• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGAMBONI

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Care Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Elimu ya awali na Msingi
      • Kilima mifugo na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Mipango na uratibu
      • Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu
      • Viwanda biashara na Uwekezaji
      • Miundombinu ,Vijijini na Mjini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa jamii na Lishe
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
        • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa ndani
      • Usimamazi wa Manunuzi
      • Maliasili na uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na uhasibu
      • Usimamizi na usafi wa Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Uvuvi
    • Elimu
    • Utumishi
    • Huhuma za Kisheria
    • Usafi wa mazingira na udhibiti wa taka ngumu
    • Michezo na Sanaa
  • Madiwani
    • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
      • Huduma za jamii
    • Ratiba za Vikao
      • Vikao vya Waheshimiwa
      • Kuonana na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
      • Miradi ya Sasa
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha
    • Hotuba
    • Gazeti la Mtandaoni
    • Vipeperushi
  • Mifumo

Soko la Tundwi Songani lazinduliwa rasmi

Posted on: March 24th, 2018

Wananchi wa mtaa wa Tungwi-Songani Kata ya Pembamnazi Manispaa ya Kigamboni wametakiwa kutunza miundombinu ya soko ili soko liweze kudumu kwa muda mrefu na kunufaisha wananchi wote kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa ijumaa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh.Maabadi Hoja alipokuwa akizindua mradi wa soko hilo lililojengwa Mtaa wa Tundwi-Songani , alisema kuwa mradi huu umenza ujenzi muda mrefu tangu mwaka 2002, hivyo tunatarajia ukamilikaji wake utaleta maendeleo kwa wananchi wote wa Tundwi Songani na jamii nzima ya Kata ya PembaMnazi hivyo ni muhimu kuhakikisha unatunzwa.

Alisema kuwa ulinzi uimarishwe wa miundombinu na kuhakikisha lengo lililokusudiwa la kuboresha mazingira na utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara na wananchi wa Tundwi na kata ya Pemba Mnazi kwa ujumla linafikiwa.

Akitoa taarifa ya mradi Mratibu wa TASAF Manispaa ya kigamboni Bi.Janet Kacholi alisema kuwa, mradi wa soko ni miongoni mwa miradi iliyoibuliwa na wananchi kupitia program ya TASAF, ambapo umelenga kutoa ajira kwa vijana kwa kupata fursa ya kuuza mazao mbalimbali na kuiwezesha Serikali kupitia Halmashauri kukusanya mapato kutokana na ushuru mbalimbali utakaotozwa kwa wafanyabiashara.

Aliongeza kuwa hadi kukamilika kwa ujenzi wa soko hilo jumla ya Tsh.91,858,842.24 zimetumika ambapo wananchi wamechanga kiasi cha Tsh.34.040.427.27 mchango wa TASAF ni Tsh.26,416,827.27 na Halmashauri ya Manispa ya kigamboni imetoa Tsh.31,401,587.7 ambazo zimekamilisha ujenzi wa meza za ndani baada ya Halmshauri ya Temeke kushindwa kutoa fedha za ukamilishaji kama ilivyoahidi wakati wa uibuaji wa mradi kabla ya kugawanywa.

Soko lipo tayari kwa matumizi ambapo vizimba /meza 60 sawa na wafanyabiashara 60 wataweza kufanya biashara ndani ya soko hilo na eneo la nje kuzunguka soko linakadiriwa kuchukua wafanyabisahara 80 ikiwa watapangwa na kusimamiwa vizuri.

Aidha Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Tundwi Bw. Mikdadi Simba alisema kuwa wananchi wamelipokea soko kwa mikono miwili na litawaletea maendelo kwa sababu wataweza kufanya biashara kisasa zaidi kwa kuzingatia mji unapanuka.

Mfanyabiashara Rehema Kambi amesema tunashukuru kwa mradi huu wa soko kwani tunauhakika wa usalama wa bidhaa zetu hazitaweza kuharibiwa kwa mvua kama kipindi cha nyuma hivyo tunaomba Manispaa ituletee miradi mingine mizuri zaidi ya huu.

