Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe @dalmia amewataka wafanyabiashara wote ndani ya Manispaa ya Kigamboni kupanga bidhaa zao kwa kufuata utaratibu mzuri ili kuiweka Wilaya ya Kigamboni katika hali ya usafi na kuepuka magonjwa ya mlipuko yanaweza kuibuka kutokana na uchafu.
Mhe Dalmia ametoa agizo hilo leo Novemba 25. 2025 katika kikao chake na viongozi wa Taasisi za Serikali, viongozi wa makundi mbalimbali ya kijamii pamoja na wadau wa Mazingira kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi yake kwa lengo la kujadili maswala mbalimbali ya kiusalama pamoja na hali ya usafi wa mazingira.
Akizungunza katika kikao hicho amezitaka wakala wa barabara Tanzania (TANROAD) pamoja na wakala wa barabara Mjini na vijijini (TARURA) Wilaya ya Kigamboni kuhakikisha wanafanyausafi kwenye barabara wanazozisimamia huku akiwataka kutekeleza majukumu yao kwa weledi.
Aidha amewataka viongozi wa makundi ya kijamii kama vile Bodadoda na Bajaji, Daladala, Machinga, Mama na Baba lishe kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri wa kushughulikia changamoto za wanachama wao na sio kukimbilia Serikalini ili kutoa malalamiko.
Kikao hicho ni mfululizo wa ratiba ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni aliyoiweka ili kukutana na viongozi pamoja na makundi mbalimbali kwa lengo la kutoa maelekezo.
Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni
Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam
Simu: +255222928468
Simu ya Mkononi: +255222928468
Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz
Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa