Kigamboni Shule ya Sekondari ni shule mpya kwenye Kata nzima ya Kigamboni , kata ya Kigamboni haijawahi kuwa na shule ya Sekondari tangu kuanzishwa kwa Manispaa. Hadi kukamilika kwa ujenzi huu kiasi cha milioni 317 kinatarajiwa kutumika, Ambapo Serikali kuu imetoa fedha kiasi cha milioni 100 kutoka kwenye mfuko wa malipo kulingana na matokeo ( PAY FOR RESULTS EP4R) Kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni imetoa fedha kiasi cha milioni 217 kutoka kwenye mapato yake ya ndani ili kukamilisha ujenzi huo.
Aidha kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Manispaa ya Kigamboni imetenga kiasi cha shilingi milioni 100 kwaajili ya kumalizia miundombinu ya vyoo, samani na ofisi z awali za waalimu zitakazowawezesha kuanza kazi mwakani.
Ukamilikaji wa jengo hilo la shule kutasaidia wanafunzi wa Kata ya Kigamboni wanaofaulu kujiunga na Kidato cha kwanza kupata shule ya karibu ya kujiunga nayo na hivyo kupunguza umbali mrefu kufata shule walizopangiwa waliokuwa wanaoupata hapo awali kabla ya kutokuwepo kwa shule hiyo.
Shule mpya ya Kigamboni Sekondari inatarajiwa kuanza kuchukua wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanzia Januari 2020
Muonekano wa Jengo kwa mbele | Muonekano wa jengo kwa upande |
Gezaulole Kata ya Somangila, Kigamboni
Anuani ya Posta: 36009 Dar es Salaam
Simu: +255222928468
Simu ya Mkononi: +255222928468
Bara pepe: info@kigambonimc.go.tz
Haki MilikiĀ©2017 Manispaa ya Kigamboni . Haki zote Zimehifadhiwa