Mwenyekiti wa mtaa wa Tundwi Bw.Rajabu Kihimbo aliongeza kuwa anaiomba manispaa ione namna ya kuwasaidia kwenye suala la umeme ili waweze kuimarisha ulinzi na wafanyabiashara waweze kufanya biashara hata nyakati za usiku.

Uzinduzi wa soko umekuja mara baada ya kukamilika kwa ujenzi uliohusisha awamu mbili awamu ya kwanza ikiwa ni ujenzi wa jengo la soko , vyoo na nyumba ya kuhifadhia vifaa mbalimbali na awamu ya pili ujenzi wa vizimba.

muonekano wa soko kwa nje.

Mratibu wa TASAF Manispaa ya Kigamboni Bi.Janet Kacholi akisoma taarifa ya mradi wa soko.

Baadhi ya wananchi waliofika kushiriki uzinduzi wa soko

Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh.Maabadi Hoja akizindua soko kwa kufungua kibao chenye maandishi ya uzinduzi wa soko hilo.

Meya wa Manispaa ya kigamboni Mh.Maabadi Hoja akisoma maandishi ya kibao cha uzinduzi mara baada ya kuzinduz kwa kutoa kitambaa.

Mathiki meya na wananchi wakisoma maandishi ya kibao cha uzinduzi wa soko hilo.

Mstahiki Meya Manispaa ya Kigamboni Mh. Maabadi Hoja akikata utepe ishara ya uzinduzi wa soko na wananchi wakishuhudia

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh.Maabadi Hoja akikagua soko kwa ndani pamoja na wananchi.

Mastahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mh. Maabadi Hoja akizungumza na wananchi wa Tundwi Songani mara baada ya kuzindua soko.

Mwananchi wa Tundwi Bi.Rehema Kambi akishukuru uongozi wa manispaa kwa kufungua soko hilo litakalowasaidia kuhifadhi mazao yao katika hali ya usalama.


Meya wa Manispaa ya kigamboni akiwa ameambatana na wananchi  wakitoka eneo la soko mara baada ya uzinduzi.

Mweyekiti wa mtaa wa Tundwi akitoa shukurani kwa kuzinduliwa soko ambalo litawasaidia wananchi

Meya wa Manispaa ya Kigamboni akisalimiana na mwananchi mara baada ya kumaliza uzinduzi.


Mzee Omary Shomvi mkazi wa mtaa wa Tundwi akisisitiza uongozi wa Manispaa kuwek umeme kwenye soko kwaajili ya kuimarisha usalama.

Matangazo

  • Tangazo la Frem za Biashara, Soko la Kibada February 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye usaili nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi February 24, 2025
  • Tangazo la uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Afya March 26, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini nafasi ya mwendesha mashine ya Bayometriki na Mwandishi msaidizi March 12, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE. DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AMEWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIBADA - MWASONGA

    April 25, 2025
  • MANISPAA YA KIGAMBONI IMEPOKEA VITI MWENDO 35 NYENYE THAMANI YA TSH MIL 8

    April 08, 2025
  • MKANDARASI TOKA SUMA JKT ATAKIWA KUANZA MAPEMA MAANDALIZI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA CHA TUNGI

    April 08, 2025
  • Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele amefanya ziara ndani ya Manispaa ya Kigamboni

    March 22, 2025
  • Angalia Zote

Video

Makala maalumu ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Kigamboni
Video zingine

Kurasa za karibu

  • Municipal councilors
  • Kigamboni Municipal History
  • Investment Opportunities
  • Fomu ya Maombi ya Kiwanja
  • Huduma za Afya na Orodha ya Vituo vya kutolea Huduma za Afya

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni

    Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam

    Simu: +255222928468

    Simu ya Mkononi: +255222928468

    Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa