonjwa wakati wanangoja huduma.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa